k majaliwa
Senior Member
- Jul 31, 2017
- 140
- 187
Naamini mko poa.
Niende kwenye mada moja kwa moja.
Nilikuwa na mpenzi ambaye tulikuwa tunapendana sana. Nilikutana nae jijini Mwanza nilipokwenda kikazi July 2015.
Safari yetu ya mapenzi ilipamba moto kila mmoja akiwa na mapenzi ya dhati kwa mwenzio.
Tukiwa tumekubaliana kufunga ndoa hapo baadae. Tulifanya mambo mengi pamoja ikiwa kujenga nyumba na kununua gari pamoja, pia niliweza kufanikiwa kumuhamishia Moro kikazi angalau awe karibu.
Hatukuwa wa imani moja, yeye alikuwa mkristo na mimi muislam lkn hili halikuwa tatizo la kutuzuia kupendana.
Tulitembeleana na kuwasiliana Mara kwa Mara bila kikwazo.
Baada ya kumwambia kuwa wakati umefika tuanze taratibu za kufunga ndoa tulikubaliana kuwa ndoa tutafungia serikalini lkn kila mtu atabaki na imani yake.
Alipowaeleza wazazi wake utofauti wa imani wazazi walilipinga kwa nguvu zote, nikamuuliza yeye mwenyewe anasemaje akajibu ananipenda na asingetamani tuachane lkn pia hawezi kufanya kinyume na wazazi wake.
Basi wakati tunaendelea kulitafakari hilo mwenzangu akabadilika, nikimpigia simu anakata meseji hajibu, baadae akaniblock kabsa.
Kitendo kile kiliniumiza sana, nikaamua kumfuata Moro nikakuta alipokuwa anaishi amehama, kwasababu nilikuwa najua shule aliyokuwa anafundisha nikaamua kumfuata shuleni.
Nilipofika shuleni sikuamini kile nilichojimbiwa...niliumia sana..nikamsihi na kumpigia magoti mbele ya walimu wenzie lakini yeye akanijibu hatoweza kuendelea na mimi tena kwani tofauti za dini hazivumiliki , pia kaendelea kusema kuwa alikuwa na mpenzi wake zamani walipotezana lakini wamekutana tena na kuamua kurudiana.
Maneno yale yalikuwa ni mkuki ndani ya moyo wangu, nillilia kama mtoto, sikuweza kula kwa siku kadhaa.
Nikaamua kujiua maana nilijisemea moyoni sitaweza kumuona mwanamke ninampenda akiolewa na mwanaume mwngine. Lkn nilikuwa nao wakanisihi nisifanye vile. Sikujua nini cha kufanya nilikuwa mtu wa kulia tu.
Sikwenda kazini kwa siku mbili mpaka rafiki yangu ambaye tunafanya nae kazi alipofanya kazi ya ziada.
Baada ya mwezi kupita nilifunga safari tena kumfuata nikiwa na lengo la kutaka kujua kuhusu gari na nyumba ambavyo tulinunua pamoja na vyote vilibaki kwangu.
Alichonijibu nikwamba vyote ameniachia kwasababu alichonitendea anajua kiliniumiza sana. Nikwamwambia achukue gari mimi nimeshapona na sina amani kumiliki Mali ambazo tulichuma pamoja akakubali nikamuachia gari .
Utendaji wangu wa kazi ukawa mbovu sana maana kila nilipokumbuka sikuweza kufanya chochote. Nilikuwa nafanya kazi kwenye NGO ya wa Marekani, kufuatia kuwa na ufanisi mbovu kazini nilisitishiwa mkataba wa kazi.
Mapenzi yanauma sana jamani usiombe ukimpenda mtu halafu akakuzingua.
Hapo ndipo shida ikazidi kuwa kubwa maana sikuwa na cha kunikeep busy ikafika wakati nikawa napoteza mpaka fahamu.
Wazazi walipofahamu shida yangu wakanitumia mtu wa kuwa nae maana nilikuwa naishi peke yangu. Hali ile ilinichukua miezi saba ndipo niliporudi normal. Baadae Mungu akajalia nikapata kazi sehemu nyingine.
Maisha yakaendelea tatizo ikawa ni ile nyumba kila nikiona namkumbuka , nikaamua kuiuza na kujenga sehemu nyingine. Maisha yakaendelea nikamtoa moyoni kabisa nikawa namuona wa kawaida sana. Baada ya mwaka mmoja kupita akaanza kunitafuta nakuomba turudiane maana jamaa amemtosa na kuoa mwanamke mwngine.
Nimemkatalia mara kadhaa lkn bado ananing'ang'ania , kila nikitaka kumkubalia nakumbuka mateso niliyopata kwasababu yake.
Naomba ushauri wenu wakuu nipo njia panda sitaki kuumia tena.
Niende kwenye mada moja kwa moja.
Nilikuwa na mpenzi ambaye tulikuwa tunapendana sana. Nilikutana nae jijini Mwanza nilipokwenda kikazi July 2015.
Safari yetu ya mapenzi ilipamba moto kila mmoja akiwa na mapenzi ya dhati kwa mwenzio.
Tukiwa tumekubaliana kufunga ndoa hapo baadae. Tulifanya mambo mengi pamoja ikiwa kujenga nyumba na kununua gari pamoja, pia niliweza kufanikiwa kumuhamishia Moro kikazi angalau awe karibu.
Hatukuwa wa imani moja, yeye alikuwa mkristo na mimi muislam lkn hili halikuwa tatizo la kutuzuia kupendana.
Tulitembeleana na kuwasiliana Mara kwa Mara bila kikwazo.
Baada ya kumwambia kuwa wakati umefika tuanze taratibu za kufunga ndoa tulikubaliana kuwa ndoa tutafungia serikalini lkn kila mtu atabaki na imani yake.
Alipowaeleza wazazi wake utofauti wa imani wazazi walilipinga kwa nguvu zote, nikamuuliza yeye mwenyewe anasemaje akajibu ananipenda na asingetamani tuachane lkn pia hawezi kufanya kinyume na wazazi wake.
Basi wakati tunaendelea kulitafakari hilo mwenzangu akabadilika, nikimpigia simu anakata meseji hajibu, baadae akaniblock kabsa.
Kitendo kile kiliniumiza sana, nikaamua kumfuata Moro nikakuta alipokuwa anaishi amehama, kwasababu nilikuwa najua shule aliyokuwa anafundisha nikaamua kumfuata shuleni.
Nilipofika shuleni sikuamini kile nilichojimbiwa...niliumia sana..nikamsihi na kumpigia magoti mbele ya walimu wenzie lakini yeye akanijibu hatoweza kuendelea na mimi tena kwani tofauti za dini hazivumiliki , pia kaendelea kusema kuwa alikuwa na mpenzi wake zamani walipotezana lakini wamekutana tena na kuamua kurudiana.
Maneno yale yalikuwa ni mkuki ndani ya moyo wangu, nillilia kama mtoto, sikuweza kula kwa siku kadhaa.
Nikaamua kujiua maana nilijisemea moyoni sitaweza kumuona mwanamke ninampenda akiolewa na mwanaume mwngine. Lkn nilikuwa nao wakanisihi nisifanye vile. Sikujua nini cha kufanya nilikuwa mtu wa kulia tu.
Sikwenda kazini kwa siku mbili mpaka rafiki yangu ambaye tunafanya nae kazi alipofanya kazi ya ziada.
Baada ya mwezi kupita nilifunga safari tena kumfuata nikiwa na lengo la kutaka kujua kuhusu gari na nyumba ambavyo tulinunua pamoja na vyote vilibaki kwangu.
Alichonijibu nikwamba vyote ameniachia kwasababu alichonitendea anajua kiliniumiza sana. Nikwamwambia achukue gari mimi nimeshapona na sina amani kumiliki Mali ambazo tulichuma pamoja akakubali nikamuachia gari .
Utendaji wangu wa kazi ukawa mbovu sana maana kila nilipokumbuka sikuweza kufanya chochote. Nilikuwa nafanya kazi kwenye NGO ya wa Marekani, kufuatia kuwa na ufanisi mbovu kazini nilisitishiwa mkataba wa kazi.
Mapenzi yanauma sana jamani usiombe ukimpenda mtu halafu akakuzingua.
Hapo ndipo shida ikazidi kuwa kubwa maana sikuwa na cha kunikeep busy ikafika wakati nikawa napoteza mpaka fahamu.
Wazazi walipofahamu shida yangu wakanitumia mtu wa kuwa nae maana nilikuwa naishi peke yangu. Hali ile ilinichukua miezi saba ndipo niliporudi normal. Baadae Mungu akajalia nikapata kazi sehemu nyingine.
Maisha yakaendelea tatizo ikawa ni ile nyumba kila nikiona namkumbuka , nikaamua kuiuza na kujenga sehemu nyingine. Maisha yakaendelea nikamtoa moyoni kabisa nikawa namuona wa kawaida sana. Baada ya mwaka mmoja kupita akaanza kunitafuta nakuomba turudiane maana jamaa amemtosa na kuoa mwanamke mwngine.
Nimemkatalia mara kadhaa lkn bado ananing'ang'ania , kila nikitaka kumkubalia nakumbuka mateso niliyopata kwasababu yake.
Naomba ushauri wenu wakuu nipo njia panda sitaki kuumia tena.