Siku ya kweli aliyokufa Mwl J K Nyerere

Ukweli hauwezi funikwa siku zote. Ni kama kuuzuia moshi kwa kawa.

Kama vile kuvuja kwa taarifa za mipango na utekelezaji wa kumwua Nyerere kulivyokuwa, kisha kuibukia 2012 kwa uwazi zaidi. Ndivyo tarehe rasmi ya kufariki inapojulikana.

Nyerere alifariki tarehe 7 Oktoba 1999.

Tarehe nyingine ni danganya toto. Ukweli unasema, huwezi kuwadanganya watu wote kwa nyakati zote. Ndicho serikali iliyoongozwa na B W Mkapa ilichofanya.


KWA HIYO????!!!!!!!!

Acha uchochezi, haifai namna hii.
 
Jamani haya ni mambo magumu sana na siyakuzungumza kirahisi tujaribu kuajadili mambo yatakayo tusaidia. Kupoteza muda kwa hasara ni kukosa hekima.watanzania sasa tuombeni hekima kwa mungu tujaliwe kama mfalme seleimani!!!!!

Sijui kama nitakuwa nimekuelewa tofauti, ina maana kuliongelea hili la tarehe halisi ya kifo cha Mwalimu ni kukosa hekima? Kama ndivyo hebu fikiri busara iliyopo kwa kuambiwa uongo kwa miaka 13 sasa, nawe kuendele kuwaaminhsha hivyo wenzako. Kwa miaka 13 serikali imewadanganya watanzania, ndiyo hekima unayoiita ya mfano wa Mfalme Solomon mwana wa Daudi?

Umewahi kufikiri ni hasara kiasi gani imekwasha patikana kwa watanzania kutokuambiwa ukweli? Kujadili ukweli ulifichwa kwako unaona ni hasara kubwa?
 
Mkuu Mwalufunamba,

1. What is your definition of Death?

2. Kwa ushahidi/vielelezo gani unaweza kutupa ili nasisi/namimi niamini kama wewe?

3. Why now? Ni kwanini kwa taarifa yako uwe nayo kwa muda sasa, na uiibue sasa?

4. Tukishajua kuwa kuwa ni tarehe halisi unataka iweje?

5. Mimi naweza kumuangalia Hayati Mwl J.K Nyerere kama Baba wa Taifa, lakini wapo wanaomuangalia pia kama Marehemu Mume na aliyekuwa baba wa familia, Je, wao wanasemaje kuhusu kauli yako?

Ninavyokumbuka, gazeti la majira la Oct 12, 1999, liliandika:
"Mwalimu Ubongo Umekufa"
Nikiwa mwanafunzi wa Sayansi kipindi hicho, nilitambua kuwa Brain death means absolute death of a being, maana ubongo ndo unaendesha kila kitu mwilini, hadi moyo(hata km utausukuma kwa mashine).
Hivyo kwangu, Mwl alishakufa tangu Oct 11 na kurudi nyuma.
Tulikuwa tunaandaliwa kisaikolojia kupokea msiba ule mkuu!
 
Source please

Hata kama nikikwambia chanzo ni Mama Maria Nyerere, si utasema huyo bibi sasa uajuza unamjia vibaya. Oooh! Alikuwa wapi miaka yote hiyo, kwanini alikubali Serikali iseme uongo juu ya kifo cha Mwalimu; na maneno kadha wa kadha, ilimradi kwamba yeye(bibi) aonekane mkosaji ...ajabu anayefunguka katika ukweli anaoneka mkosaji sana...lakini anayeuficha huyo ndiyo mtu mzuri. Duh!!

Tulia na endelea kusoma tu, utaujua ukweli.
 
KWA HIYO????!!!!!!!!

Acha uchochezi, haifai namna hii.

Tafadhali, naomba unipatie tafsiri ya kisheria ya neno ulilotumia na kuonyesha kimuktadha kwamba kile nilichoandika kinawachochea watu. Kama ukishindwa naomba unitake radhi peupe yaani kwa uwazi hapa hapa.

Vinginevyo nitawaomc moderators waingilie kati kuchukua hatua dhidi yako.
 
Matukio tata kabla ya Kifo chake kutangazwa:
Barabara ya kutoka Mgulani JKT na ya uwanja wa taifa hadi keko zilitengenezwa usiku wiki moja kabla kifo chake kutangazwa rasmi. Kigunge alipotoka Uingereza (kabla ya kifo kutangazwa) alikwenda moja kwa moja Butiama.

Mkuu, unakumbuka barabara ya Musoma -Butiama ilianza kutengenezwa lini? Halafu fikiri utaratibu wa kuzichomoa pesa za serikali kwa shughuli hiyo zilianza lini.

Kama haitoshi hebu tujiulize nini kilitokea ama kusemwa tarehe 7 Oktoba 1999. Kingunge si wakuaminika Mar Kawawa labda, lakini hayupo. Mama Maria, Rosemary na Charles wanaweza kusema kitu lakini kabla hawajasema tujiulize siku hiyo walisema nini?

Mazingira ya kuziandaa nyumba za Nyerere, ya Msasani na Butiama, tayari kupokea ugeni yalianza lini?

Mkuu, nimekazia tu kile ulichokieleza.
 
Ukweli hauwezi funikwa siku zote. Ni kama kuuzuia moshi kwa kawa.

Kama vile kuvuja kwa taarifa za mipango na utekelezaji wa kumwua Nyerere kulivyokuwa, kisha kuibukia 2012 kwa uwazi zaidi. Ndivyo tarehe rasmi ya kufariki inapojulikana.

Nyerere alifariki tarehe 7 Oktoba 1999.

Tarehe nyingine ni danganya toto. Ukweli unasema, huwezi kuwadanganya watu wote kwa nyakati zote. Ndicho serikali iliyoongozwa na B W Mkapa ilichofanya.

Kwanini Unatuchosha na HABARI zisizo na UCHUNGUZI ? ZISIZO na UMAANA YOYOTE ? NI UMBEA MTUPU LAKINI na MODS waMEMEACHA HUO UMBEA KUENDELEE NA KUTAMBAA; WAKATI SISI TUKIWEKA HABARI zenye MWELEKEO na UMAANA zinatupwa chini... [ kama ni nchi zilizoendelea Jamii Forums, na Mwandishi wote Mahakamani Sababu ni Umbea wa Jikoni]

* Fafaunua Habari zako kama sio stay safe kama sie Hakuna haja ya kuwa MDODOSA wa Maana... Soma Habari Iliyoandikwa na Mwandishi wa Maana na Iweke kwenye Jamii Forums...
 
Nyerere kafariki, hatunaye tena duniani since oct 1999 KWISHA! Kuanza kujadili mara ooh tarehe sio, ooh hakufa bali kauawa, haisaidii ni kupoteza muda bure! wengine watakuja na POROJO hapa et alikuwa freemasonic member! so that the devils wamemchukua hivyo hajafa bado! HUKU NI KUMDHALILISHA KIONGOZI WETU SHUPAVU! TULIKUWA NAE, AKATANGULIA MBELE YA HAKI, TUKALIA NA SASA CHENYE WAJIBU KWETU NI KUYAENDELEZA MAZURI ALIYOTUACHIA!

Hata tukifanyaje, Nyerere hatoabika. Kinachotokea hapa nikwamba uovu wa viongozi waliomrithi ndio unazidi kua 'UCHI'.
 
Kingunge aliyekuwepo anasema hana dini. Japo najua viongozi wote wakubwa wakifa lazima nchi zimalize matayalisho ya kiuongozi ndo habari zitoke
 
Umekuaje hajafanya research? Binafsi sijui mwalimu alifariki lini ila najua kifo chake kilitangazwa tarehe 14 October. Kama angekuwa amefariki tarehe 14 iweje nyimbo za kina Komba zianze kupigwa radioni immediately dakika chache baada ya Mkapa kutangaza kifo chake?

kwa maana hiyo Komba alijulishwa kifo cha Mwalimu kabla ya Watanzania wote? Anyway hizi ni porojo tu reality ni kuwa mwalimu alikufa na kama taifa tunakubaliana alikufa tarehe 14/10/1999, sasa kama una ushahidi wowote wa kitibabu toka st Thomas tuwekee ili utumike kama ushahidi wa kuisukuma serikali iweke historia na kumbukumbu kuhusu kifo cha mwalimu sawasawa na aliyedanganya taifa awajibishwe!
 

Kwanini Unatuchosha na HABARI zisizo na UCHUNGUZI ? ZISIZO na UMAANA YOYOTE ? NI UMBEA MTUPU LAKINI na MODS waMEMEACHA HUO UMBEA KUENDELEE NA KUTAMBAA; WAKATI SISI TUKIWEKA HABARI zenye MWELEKEO na UMAANA zinatupwa chini... [ kama ni nchi zilizoendelea Jamii Forums, na Mwandishi wote Mahakamani Sababu ni Umbea wa Jikoni]

* Fafaunua Habari zako kama sio stay safe kama sie Hakuna haja ya kuwa MDODOSA wa Maana... Soma Habari Iliyoandikwa na Mwandishi wa Maana na Iweke kwenye Jamii Forums...

Hii ni jamiiforums si journalistforum. Mtu asipaswa kuwa mwanajf isipokuwa kwa concert ya wazazi ni yule mwenye miaka chini ya 18, lakini wengine maadam ni wanajamii wana akili timamu, ruksa kujiunga na JF. Kasome vizuri masharti ya kujiunga na Jf.

Si kweli habari zote nzito humu Jf, toka zama za Jamboforum zililetwa na waandishi wa habari. Jaribu kusoma post za zamaaani zilizopo humu utakubaliana nami na kujua mambo mengi ya ajabu ya kuwa kweli Jf ni kishma cha maarifa na watu wanabishana kwa hoja si wale walio katika payroll ya mafisadi.

Ukitegemea habari za kuandikwa na hao unaowaita "waandishi wa maana" iko siku utabaki mdomo wazi. Unajua Kikwete aliwatumia wakina nani kumpamba yeye na kumshambulia Sumaye akitumia magazeti kama RAI na Majira back to 2005?

Come on!!
 
Back
Top Bottom