Analyse
JF-Expert Member
- Jan 19, 2014
- 17,641
- 47,660
Habari zenu wana MMU.
Binafsi toka nianzage mahusiano sijawahi kuuza mechi.Ila kila nkikumbuka siku ya kwanza naenda kununua condom dukani,basi huwa nacheka sana.Nakumbuka ndio nilikuwa nimemaliza form 4,nipo tu kitaa.Sasa siku hiyo nikapewa ahadi ya kupewa mchezo na binti flani hivi.
Basi nkasema hapa inabidi ninunue kinga siku moja kabla walau niwe nazo karibu tu.Nkasubiria hadi kigiza giza kimeingia,then nkajisogeza hadi maeneo ya dukani (nakumbuka lile duka lilikuwa ni kama mtaa wa 10 hivi kutoka home ).
Nlipofika pale dukani,nakumbuka nlikuta watu kadhaa,ikabidi nitulie pembeni kwanza ili wahudumiwe. Walipoisha nkasogea na mimi. Nilipotaka tu kuelezea shida yangu akaja babu mmoja pale dukani,nkaona soo ikabidi nimpishe ahudumiwe yeye kwanza. (Babu alinishkuru akidhani ni ukarimu kumbe nlikuwa naona aibu mwenzie ).
Babu alipoondoka nkampatia muuza duka hela ila kabla sijamuelezea shida yangu,akaja mama flan hivi pale dukani. Nkamind sana kimoyo moyo nikazidi kuogopa kutaja neno condom mbele ya yule mama (hapo muuza duka kashachukua hela yangu ananiangalia tu).
Nilipoona yule mama haondoki nkamwambia muuza duka nirudishie hela yangu. Jamaa akacheka tu akaingia dukan kwake kama anatafuta kitu then akanipa kibox kimefungwa ndani ya gazeti. Nkabaki namwangalia tu (kimoyo moyo namshangaa huyu jamaa vipi?)
Sema nikarudi nyuma kumpisha kwanza yule mama.Nlipoangalia ndani nikakuta condom,nikasmile kisha nikaondoka.
Toka siku ile,lile ndio likawa duka langu la kununulia ile bidhaa hadi nlipozoea.
Hebu tuelezane wakuu,na nyie mlikuwa mnaona soo kama mimi?
Au nipo peke yangu kwa ili?
Kizzy Wizzy MO11 The Boss mshana jr
Binafsi toka nianzage mahusiano sijawahi kuuza mechi.Ila kila nkikumbuka siku ya kwanza naenda kununua condom dukani,basi huwa nacheka sana.Nakumbuka ndio nilikuwa nimemaliza form 4,nipo tu kitaa.Sasa siku hiyo nikapewa ahadi ya kupewa mchezo na binti flani hivi.
Basi nkasema hapa inabidi ninunue kinga siku moja kabla walau niwe nazo karibu tu.Nkasubiria hadi kigiza giza kimeingia,then nkajisogeza hadi maeneo ya dukani (nakumbuka lile duka lilikuwa ni kama mtaa wa 10 hivi kutoka home ).
Nlipofika pale dukani,nakumbuka nlikuta watu kadhaa,ikabidi nitulie pembeni kwanza ili wahudumiwe. Walipoisha nkasogea na mimi. Nilipotaka tu kuelezea shida yangu akaja babu mmoja pale dukani,nkaona soo ikabidi nimpishe ahudumiwe yeye kwanza. (Babu alinishkuru akidhani ni ukarimu kumbe nlikuwa naona aibu mwenzie ).
Babu alipoondoka nkampatia muuza duka hela ila kabla sijamuelezea shida yangu,akaja mama flan hivi pale dukani. Nkamind sana kimoyo moyo nikazidi kuogopa kutaja neno condom mbele ya yule mama (hapo muuza duka kashachukua hela yangu ananiangalia tu).
Nilipoona yule mama haondoki nkamwambia muuza duka nirudishie hela yangu. Jamaa akacheka tu akaingia dukan kwake kama anatafuta kitu then akanipa kibox kimefungwa ndani ya gazeti. Nkabaki namwangalia tu (kimoyo moyo namshangaa huyu jamaa vipi?)
Sema nikarudi nyuma kumpisha kwanza yule mama.Nlipoangalia ndani nikakuta condom,nikasmile kisha nikaondoka.
Toka siku ile,lile ndio likawa duka langu la kununulia ile bidhaa hadi nlipozoea.
Hebu tuelezane wakuu,na nyie mlikuwa mnaona soo kama mimi?
Au nipo peke yangu kwa ili?
Kizzy Wizzy MO11 The Boss mshana jr