Siku walipokwenda kwa mara ya kwanza gesti

Aiseee... Bitu keshaharibu. Baba Juliana nae...binti aliyemaliza chuo bado tu anamchapa loh
 
NI SHIIDA!-20

ILIPOISHIA

"Mpenzi wangu mbona hupokei simu yangu? Hebu niambie pafyumu yangu ya UDV uliichukua?"
SEREBUKA NAYO SASA...


Bitungu aliendelea kufloo lakini bado upande wa pili hakujibiwa kitu chochote zaidi ya kimya kutanda. Alichokifanya aliikata simu na kuipiga kwa mara ya pili. Napo ikapokelewa tena na kumfanya atabasamu.


"Sweet wangu nitakuchukia? Embu niambie kama nimekuudhi nisamehe jamani bado nakupenda na sitaki kukupoteza hata kidogo!"


Bitungu aliendelea kuchanika maneno ya kimahaba bila hata kujua kinachoendelea upande wa pili. Safari hii aliipoza zaidi sauti yake huku akiwa amejilaza juu ya kitanda cha gesti na kuendelea kutoa sauti ya kubembeleza.


Akiwa katika kubembeleza bila kujibiwa mara akasikia makelele ya majibizano kati ya mume na mke yakiendelea. Akainuka harakaharaka pale kitandani akiwa hajiamini kwa kinachoendelea. Akaisogeza tena simu yake sikioni na kuendelea kusikia majibizano yale.


***Ugomvi uliendelea kuwa mkali kati ya baba Juliana na mkewe. Simu iliyopigwa na maneno yaliyokuwa yakiongelewa yalizidisha hasira za baba Juliana. Alijiangalia mara mbilimbili mwili wake ulivyotota kwa jasho na meno yakiumana kisha akamgeukia mkewe huku akimkazia macho na vidole akimnyooshea.


"Nikisema nianze kukutandika kama mtoto wako huyo nitakuwa nimekosea?"
"Kwani nimekosa nini mume wangu?""Si simu! Unajifanya hujui kinachoendelea?"
"Imefanyaje? Kwani we huwa hupigiwi simu na watu waliokosea namba?"


"Mama Juliana? Hivi ni mtoto gani utamdanganya kwa hiki kinachoendelea kwenye simu?"
"Mume wangu, leo unaonekana kuwa na hasira sana. Hiyo namba kubaliana na mimi kuwa imekosewa na imekuja kwa bahati mbaya.""Nakujisevu imejisevu kwa bahati mbaya siyo!"


"Kwani imejisevuje mume wangu si namba tu imetokea!"
"Batu sijui Bitu! Si umeandika wewe hapa unajifanya hujui siyo?"
Baba Juliana alimsogezea kwa ukaribu mama Juliana na kuanza kumwonyesha jina la Bitu kwenye ile simu yake. Simu haikuwa imekatwa hali iliyomfanya mama Juliana ashtuke na kutaka kuikata lakini baba Juliana akamuwahi na kuusogeza mkono wake pembeni.


"Unataka kufanyaje? Si umesema amekosea! Sasa kuanzia sasa hii namba nakula nayo sahani moja ama zangu ama zake pumbavu!""Msimamo wangu uko palepale mume wangu, siwezi kukusaliti hata siku moja na hiyo namba imekosewa.


Kama ukichukua maamuzi mabaya shauri yako wala usinishirikishe!"
"Nitaelewa tu msaliti ama siyo msaliti ngoja nilifanyie kazi. Kukuachia uhuru na mtoto wako mnautumia vibaya!""Amua utakavyofanya na ukweli utaujua maana nakwambia sijui lolote unaendelea kukazania, amua tu!"


Iliimbidi mama Juliana azuge kuwa amekasirika ili baba Juliana aamini lakini wapi! Ndiyo kwanza baba Juliana aliondoka chumbani mule na kumuacha Juliana na mama yake wakiwa kwenye butwaa. Vita ikaanza upya kwa Juliana na mama yake.


"Halafu wewe mshenzi wewe? Kwanza una bahati sana baba yako kasahau kuhusu pafyumu hii. Haya niambie ukweli umeitoa wapi hii pafyumu ya kiume?""Mama si nilishakwambia kuwa nilijibanabana nikanunua!""Unasemaje? Ukanunua siyo?"


Hasira za mama Juliana zilimwishia Juliana. Tayari alishajiona amempoteza Bitungu kwa jinsi mumewe alivyoondoka kwa hasira akiwa na simu yake mbaya zaidi aliposema atakula nayo sahani moja kuhakikisha anamjua na kumpata. Alimshika Juliana kwa nguvu kisha akamwachia."Nakupa nusu saa, naenda chumbani huko alipo baba yako, nikirudi nataka uiniambie ukweli wote hii pafyumu umeitoa wapi?"


Kitendo cha mama Juliana kuondoka huku nyuma kamwacha Juliana na maswali ya sintofahamu. Cha kwanza mama yake alivyojichanganya kwenye jina la Bitu lililokuwa kwenye simu ya mama yake na pili ni kumjibu mama yake juu ya ile pafyumu alipoitoa.


"Nitamweleza pafyumu ya Bitungu akinipiga namwambia baba ukweli wote hadi nilivyomshuhudia gesti kule Bagamoyo kama kukosa tukose wote tu."Juliana alijiongelea na kujijibu mwenyewe. Aliiweka ile pafyumu pembeni kisha akajipindua pale kitandani na kuanza kuutafuta usingizi akiwa na maswali kibao kichwani.
***
Muda wote Bitungu alibaki na bumbuwazi asijue lipi la kufanya. Maneno ya mwisho aliyoyasikia kwenye simu yalimpagawisha zaidi. "Ina maana atakula sahani moja na mimi? Hapana mimi kidume kwanza atakuwa ni hawara wake tu."


"Lakini bado picha haijanijia! Kweli sweet wangu ndiyo aniingize kwenye matatizo? Na kwa nini simu alimpa mume aipokee kama kweli ananipenda?"Alichokifanya Bitungu ni kutoka moja kwa moja hadi bafuni na kuoga kwa mara nyingine kisha akavaa nguo na kulipia mule gesti na kuondoka.


"Kama anajijua ni mke wa mtu basi na mimi ni mume wa mtu, naenda kuusema ukweli wote kwa huyo mumewe anayetaka kula sahani moja na mimi."

Ukimwaga ugali namwaga mboga, tukutane j5 ijayo.............
 
Asante mkuu Daudi1 mama juliana nimemuaminia ningekuwa mimi pale ningezimia hakyamama
 
Last edited by a moderator:
Asante mkuu Daudi1 mama juliana nimemuaminia ningekuwa mimi pale ningezimia hakyamama
Ashamuona mumewe ----- ndo maana lakin kama angekuwa anamuheshimu mume wake asingepata hata nguvu za kumhoji mwanae kuhusu pafyumu angeenda kuzindukia hospital
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom