Siku moja na Sir Andy Chande

Kwenye video ya Tunda special ya Muumin Mwinjuma yupo Idd Janguo pia na micheni yake kutoka Texas.

Na video za awali za Twanga Haji Janguo naye aliuza fuvu kwenye zile video akiwa na kamarade Ally Choki.
Ama kweli kila kitabu na zama zake,saa hizi ukiyataja hayo majina utaulizwa hao ndio nani?pia kweny enzi hizo alikuwepo marehemu Ipi Malecela ,da jamaa walitikisa Dar na walikula bata sana.
 
Mzee wetu tunashukuru kwa kutupa elimu ambayo wengi hawaijui. Nakuombea kwa Allah( S.W) akuzidishie pale palipopungua. Amina.
 
Mohamed: bahati mbaya (nzuri?) wewe sikujui lakini Janguo na Dau na Chande nawajua. Kama Dau alikukabidhi madaraka itakuwa ni kwa kukupenda mujaheedina mwenziye na si vinginevyo. Cairo Road mlienda kufanya nini?

Directorate ya Marketing nawajua maafisa si china ya 5 waliokuzidi (nasema walikuzidi kwa vile setup yake ninaijua na wewe si mmojawapo. Kwenye ngazi iliyofuata chini yao kulikuwa na wati 17, inawezekana labda umo humo, lakini way way down.

Kwa mdomo wako mwenyewe umesema siku ile (yako na Chande) Janguo aliamua yeye kupresent ripoti ya marketing: ni kwa sababu hakuona mtu. Fani yako wewe ni insurance mambo ya marketing wapi na wapi?
WM
 
William...
Una haraka sana.
Soma maelezo yangu kwa utulivu.

Nimekueleza kuwa idarani tulikuwa watu wawili tu.
Hii ilikwa mwaka wa 1993.

Sababu ndiyo iliyonifanya mimi kukaimu kwani isingewezekana kuacha nafasi bila mtu wa kukaimu.

Hakika mimi nilikuwa Idara ya Insurance lakini nilihamishwa idara hiyo nikapelekwa Idara ya Biashara.

Nikahamishwa tena Idara ya Biashara nikapelekwa Idara ya Masoko.

Hili la mujahid sijui linakuja vipi hapa.
Ikiwa una maana nilipata kazi kwa Uislam wangu basi hii ni barabara ya njia mbili.

Lazima wawepo na wa dini nyingine ambao nao wamenufaika kwa dini yao.

Kuhusu Cairo Road nifafanulie nikupe jibu.
Binafsi nimefika Cairo mara mbili 1988 na 1991 lakini sina kumbukumbu ya mtaa huo.
 
Mzee Chande aliwahi kuwataja wanachama maarufu wa klabu yake. NakumbukaNakumbuka alimtaja pia Mkapa
 
Mzee wangu Mohamed niliwahi kukuomba uandike kidogo tanzia ya sir kahama hujanijibu kabisa
Maishapopote,
Niwie radhi kuwa sijakujibu.
Kuna mambo sharti uyape muda kuyaandika.

Nitakupa mfano.

Daisy Sykes
alipokufa baba yake Abdul Sykes 1968 alitaka kuandika historia
yake.

Mwalimu wake wa historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam John Iliffe alimwambia
hilo ni somo zito linahitaji kupewa muda.

Alimwambia hivi kwa sababu tayari palishatokea maneno kuhusu historia ya TANU.
Kuna watu walikuwa wanajaribu kulifuta jina la baba yake na familia yao katika
historia ya Tanganyika.

Hakutaka Daisy amwage petrol kwenye moto.
 
Ok..lkn kama utaniahidi utaiandika ntashkuru
 
Maudhui ni kwamba ukitumbuliwa usibwatuke na kuropoka we kaa kimya na uangalie una move vipi na kuweka mambo kwenye mstari na hiyo wanaweza watoto wa mjini tu
 
Nikupe pongezi mzee wangu MS kwa historia fupi uliyo tupa kwa jinsi unavyo mfahamu Sir Andy. Nipende kuwaomba wa Jf tutumie fursa hii adhimu kumuuliza mzee wetu Ms mambo Yale tunayo taka kufahamu kwani kwa mtazamo wangu nimendua yapo mengi mazuri anaweza kutujuza.
 
Bandari iliwanufaisha sana watu wa imani ile, kwahiyo hapo Nyerere hakuwa na tatizo.
Huu uzi umeweka wazi mambo mengi sana....ukweli ni kitu cha ajabu. Hakuna anayeweza kuufuta
 
Andy Chande alimwambi Mwl Nyerere "hauwezi kufufua uchumi kwa kutaifisha mali za watu, historia itatuhukumu kati mimi na wewe nani alikuwa sahihi"
Naam historia imehukumu kwa uwazi kabisa Chande alikuwa sahihi.
BURIANI SIR CHANDE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…