William,
Wewe una pupa sana ya kutaka kujibizana na mie.
Unatakiwa kabla hujaandika kitu angalau basi fanya utafiti kidogo wa
somo lenyewe ulijue ndipo unyanyue kalamu.
Kitabu cha
Abdul Sykes cha Kiingereza ndicho kitabu nilichoandika kwanza
na kikapigwa chapa London 1998 baada ya kila ''publisher,'' hapa nyumbani
kukiogopa.
Tafsiri ya Kiswahili ikachapwa Nairobi 2002.
Kuhusu kuwa kitabu kina lugha mbovu huo ni muhali jambo hilo haliwezekani.
Mwandishi ana first class merit pass katika English Oral Cambridge.
Jingine mimi (samahani napiga zumari langu mwenyewe) mtaalamu wa lugha
ya Kiingereza na nipo katika mradi wa Oxford University Press wa kusomesha
Kiingereza Shule za Msingi na Sekondari.
Nimechapa vitabu viwili na Oxford kimoja ni African Anthology: ''The Mermaid
of Msambweni,'' kikijumuisha waandishi kutoka nchi mbali mbali za Afrika na
kingine ''The Torch on Kilimanjaro.''
Hiyo moja.
Pili mswada ulipita miko miwili ya wataalam wa lugha ya Kiingereza kabla ya
kupelekwa Uingereza kwa uchapaji na huko pia ukapitia mkono wa mhariri
mama mmoja Mwingereza Prof. wa African History.
Kwa kawaida mhariri hatakiwi ajulikane na mwandishi.
Huyu mama alipomaliza kuhariri kitabu kile alimpa ''note,'' publisher aniletee.
Katika note ile alinambia kuwa amepata furaha sana kukihahriri kitabu changu
na mwisho akaniambia, ''Mohamed you are a story teller.''
Hapa panatosha.
Kifua chako kinafukuta kwa joto.
Iweje huyu Mswahili apewe hivi vyote.
Unaumia kama wengi walivyoumia.
Nakuongezea jambo.
Kitabu cha
Abdul Sykes kikafanyiwa ''review,'' na mabingwa wa African History,
John Iliffe Cambridge University na
Jonathon Glassman Northwestern University,
Chicago.
Hizi ''review,'' zipo katika Cambridge Journal of African History.
Bila shaka unajua hii nini maana yake.
Huyu
Jonathon Glassman akinletea wanafunzi wake Tanga kunihoji wale ambao
walikuwa wanaandika tasnifu zao za Ph D katika historia ya Tanzania.
Bila shaka unajua hii nini maana yake.
Jonathon Glassman akanialika kuzungumza chuoni kwake Northwestern University
Chicago na nikazungumza katika ukumbi wa
Eduardo Mondlane.
Bila shaka unajua hii nini maana yake.
Ikafuatia na kazi yangu kuchapwa katika Dictionary of African Dictionary (DAB) mradi
wa Harvard na Oxford University Press, New York 2011.
Bila shaka unajua hii nini maana yake.
Sasa ndipo ninapokuhurumia ndugu yangu.
Ikiwa wewe umejenga hoja yako kuwa
Sykes Kiingereza ni tafsiri ya kitabu cha
Sykes
Kiswahili kweli mimi haja ya mimi kukaa kukujibu hayo uliyojenga, Waingereza watasema
katika, ''wrong premise?''
Kukusaidia unijue vyema hebu ingia hapo chini:
Mohamed Said: ''The Torch on Kilimanjaro''
Mohamed Said: KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN BIOGRAPHY (DAB) OXFORD UNIVERSITY PRESS, NEW YORK