William...
Unaandika vizuri na nakuelewa vyema.
Sina sababu ya kusema uongo.
Niliyokueleza ndivyo ilivyotokea.
Si hilo tu.
Nimewahi vilevile kuwa katika ''delegation,'' ya Bandari iliyokwenda Lusaka,
Zambia kuhudhuria mkutano ambao wajumbe ni wakurugenzi.
Kulikuwa na Kamati ikiitwa Transport Coordination Committee ambayo
ilijumuisha THA, TAZARA, TRC na wengine sikumbuki maana miaka imepita
hawa ni watumia bandari na wasafirishaji kutoka Zambia, Malawi na Congo.
Tulikuwa na mikutano tukifanya Malawi na Zambia kila baada ya muda hivi na
ikizunguka kati ya nchi hizo.
Azma ya mikutano hii ilikuwa kujaribu kuleta ufanisi Bandari ya Dar es Salaam
kwa kukutana mara kwa mara na kujadili matatizo ya usafirishaji wa mizigo.
Waliokuwa wanahudhuria vikao hivi katika nchi hizo ni Mkurugenzi Mkuu,
Mkurugenzi wa Masoko na Mkurugenzi wa Utekelezaji.
Ikatokea kuwa Mkurugenzi wa Masoko Dr. Dau alikuwa Ulaya na ofisi ninakaimu
mimi.
Kwa adabu za ofisi nilimpelekea mkubwa wangu taarifa ya mkutano wa Lusaka
na nikamfahamisha kuwa napeleka taarifa kwa ''travel agent,'' atayarishe tiketi yake
ili yeye atue Nairobi na hapo aunganishe ndege moja kwa moja hadi Lusaka badala
ya kuja Dar kwa hofu ya kuchelewa kikao.
Jibu lililokuja kwangu kutoka wa Dr. Dau ni kuwa yeye ofisi ameniachia nakaimu kwa
hiyo nitimize wajibu wangu.
Mimi nilisafiri na wakurugenzi hao niliokutajia hapo juu kwenda Lusaka kwenye
mkutano ule.
Iko picha tumepiga Pomodzi Hotel Lusaka niko bega kwa bega na wazee wangu
wakurugenzi.
Kwako lipi kubwa hili la Chande au hili la Lusaka?
Nina mengi.
Hayo ya kutoeleza utafishaji wa mabenki nisingeweza kuyaandika katika kitabu cha
Sykes kwani si mahali pake.