Siku mchepuko uliponiambia ana ujauzito wangu

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,482
40,494
Ilikuwa kama siku ya alhamisi hivi, mwaka juzi; rafiki yangu mmoja akanipigia simu, na kunijulisha ana ujumbe wangu, nikamuuliza ujumbe gani? akasema kuna dada fulani anakutafuta sana, anasema kwenye simu yako hakupati.

Nikamuuliza ana tatizo gani? akajibu, ''anasema ana ujauzito wako, pia yeye ana mume, na wewe una mke kwa hiyo ni changamoto; pia anahofia mumewe akijua itakuwa tatizo kubwa.'' Nikamuuliza yuko wapi, na anaitwa nani?, aliponiambia jina tu, nikakumbuka kweli nilishakuwa naye kwenye mahusiano.

Basi tukapeana 'appointment' kesho yake tuonane, mida ya saa tatu usiku.

Muda ulipofika nikaenda zangu kwenye eneo la tukio, nikawa napiga mvinyo wangu taratibu. Baada ya kama dakika 20 wakawa wamefika, wadada wawili, pamoja na huyo rafiki yangu.

Tukasalimiana, na mhudumu akaja kuwahudumia.

Kutokana na mbinu nilizozipata jando, kama mwanaume kamili, sitakiwi kumuharasi mtoto wa kike, zaidi ya kumpeti peti tu.

Tukawa tunapiga stori nyingi tu, za kuchekesha ili kumuweka sawa na ajione hakukosea kukutana na mimi; baada ya lisaa limoja na nusu kupita, nikamsogelea mrembo, na mazungumzo yakawa hivi:-

Mimi: Niambie mpenzi wangu, unachangamoto gani?
Yeye : Unajua baby, nina ujauzito wako
Mimi: (Sikushtuka, nikawa nampiga mgongoni kidogo ili aweze kupata joto), Sawa, wewe ulikuwa unatakaje; kwa sababu mimi nakusikiliza wewe, utakachokitaka mimi sitapinga?
Yeye: Mimi nataka nitoe, kwa sababu mume wangu akijua itakuwa tatizo
Mimi: Sawa ata ungetaka kuzaa kwangu haina shida, mi napenda watoto, nami kuwa na watoto wengi ni furaha pia
Yeye: Hapana, itaniharibia ndoa, naomba ukubaliane na maamuzi yangu.
Mimi: Sawa, nakubaliana na maamuzi yako,utakapokwama usisite kunijulisha
Yeye: (Akachukua glass tukagonga 'cheers' akani 'kiss' tukaendelea kupiga mvinyo huku tukiwa na furaha tele, akiwa ananiimbia wimbo fulani hivi wa mahaba)

Baada ya kukaa muda mrefu, tuliagana na wao wakaondoka; baada ya kufika akanipigia simu kwa furaha sana; akanishukuru kwa kumpokea vizuri, kwa sababu alikuwa akihisi labda ningemtukana au ningekataa huo ujauzito.

Akasema ''Equation x, you are a real gentleman''
 
Back
Top Bottom