Tonge
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 695
- 12
Nimewaza sana kuhusu ndoa za siku hizi zinagharama kubwa lakini utakuta watu wamekua BF na walikuwa wanachengana kwa miaka saba au zaidi. Zamani zile mke na mume wanaoana bila hata kukutana kimwili na ni lazima kitambaa chenye damu kitoke chumbani siku ya harusi kiende hadharani watu waone na kushangilia sana, mi si wa zamani sana ila nilishuhudia moja, hii ina maana kuwa enzi hicho bikira ni kitu cha dhamani sana.Je miaka hii yapo hayo? ndio maana nasema tunapasha kiporo moto maana kila kitu tumemaliza hata ile bikira ya nyuma utakuta haipo. Je mahali iwe kubwa na gharama kubwa za kuandaa harusi za nini?. Naomba maoni yenu wanaJF.