Hamuwezi kuchukua nchi hii bado sana CDM. Ni chama cha kichanga sana. Viongozi wenu wengi wao ni wakabila, wadini na wakanda sana. Hiki chama ni Kama chama cha ukoo mfano Lissu yupo na dada yake bungeni, Lema yupo pia na dada yake, Mtei kaweka mkwe wake kabisa kukata mzizi wa fitna yaan Hiki chama Hiki mmmmmh mmmh
Ni kweli kabisa, sababu zipo wazi sana kwa mwenye akili, vyama wakati vinaanza, vinaanza na wanadungu wengi kuliko wanachama wa koo mbalimbali, ni hali ya kawaida kwa chama kinachooanza, kwa CDM hali ni hiyo hiyo, wanaanza wanaukoo, kwa koo kama hamsini hivi harafu wengine wanajiunga polepole tena kuwa kufuata katiba na mafanikio yanayopatikana. AIBU NI KWA CCM yenye zaidi ya miaka 59 tangu TANU, ambapo mpaka leo majina ni yaleyale ya koo zile kama 8-50 tu, Nape na Baba yake, Mwinyi na Wanae, Msuya na Mwanae David, Kikwete na Mkewe na Mwanae Rz1, Karume na Wanae, Mzindakaya na Mwanae huko Busega, Makamba na Mwanae January, Kawawa na Wanae Vita na dada yake, majina ni mengi sana kwa CCM. ukilinganisha after 50 years bado koo ni zile zile na watumwa wao, huwezi kusema CDM ni ya familia au koo au kabila, inamiaka pungufu ya 25 nusu ya CCM. AIBU YA CHAMA KUWA CHA WATU WALEWALE NI KWA CCM. Tumeona ubunge wa EA watoto wa wakubwa CCM walivyonyukana, ni wao tu Kimbisa na Shyrose ni watumwa wao tu, lazima wawepo kuonogesha mambo.
Cha mwisho unaangalia koo hizo za CDM na KOO ZA CCM zinafanya nini kwa taifa hili? upande mmoja wezi na upande mwingine wapinga wizi, unachagua nini??? kuna mtu anasaini mkataba wa kitaifa kwa niaba ya wananchi harafu anakomaa ni siri kati yake na mwekezaji??? huyo si ni mwizi au unataka umpe jina gani jipya hapa duniani???