Siku ATCL itakapoitwa "Air Tanzania Express"

Siku ATCL itakapoitwa "Air Tanzania Express"

OkSIR

Senior Member
Joined
Jun 3, 2009
Posts
108
Reaction score
1
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kampuni ya ndege ya tanzania (ATCL)liko katika mchaakato wa kubadili jina na kuitwa AIRTANZANIA EXPRESS...akiongea na mtoa chanzo amesema wameambiwa tangu mwezi wa 4 kutafuta pesa kwa ajili ya redanders ya wafanyakazi wote inayokadiriwa kufikia billion 16.....na kuanza kuajiri upya.akiwa katika kuongea kwa machungu alisema laiti wanaotarajiwa kufanya haya mwl nyerere asikie na kuwahoji mmoja baada ya mwingine.......
Habari zaidi zinasema kampuni hiyo mpya inayotarajiwa kuanzishwa na wachina wanaoitwa sonagol ilitarajiwa kuanza kazi rasmi jul 02/2009 lakini kutokana na mchakato wa madeni ya kampuni hii wachina waliona kuibeba ATCL kama yenyewe bora waende sudan kusaka madini...wakiwa katika mikutano yao wachina hao ambao inasemekana walikuja kwa nia ya kusaini mikataba kulingana na makubaliano ya awali na serikali walijikuta wakiambiwa tofauti na hivyo kutoa mwongozo wao wa kuichukua kampuni hiyo ambapo moja ya mada iliyoitetemesha serikali ni swala la madeni ya kampuni.likifwatiwa na swala la nani awe CEO, nani awe CFO..katika mchakato huo viongozi wa sonagol kampuni iliokabidhiwa jukumu la kuinyanyua aitanzania wamesema na kuweka wazi vyeo vya CEO&CFO lazima vikaliwe na watu wao hapo moto mwingine ukaanza....., ilikubaliwa serikali waendelee kubeba madeni ya kampuni huku wachina wakijitayarisha kuanzisha shirika lao jipya litakalojulikana kaama AIRTANZANIA EXPRESS....
kwa mwenye dondooo zaidi atuletee jukwaani tutathmini kweli imefikia hatua ya kuanzishwa shirika jipya ama uzandiki wa viongozi wetu....

ukiwa katika kutoa mawazo yako binafsi kwa ajili ya ufanisi wa kampuni hii angalia mambo yafuatayo

1)))je ni kweli shirika limefikia hali mbaya kubadilishwa jina na kupewa wachina

2))je kuna haja ya kuwa na Top management itakayoongozwa na wachina...\

3)je ni kweli tanzania na serikali ya tanzania imeshindwa kabisa kulinyanyua kampuni hii bila kutegemea wawekezaji...ni kweli hakuna kiongozi ambae anajua airline industry vyema na kuweza kuikoa kampuni hii pasipo kutegemea hawa wachina...

4)tusiache kuangalia haswa nini chanzo kilichoipelekea kampuni hii kufikia hapo ilipo,,...

unakaribishwa
 
1)))je ni kweli shirika limefikia hali mbaya kubadilishwa jina na kupewa wachina

2))je kuna haja ya kuwa na Top management itakayoongozwa na wachina...\

3)je ni kweli tanzania na serikali ya tanzania imeshindwa kabisa kulinyanyua kampuni hii bila kutegemea wawekezaji...ni kweli hakuna kiongozi ambae anajua airline industry vyema na kuweza kuikoa kampuni hii pasipo kutegemea hawa wachina...

4)tusiache kuangalia haswa nini chanzo kilichoipelekea kampuni hii kufikia hapo ilipo,,...

unakaribishwa

Sasa mkuu si ungetoa japo mapendekezo yako kuhusu hiyo top management wapewe kina nani?

Wamekuja Makaburu mmelalamika, Wahindi TRC, mmelalamika, Wakija Waarabu mna lalamika, Wawekezaji gani mnao wataka nyinyi?
 
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kampuni ya ndege ya tanzania (ATCL)liko katika mchaakato wa kubadili jina na kuitwa AIRTANZANIA EXPRESS...akiongea na mtoa chanzo amesema wameambiwa tangu mwezi wa 4 kutafuta pesa kwa ajili ya redanders ya wafanyakazi wote inayokadiriwa kufikia billion 16.....na kuanza kuajiri upya.akiwa katika kuongea kwa machungu alisema laiti wanaotarajiwa kufanya haya mwl nyerere asikie na kuwahoji mmoja baada ya mwingine.......
Habari zaidi zinasema kampuni hiyo mpya inayotarajiwa kuanzishwa na wachina wanaoitwa sonagol ilitarajiwa kuanza kazi rasmi jul 02/2009 lakini kutokana na mchakato wa madeni ya kampuni hii wachina waliona kuibeba ATCL kama yenyewe bora waende sudan kusaka madini...wakiwa katika mikutano yao wachina hao ambao inasemekana walikuja kwa nia ya kusaini mikataba kulingana na makubaliano ya awali na serikali walijikuta wakiambiwa tofauti na hivyo kutoa mwongozo wao wa kuichukua kampuni hiyo ambapo moja ya mada iliyoitetemesha serikali ni swala la madeni ya kampuni.likifwatiwa na swala la nani awe CEO, nani awe CFO..katika mchakato huo viongozi wa sonagol kampuni iliokabidhiwa jukumu la kuinyanyua aitanzania wamesema na kuweka wazi vyeo vya CEO&CFO lazima vikaliwe na watu wao hapo moto mwingine ukaanza....., ilikubaliwa serikali waendelee kubeba madeni ya kampuni huku wachina wakijitayarisha kuanzisha shirika lao jipya litakalojulikana kaama AIRTANZANIA EXPRESS....
kwa mwenye dondooo zaidi atuletee jukwaani tutathmini kweli imefikia hatua ya kuanzishwa shirika jipya ama uzandiki wa viongozi wetu....

ukiwa katika kutoa mawazo yako binafsi kwa ajili ya ufanisi wa kampuni hii angalia mambo yafuatayo

1)))je ni kweli shirika limefikia hali mbaya kubadilishwa jina na kupewa wachina

2))je kuna haja ya kuwa na Top management itakayoongozwa na wachina...\

3)je ni kweli tanzania na serikali ya tanzania imeshindwa kabisa kulinyanyua kampuni hii bila kutegemea wawekezaji...ni kweli hakuna kiongozi ambae anajua airline industry vyema na kuweza kuikoa kampuni hii pasipo kutegemea hawa wachina...

4)tusiache kuangalia haswa nini chanzo kilichoipelekea kampuni hii kufikia hapo ilipo,,...

unakaribishwa

1.Swali la kwanza lipo wazi kabisa. Shirika la ndege lina hali mbaya. Sidhani kama hili swala ni debatable.

2.Kwa nini wasiweke watu wao? Hata wewe ukiwa na biashara si utataka uajiri watu unaodhani wewe wanafaa? Sasa amuweke tu Mtanzania ili iweje? It is a business na hata ingekua mimi ningeweka mtu ninayeona mimi anafaa. Mambo ya kupeana nafasi kwa kuangalia fulani ana toka wapi haiko sehemu zote.

3.Obviously wameshindwa ndiyo maana wana tafuta wawekezaji. Ila hilo la wawekezaji sio neno. Kutafuta mbia anayeweza kukusaidia kufanikiwa zaidi siyo vibaya. Ethiopian, shirika la ndege la Ethiopia serikali ina ubia na wawekezaji tokea Marekani. Angali shirika lao lilivyo na mafanikio kuliko shirika letu. Partnership or investors is not the issue. Tatizo kubwa ni rushwa na kupeana nafasi kwa kujuana.
 
Kwa hiyo madeni tunaachiwa sisi, kampuni wanachukua wao? Hii ndo mikataba yetu TZ daily! Mtu ashakomba 15% hapo anatuachia sisi mzigo!

Kama hivyo bora kampuni iachiwe iingie kwenye bankruptcy ili waweze kupunguza hayo madeni, kama GM walivyofanya.
 
ATCL ilipokuwa inabinafsishwa kwa makaburu haikuwa na hali mbaya kama ilivyo sasa. Lakini hata hivyo isionekane kwamba kubinafsisha ndio njia pekee ya kuyaendesha makampuni/mashirika kwa tija, kwani hata wazalendo wanaweza kufanya makubwa zaidi; mfano CRDB bank. Hapa kwetu kuna nini? Mbona uwekezaji wa kigeni kwenye nchi nyingine umekuwa na faida? Mbona hatujifunzi?
 
ATCL ilipokuwa inabinafsishwa kwa makaburu haikuwa na hali mbaya kama ilivyo sasa. Lakini hata hivyo isionekane kwamba kubinafsisha ndio njia pekee ya kuyaendesha makampuni/mashirika kwa tija, kwani hata wazalendo wanaweza kufanya makubwa zaidi; mfano CRDB bank. Hapa kwetu kuna nini? Mbona uwekezaji wa kigeni kwenye nchi nyingine umekuwa na faida? Mbona hatujifunzi?
Una uhakika na unacho kisema ndugu!?

DANIDA wanafanya nini CRDB? Au nalo ni shirika la wazalendo wa Kitanzania?

Gonga hapa upate kufunua masikio. CRDB
CRDB BANK LIMITED is owned by over 11,000 shareholders under the following major groups (by value of shares):

Private individuals 37.0

Co operatives 14.0

Companies 10.2

DANIDA investment fund 30.0

Parastatals ( NIC & PPF ) 8 .8​
 
Watafute wawekezaji toka kwenye airlines hivi hao wachina wachimba madini kweli nao si watauza share zao kwa kampuni za ndege jamani hapa mbona iko wazi!!haihitaji kuwa PHD kujua....sasa nini jamani??mbona tunatetemeka sana na jina wawekezaji??tuitishe mchakato watakuja tu ila hao wachina fake....
 
Jamani kweli tungependa hili kampuni lichukuliwe na watu lakini tunachoomba kwa serikali wawape watu walio serious..s...........jamani mmeona ile barabara ya sam nujoma;wengi walilamika jamani wachina na barabara wapi na wapi....waliokaa kimya wakaakaa kimya...hivi sasa tuongeapo nimekuta folen kubwa pale barabarani....ujenzi wameanza kuichimba upya sikuishia hapo .nikaamua kusimama na kuuliza nikaambiwa kuna sehemu nyingi tu zina mawimbi......,ati wameamuriwa kuzirekebisha na katibu wa wizarani.....niliskitika sana...kinachosemekana na ambacho hakuna uwazi hawa wah walitaka kupewa vitalu kule mtwara....,wachimbe mafuta ikashindikana..,nikaona vyema tulete hoja kwa watanzania wenyewe...
 
mimi kinachonitatiza ni hawa wachina;...;jamani leo hii nimepita pale barabara ya sam nujoma wameanza kuirekebisha tena upya..wakati wa ujenzi watu wengi waliongea jamani wachina na bara bara wapi na wapi
 
mimi kinachonitatiza ni hawa wachina;...;jamani leo hii nimepita pale barabara ya sam nujoma wameanza kuirekebisha tena upya..wakati wa ujenzi watu wengi waliongea jamani wachina na bara bara wapi na wapi

kama ulikuwepo nami nimepita hapo jioni hii aiibu aiibu anyway sijui...tuwapeni as long nasikia hizo ndege zinazofanya kazi atc ni zao tutafanyaje??
 
Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kampuni ya ndege ya tanzania (ATCL)liko katika mchaakato wa kubadili jina na kuitwa AIRTANZANIA EXPRESS...akiongea na mtoa chanzo amesema wameambiwa tangu mwezi wa 4 kutafuta pesa kwa ajili ya redanders ya wafanyakazi wote inayokadiriwa kufikia billion 16.....na kuanza kuajiri upya.akiwa katika kuongea kwa machungu alisema laiti wanaotarajiwa kufanya haya mwl nyerere asikie na kuwahoji mmoja baada ya mwingine.......
Habari zaidi zinasema kampuni hiyo mpya inayotarajiwa kuanzishwa na wachina wanaoitwa sonagol ilitarajiwa kuanza kazi rasmi jul 02/2009 lakini kutokana na mchakato wa madeni ya kampuni hii wachina waliona kuibeba ATCL kama yenyewe bora waende sudan kusaka madini...wakiwa katika mikutano yao wachina hao ambao inasemekana walikuja kwa nia ya kusaini mikataba kulingana na makubaliano ya awali na serikali walijikuta wakiambiwa tofauti na hivyo kutoa mwongozo wao wa kuichukua kampuni hiyo ambapo moja ya mada iliyoitetemesha serikali ni swala la madeni ya kampuni.likifwatiwa na swala la nani awe CEO, nani awe CFO..katika mchakato huo viongozi wa sonagol kampuni iliokabidhiwa jukumu la kuinyanyua aitanzania wamesema na kuweka wazi vyeo vya CEO&CFO lazima vikaliwe na watu wao hapo moto mwingine ukaanza....., ilikubaliwa serikali waendelee kubeba madeni ya kampuni huku wachina wakijitayarisha kuanzisha shirika lao jipya litakalojulikana kaama AIRTANZANIA EXPRESS....
kwa mwenye dondooo zaidi atuletee jukwaani tutathmini kweli imefikia hatua ya kuanzishwa shirika jipya ama uzandiki wa viongozi wetu....

ukiwa katika kutoa mawazo yako binafsi kwa ajili ya ufanisi wa kampuni hii angalia mambo yafuatayo
1)))je ni kweli shirika limefikia hali mbaya kubadilishwa jina na kupewa wachina

Kimsingi kwa hali iliyonayo ATCL ilipaswa iwe kwa mfilisi kwani kisheria imefilisika. Njia itakayoweza kuisaidia kuonekana kwa Air Tanzania hewani kuundwa kwa kampuni nyingine kabisa ambayo haitakuwa na uhusiano wowote na ATCL.

2))je kuna haja ya kuwa na Top management itakayoongozwa na wachina...\

Juu ya kuwa na top menejimenti itakayoongozwa na wachina hili haliwezi kuepukika, kwani kama Wachina wananunua hisa Air Tanzania basi ni lazima wawepo kuendesha mali yao. Composition ya kwenye timu ya menejimenti na ile bodi ya wakurugenzi itatokana na makubaliano ya mkataba baina ya pande mbili yaani wachina na watanzania.
Lakini hata hivyo labda bado ndugu yangu una ile kumbukumbu mbaya kabisa ya ubia kati ya SAA na Serikali ya Tanzania ambapo katika mkataba ule serikali yetu ikiwa na hisa 51% iliridhia matakwa mbalimbali ya SAA ikiwemo kuunda management team ya wa-south africa pekee, kuondolewa uhuru wa kuteua Mwenyekiti wa Bodi (refer uteuzi wa Mwenyekiti wa kwanza wa bodi Mh Shelukindo uliodumu kwa masaa machache kabla ya kuamriwa kuondolewa na SAA) , kuhamisha shughuli nyeti za utendaji wa ATCL kupeleka South Africa (kama vile Maintenance, Mafunzo, Finance, Ticketing, Fuel etc) ili iwe rahisi ku-cripple.
Ni vema serikali this time iwe makini kuepusha makosa yaliyojitokeza hapo awali.

3)je ni kweli tanzania na serikali ya tanzania imeshindwa kabisa kulinyanyua kampuni hii bila kutegemea wawekezaji...ni kweli hakuna kiongozi ambae anajua airline industry vyema na kuweza kuikoa kampuni hii pasipo kutegemea hawa wachina...

Pamoja na kuwa na wataalum wenye uwezo wa kuiongoza ATCL wapo, lakini kama serikali haina fedha za kuwekeza katika hiyo Airline ni kazi bure. ATCL inahitaji injection ya mtaji wa kutosha utakaoiwezesha kugeuka na kuwa profitable airline, na hili ndiyo lengo kuu na siyo suala la kusema ATCL inahitaji madege makubwa au kwenda safari za mabara, la hasha inabidi ATCL iwe na mkakati wa kuwa airline inayopata faida. Baada ya hapo au ndani ya hapo kama kuna haja ya kuwa na madege makubwa au kufanya safari za mabara then uamuzi unakuwa ni sahihi.

4)tusiache kuangalia haswa nini chanzo kilichoipelekea kampuni hii kufikia hapo ilipo,,...

ATCL imefikia hapo ilipofikia kutokana na sababu mbalimbali,
Sababu ya kwanza ni ya kihistoria wakati wa enzi za Air Tanzania Corporation. Kipindi kile ATC iliendeshwa bila ya kujali faida na badala yake ilikuwa inajali kutoa huduma katika mpangilio wa kisiasa zaidi. Na hii ilitokana na kuwa ATC ilikuwa inamilikiwa 100% na serikali kwa hiyo serikali ndiyo iliyokuwa na kauli ya mwisho juu ya ATC. Hali hii iliifanya ATC kutegemea ruzuku za serikali na hata kuharibu kabisa capital structure yake kuwa si ya kuvutia.
Sababu nyingine ni kuwa ATCL haikukuwa kutokana na wakati matokeo yake ilifika kipindi ambacho ilidumaa yaani ilifikia ukomo wa kukua. Ujenzi wa maitenance hangar pale KIA ilikuwa ndiyo njia mojawapo za kuifanaya ATC kukua kwa maana ilikuwa na nafasi ya kupanua shughuli za Aircraft maintenance kwa kiwango kikubwa. Facilities kama hizo sasa hivi zimekuwa kwa kiwango kikubwa kule Madagascar, Ethiopia, Kenya na South Africa.
Sababu ya tatu, ni kwamba kwa vile ATC haikuwa na mvuto wakati wa ubinafsishaji wake, ilipeka kutokupata wabia ambao walikuwa serious na business, matokeo yake akapatikana SAA ambaye alikuwa na mission tofauti na malengo yetu ya ubinafsishaji. Kwahiyo kitendo cha SAA kuweko ndani ya ATCL kilitosha kabisa kuifikisha hapo ilipo leo. Japo 'laiti' haitangulii basi nadiriki kusema kwamba ATC ilikuwa bora sana hadi ilipofika 02 Disemba 2002 baada ya hapo kazi ilikuwa ni moja tu kuhakikisha ATCL inaondoka katika ramani ya dunia na hili jambo limefanikiwa na ATCL imepewa ugonjwa ambao haiwezi kukwepa kifo chake.


unakaribishwa


Mwisho labda nitoe ushauri kwa kadri hali ilivyo.
Ujio wa mchina unaweza kuwa ni faraja tu kwa wakati huu japokuwa si mwarobaini wa matatizo yetu, kwani at anytime akiona kuwa hapati anachokitaka anaweza ku-pull out na tusimfanye chochote.
Ninashauri kuwa wafanyakazi waliokuwepo wote wastaafishwe au ajira zao zikome kwa ATCL na walipwe haki zao zote wanazostahili.
Pili, kampuni mpya iajiri wafanyakazi katika makubaliano mapya na iwachukuwe wale ambao itakuwa inawahitaji tu.
Tatu, serikali ni lazima iwe na nafasi katika top management kwa maana kuwa members wengine wawe ni watanzania. Kwa mfano kama CEO na CFO watatoka China then position zingine ziwe ni za watanzania.
Nne, kama serikali itakuwa ndiyo majority shareholder, basi suala la kuchagua Mwenyekiti wa Bodi liwe mikononi mwake na wala si mikononi mwa minority kama ilivyokuwa hapo siku za nyuma kwa SAA.
Tano, kampuni inatakiwa kuwa mikakati ya kweli ya kuifanya iwe profitable na si vinginevyo kwa maana hiyo serikali ni lazima ichangie in full katika fungu la uendeshaji na si kwa mafungu-mafungu. Pia ihakikishe inaweka bodi yenye uwezo wa kusimamia kampuni hiyo.
Sita, tubadilshe mind set zetu, tufanye kazi kwa bidii na ikibidi tutumie kale kamsemo ka 'asiyefanya kazi na asile'
 
Last edited:
last night nimeona kitu CBS (letterman show) sikuamini lakini baada ya muda one of my friends akaniambia same thing ndio nikaamini nilichoona ni kweli....AIRTANZANIA walikuwa wanatangaza shirika lao kwenye kipindi cha letterman,hivi wana ndege hata moja inayo operate states? au target yao ni nini? au ndio ulaji wa wajanja tu...naomba maelezo!
 
Sasa mkuu si ungetoa japo mapendekezo yako kuhusu hiyo top management wapewe kina nani?

Wamekuja Makaburu mmelalamika, Wahindi TRC, mmelalamika, Wakija Waarabu mna lalamika, Wawekezaji gani mnao wataka nyinyi?
Ungeongezea kwamba "wabongo" wameshindwa walipewa for 50 years wanaiba na kujaza matumbo yao.
 
Ukweli ni kwamba kampuni ilitakiwa iachwe ife! Kama kuna haja ya kuwa na National carrier basi wangeanza mwanzo kabisa.
 
Ukweli ni kwamba kampuni ilitakiwa iachwe ife! Kama kuna haja ya kuwa na National carrier basi wangeanza mwanzo kabisa.

Mie kuna kitu sielewi... Kila move inayopendekezwa, tunaizika mapema sana kabla ya kupima!!! Sasa tufanyeje na ATC? au tuliache ndege zichoke mpaka zianguke ziue ziishe halafu ibaki historia kama dinosaurs??

Wasauzi, wamasai, wachagga, wanyasa wote tuliwawasha na sasa wachina!! kwangu tatizo si nani anawekeza, tatizo ni uwezo wa baadhi ya watendaji kusimami utekelezaji

Wale wenzetu weledi--- hedu saidia masikini kimawazo naye arushe ndege!!!
 
Back
Top Bottom