Siku ambayo sitaisahau

Siku ambayo sitaisahau

Pole..Mshikaji sio muaminifu cha msingi tuliza kichwa usije ukafanya maamuzi mabaya.
 
Ilikuwa ni siku ya alhamisi, mpenzi wangu alinipia simu kwamba anaitaji tuonane. Kwa kweli alinishtua sana, nilijua labda amepatwa na tatizo. Nilipofika kwake aliniambia kwamba anaitaji kutoka na mimi kwenye sikukuu ya pasaka. Kwa7bu ya upendo wangu kwake nilimkubalia ombi lake. Ilipofika siku ya jumapili asubuhi alinipigia simu kwamba anajisikia vibaya (anaumwa), kwahiyo hawezi kwenda sehemu yoyote siku hiyo. Kwa kweli nilimuhurumia sana, nakumuahidi nitaenda kumuona siku hiyo. Japo kuwa alinikatalia kwenda kumuona, sikukata tamaa jioni nilienda kumuona, cha kushangaza sikumkuta na mlango ulikuwa umefungwa. Nikaanza kuwauliza majirani zake, walinijibu kwamba aliwahaga anakuja kwangu, nalipojaribu kupigia simu hakupatikana. Nikaamua kurudi nyumbani, wakat nipo njiani nikapigiwa simu na rafiki yangu kwamba amemuona mpenzi wangu akiwa na msichana mwingine wakiwa kwenye Bar fulani. Nakachukua bodaboda hadi eneo husika na nilichokishuhudia ni Mungu mwenyewe anajua. Jamani nimevurugwa sana. Nilikuwa naitaji marafiki wa kunifariji. Sichagui Dini, kabila wala jinsia. Wote kwangu ni marafiki tu.
ulimkuta anafanya nn?na nani?mbona kama hujamalizia vile?
 
Sikia rafiki humu ndan hakuna awezae kuku fariji inavyo stahili maana faraja za wanadamu zote hazitoshelezi mwishowe kuumia tena,majuto,lawama,nk.mwite YESU awe mfarij wako had mwisho wa dahari.
 
usisahau jina la hiyo bar!, ni muhimu sana ktk kumbukumbu zako/historically
 
Uliyemuona yuko na mtu wako unamjua?
kama hujamalizia kitu
yukoje?

kakuzidi nini zaidi?
 
Ulichokishuhudia ni Mungu pamoja na wewe mnajua ndo maana umeumia sana ila pole. Story yako ulivoandika mwanzoni nikajua kidume mwenzangu katendwa kumbee ni maua yetu polee jamanii
 
Pole mumy,hebu nitafute PM nikupe ushauri upoze huo moyo uliovunjika.
Maana kivyovyote maisha lazima yaendee.
ACHA UJINGA!

UMPE USHARI WA NINI!!

WEWE WATAKA KUTUHARIBIA WANA OPOCHUNITI YA KUPIGA TONGOZO TU HAPA!
 
Back
Top Bottom