Siku 100 za Edward Lowassa Madarakani

Siku 100 za Edward Lowassa Madarakani

Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali

1. Hakuwa RAIS
2. Alikuwa CCM
3.Alizungukwa na mfumo mchafu ufanyao kazi kwa mazoea na sio kwa ufanisi

Machache aliyoyafanya ni NOTABLE, japo hayakufikia kiwango ambacho kilitakiwa kwa sababu Misisiemu walienda haendani na mfumo wao wa kuiba kupitia miradi ya wananchi.
 
Mhhhh!! Hayo yote ndani ya siku 100. Nadhani hata baraza la mawaziri litakuwa bado halijaanza kazi.

Mengi ni porojo,kumbuka bajetı ya serikali itakuwa bado haijapitishwa.Kushusha PAYE,kuongeza mishahara itakuwa ni ngumu.Kuondoa michago na ada mashuleni na vyuo vikuu, hzo anatoa tu statement za kisiasa(kuanzia tar 1 januari,2017 hakutakuwa na ada).Tume na upatikanaji wa dawa mahospitalıni inawezekana hata ndani ya wiki moja.OTHERWISE, ni mbwembwe tu za kısıasa!
 
5. Kuhusu kuondoa kero kwa mama ntilie, bodaboda na machinga, hilo lipo kwenye utekelezaji wa mamlaka za serikali za mitaa. Halihitaji usimamizi wa Rais. Atakuwa Rais wa ajabu sana kama atakaa barabarani kuhakikisha hakuna kamata kamata ya bodaboda. Ni ulaghai wa kisiasa huu
 
Ile ilani aliyotuambia tukaisome kwenye website ameachana nayo, siyo? Kila siku anabadilisha vipaumbele!

Hakuna jambo baya kama mtu kutumia hali ya maisha ya watu wengine ili atimize malengo yake ya kisiasa! Lowassa amekaa CCM miaka 40, na sehemu zote alizopita ameacha makovu. Hapo kwenye maji. Mbona alivyokuwa waziri mkuu hakusema chochote kuhusu machina na mama ntilie?
 
Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali

Acha tuinywe hata kama ni sumu.wewe inakuuma nini kama tutakufa.
 
6. Kuhusu tatizo la maji nchini, Lowasa alikuwa Waziri wa Maji na wakati huo hakuweka mipango yoyote ya kuondoa tatizo hilo. Hata jimbo la Monduli analoliongoza, wananchi wanakunywa mikojo ya Ng'ombe kwa kukosa maji safi na salama licha ya yeye kujinasibu kuwa anauchukia umaskini. Kwa sasa serikali inatekeleza mpango kabambe wa kuondoa tatizo hilo kwa vijiji vyote ambapo kila mwaka halmashauri hupewa fedha za miradi ya maji kwa vijiji zaidi ya 10
 
4. Kuhusu kupunguza foleni ya Dar es Salaam, hilo tayari lipo kwenye utekelezaji. Miundombinu ya DART inaendelea kukamilishwa na zaidi ya mabasi 140 yameshaingia nchini. Mabasi hayo ni ya kisasa na makubwa ambayo yatapita kwenye njia rasmi na hivyo kuharakisha movement ya magari. Kweli Lowasa ni tapeli
Nani kakwambia DART itapunguza foleni DSM akili zako za kushikiwa ww.DART ni mradi wakufanya mabeberu wachache washikirie ishu ya usafiri DSM wapige pesa wao waweke daladala za maskini pembeni wakauze kahawa magomeni
 
Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali
Wakati akiwa madarakani Kikwete alikuwa Msoga analima mihogo, siyo??
 
6. Kuhusu tatizo la maji nchini, Lowasa alikuwa Waziri wa Maji na wakati huo hakuweka mipango yoyote ya kuondoa tatizo hilo. Hata jimbo la Monduli analoliongoza, wananchi wanakunywa mikojo ya Ng'ombe kwa kukosa maji safi na salama licha ya yeye kujinasibu kuwa anauchukia umaskini. Kwa sasa serikali inatekeleza mpango kabambe wa kuondoa tatizo hilo kwa vijiji vyote ambapo kila mwaka halmashauri hupewa fedha za miradi ya maji kwa vijiji zaidi ya 10

Kumbe wewe kichaa
 
7. Kuhusu mfumo rafiki na bora kwa wafanyabiashara, hilo linajulikana kuwa utawala wa Lowasa ni wa kukumbatia wakwepa kodi kwa vile hao ndio wanaompeleka Ikulu. CCM imeshamaliza kutengeleza mfumo na kwa sasa kinachoendelea ni kutoa elimu kwa wafanyabiashara ili walipe kodi bila ya shuruti
 
Sasa kama alikaa madarakani kwa muda wa siku 800 akiwa Waziri Mkuu na hakufanya hayo atawezaje ndani ya siku 100? Tumia akili. Lowasa ni sumu iliyojificha ndani ya asali

Hata useme ni sumu iliyo kwenye maziwa kura zetu anazo.
 
na hiyo ndani ya siku 100 asisahau kutuwekea na treni za umeme(sub way) ili na sisi tuwaringishie Kenya.
maana uwezo anao
Umeujuaje uwezo wake? Mnasaidiana na mama Regina??
 
8. Kuhusu kufuta ada na michango kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, hilo ni jambo ambalo Liwasa hawezi kulifanya kwa siku 100. Kwanza akumbuke kuwa kuna shule za binafsi na za umma. Pia kuna vyuo vya binafsi na vya umma. Kusema kuwa atafuta michango na ada kwa shule zote ni kujidanganya. Pia kabla ya kufuta, kuna mambo ya kisera ambayo yanapaswa kujadiliwa. CCM wameshaanza chekechea hadi chuo Kikuu kwa shule za Umma.
 
7. Kuhusu mfumo rafiki na bora kwa wafanyabiashara, hilo linajulikana kuwa utawala wa Lowasa ni wa kukumbatia wakwepa kodi kwa vile hao ndio wanaompeleka Ikulu. CCM imeshamaliza kutengeleza mfumo na kwa sasa kinachoendelea ni kutoa elimu kwa wafanyabiashara ili walipe kodi bila ya shuruti

Naona sasa ni wazi unachanganyikiwa
 
# 7 Inanifanye nimpe kura yangu LOWASA

maana east africa wamefanya Tanzania soko lao sisi hatuuzi vitu kwao wakati tuna bandari
_sox ni rahisi kampala wakati wanazotolea bandari ya dar
 
9. Kuhusu kupunguza PAYE, hapa ndipo ninapomuona Liwasa ni laghai. Serikali imekuwa ikipunguza kodi hiyo kila mwaka. Ilikuwa asilimia 18 ambapo kwa sasa PAYE ni asilimia 11. Lengo ni kufikia digit moja by the end of 2016
 
Back
Top Bottom