Ocampo four
JF Senior Expert Member
- Feb 28, 2014
- 5,789
- 2,159
- Thread starter
- #41
6. Kuhusu tatizo la maji nchini, Lowasa alikuwa Waziri wa Maji na wakati huo hakuweka mipango yoyote ya kuondoa tatizo hilo. Hata jimbo la Monduli analoliongoza, wananchi wanakunywa mikojo ya Ng'ombe kwa kukosa maji safi na salama licha ya yeye kujinasibu kuwa anauchukia umaskini. Kwa sasa serikali inatekeleza mpango kabambe wa kuondoa tatizo hilo kwa vijiji vyote ambapo kila mwaka halmashauri hupewa fedha za miradi ya maji kwa vijiji zaidi ya 10
Alitoa maji kutoka Mwanza kwenda Shinyanga. Na plan yake ilikuwa ni kuyapeleka Dodoma via Singida... In that case mikoa zaidi ya 7 ungefaidika na huo mradi