Sijui ni Malaria?

Sijui ni Malaria?

Mzee wa Shida

Member
Joined
Nov 29, 2014
Posts
66
Reaction score
5
Sijui ni Malaria? Yani naumwa kweli, hata kula nashindwa; asubuhi yenyewe nimekula chapati 9 tu, maandazi 7, mihogo 7, vitumbua 10, mikate 6, magimbi 5, ndizi za kukaanga 4, sambusa 5, sahani za ubwabwa 3, mtori bakuli 2, pilau sahani 5, kulikuwa na kiporo cha makande nimejazia jazia ivyo ivyo kigonjwagonjwa.

Sahivi natoka kwa Doctor kuchukua dawa ya kuleta hamu ya kula, kwa kweli hali yangu ni mbaya.

By Mwanao mkristo rose
 
Aseee....homa yako unatakiwa kupimwa kwa kuwekewa mkono shavuni....Hamna jinsi sasa!
 
Hahahaaaaaa, hiyo malaria sasa ni mbaya maana inakufanya ule chakula cha watu ishirini na bado hakikutoshi. Jiandie kuzikwa kipindi cha njaa maana utakufa kutokana na ukosefu wa chakula.
Hata manenge na Mandawa hawakuwa hivyo. Pole sana.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom