Sijui mama Janeth Magufuli ataanzisha taasisi gani?

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
Baada ya kupita kwa awamu mbili za kwanza za Baba wa taifa marehemu Mwl Julius K. Nyerere na ile ya mzee Ally Hassani Mwinyi, marais waliofuata yaani wa awamu ya tatu Bwana Benjamini Mkapa na huyu aliyeondoka wa awamu ya nne Prof. Jakaya Kikwete walianzisha utaratibu mpya wa wake zao kuanzisha taasisi binafsi au NGO wakiwa ikulu.

Mke wa rais wa awamu ya tatu mama Anna Mkapa alianzisha taasisi au NGO yake aliyoiita EOTF na baaada ya kuondoka ikulu akaondoka nayo. Rais wa awamu ya nne mkewe mama Salma Kikwete alianzisha WAMA ambayo nayo atakwenda nayo. Sasa kama utaratibu huo utaendelea sijui mama Janeth Magufuli atakuja na NGO gani?

Labda tutegemee VIMA yaani Vijana na Maendeleo, au BAMA yaani Baba na Maendeleo au OA yaani Okoa Albino na pengine labda SAWA yaani Saidia Wazee.

Karibu sana ikulu mama Janeth Magufuli msaidie mzee kutimiza ahadi zake nyingi alizo ahidi. Mkumbushe asisahau kuanzisha mapema mahakama ya Mafisadi kama alivyosema akiingia tu hiyo itakuwa ni ajenda namba moja.

Nyingine ni kufuta ushuru wa biashara ndogo ndogo na mazao, kupunguza kodi za PAYE ba leseni za biashara, kufuta karo na michango yote shuleni ikiwa ni pamoja na ya mlinzi, mitihani, na madawati, kuunda baraza dogo la mawaziri linalowajibika na kujenga utaifa. Kila la kheri wanaikulu wapya!
 
Sio lazima aanzishe taasisi kama wengine.
Anaweza akawa balozi wa taasisi zilizopo.
Au hata akaendeleza WAMA.
 
1. Aongee na TASAF, ESRF, REPOA, TLS na wadau wengine. . . .,atapata issues zinazohitaji kushughulikiwa yeye akaunda "an umbrella" tu ya kuhakikisha wadau hao wanafanya yale yenye changamoto watakayokubaliana. . . . .Sio lazima aunde taasisi ambayo kimsingi itashughulikia mambo ambayo tayari kuna agents wako field na experience kubwaa. . . .just a sort of partnership na waliopo inaweza leta matunda
2. Akiwa kama mwalimu anaweza ongeza na yale aliyoyaishi na kuyajua kwa muda mrefu. . . . . .madawati, vyoo bora na maji akishirikiana na TAMISEMI

Mambo ya kufanya yapo mengi sana akiamua kusaidia jamii
 
mama amsaidie mzee kivp tunataka mawazo ya yeye kama yeye maswala ya kushauriwa wrongly ndo hvhv unakuta tunaingia kwenye shida zisizo za msingi JPM do your thing baba
 
Unaonekana usoni u mtaratibu mshauri John apunguze jaziba Urais unahitaji hekima na busara aache dharau na mjivuno , kila la kheri shem.
 
Ni kweli serikali ya awamu ya 5 ina mabadiliko makubwa ukilinganisha na zile zilizopita. Katika awamu zilizopita wake za maraisi wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania walikuwa na michango mingi kijamii. Kwa mfano walifungua mifuko ya kijamii hasa ya wanawake, walikuwa na campain tofauti hasa za mama na watoto, pia walianzidha miradi mbalimbali. Na hii haikuwa tanzania peke yake. Hata nchi za wenzetu. Wake za maraisi huwa wana mchango flani katika jamii. Huwezi kuitwa First lady huna mchango wowote katika nchi yako.

Swali langu ni kwanini First lady wetu wa sasa hajihusishi na mambo ya kijamii?
 
Muacheni afanye mambo yake, nimempenda sana huyu mama..hana kimbelembele..
Wanawake wengine waume zao wakiwa na cheo fulani basi nao wanajiona kama "wanashea" mamlaka!
Kwenye budget huwa kuna pesa inatengwa kwa ajiri ya ma First lady kutoa michango ya kijamii. Pia kuna mifuko ya wakinamama ambayo husimamiwa na mafirsty ladies.
 
Back
Top Bottom