mafoleni
JF-Expert Member
- Nov 18, 2016
- 220
- 371
TFF yawaondoa wachezaji wa Simba ndani ya ‘Taifa Stars’, viongozi wao kupelekwa kwa pilato
702
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limewaengua katika kikosi cha timu ya taifa ‘Taifa Stars’ wachezaji sita wa timu ya Simba kutokana na kuchelewa kuripoti kambini kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na kocha, Emmanuel Amunike.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao
Nyota hao walitakiwa kuripoti kambini jana usiku huku wakiwa wamepewa taarifa wakati Aishi Manula pekee ndiye aliyeripoti.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao amewaambia waandishi wa habari kuwa kocha Amunike amekasirishwa na kitendo hicho na kuamua kuchukua maamuzi hayo amabayo Shirikisho hilo chini ya Rais Wallace Karia wamelipitisha.
“Wachezaji wote wa Simba walioitwa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ isipokuwa Aishi Manula wameenguliwa katika kikosi kinachojiandaa na mchezo wa kufuzu dhidi ya Uganda kutokana na kutoripoti kambini kwa muda uliopangwa,” Wilfred Kidao Katibu Mkuu TFF.
Kidao ameongeza kuwa TFF iliamua kusogeza mbele mechi za Simba, Azam na Yanga zilipokuwa zichezwe Septemba mosi na pili ili kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Afrika dhidi ya Uganda ‘The Cranes’ utakaofanyika Septemba 8 jijini Kampala. “TFF imewaengua wachezaji sita wa Simba kwenye kikosi cha timu ya taifa kutokana na kuchelewa kuripoti kambini licha ya kupewa taarifa mapema,” alisema Kidao.
Wachezaji hao ni Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Hassan Dilunga, John Bocco na Shiza Kichuya.
Mbali na wachezaji hao viongozi wa Simba, Hamisi Kisiwa na meneja Richard Robert watapelekwa katika kamati ya maadili ya TFF siku ya Jumamosi ili kuchukuliwa hatua.
Sent using Jamii Forums mobile app
702
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limewaengua katika kikosi cha timu ya taifa ‘Taifa Stars’ wachezaji sita wa timu ya Simba kutokana na kuchelewa kuripoti kambini kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na kocha, Emmanuel Amunike.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao
Nyota hao walitakiwa kuripoti kambini jana usiku huku wakiwa wamepewa taarifa wakati Aishi Manula pekee ndiye aliyeripoti.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao amewaambia waandishi wa habari kuwa kocha Amunike amekasirishwa na kitendo hicho na kuamua kuchukua maamuzi hayo amabayo Shirikisho hilo chini ya Rais Wallace Karia wamelipitisha.
“Wachezaji wote wa Simba walioitwa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ isipokuwa Aishi Manula wameenguliwa katika kikosi kinachojiandaa na mchezo wa kufuzu dhidi ya Uganda kutokana na kutoripoti kambini kwa muda uliopangwa,” Wilfred Kidao Katibu Mkuu TFF.
Kidao ameongeza kuwa TFF iliamua kusogeza mbele mechi za Simba, Azam na Yanga zilipokuwa zichezwe Septemba mosi na pili ili kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Afrika dhidi ya Uganda ‘The Cranes’ utakaofanyika Septemba 8 jijini Kampala. “TFF imewaengua wachezaji sita wa Simba kwenye kikosi cha timu ya taifa kutokana na kuchelewa kuripoti kambini licha ya kupewa taarifa mapema,” alisema Kidao.
Wachezaji hao ni Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Hassan Dilunga, John Bocco na Shiza Kichuya.
Mbali na wachezaji hao viongozi wa Simba, Hamisi Kisiwa na meneja Richard Robert watapelekwa katika kamati ya maadili ya TFF siku ya Jumamosi ili kuchukuliwa hatua.
Sent using Jamii Forums mobile app