Sijawahi kupanda ndege

Sijawahi kupanda ndege

Na pia kuna makelele sjui niite sauti flani kama mruzi, huwa inasikika ndege inapokaribia kutua aisee mwanzo ilinisumbua sana. Hii huwa sauti ya nini maana mpaka masikio huwa yanaziba.

Mimi hii imenishinda kuizoea, hasa napotua DSM Airport kwa safari za humu ndani.

Yaani masikio yanaziba, kichwa kinagonga balaa.
 
nilitaka kumwambia kuwa Huduma za vyakula na vyakunywa ni buree ila nikaona aibu.

maana nasikia ndege za kwenda nje wanatoa vyakula bure sasa iweje fastjet waniuzie Maji? ndo maana walinizuia nisiingie na Maji yangu hili ninunue yao .siku hizi nishawajulia sinunue chochote

PrecisionAir wanagawa bure, ila wakipita umesinzia ndo imetoka.

Kuna siku nilikuja kushtuka wameshapita ilibidi niwafate, wakasema kwangu walishapita, niliwamind mpaka wakanipa.
 
Wakuu habari za leo.
Kichwa kinajieleza, sasa nataka kuvunja rekodi hii, naomba kufahamu A to Z, nikitaka kwenda Mwanza toka Dar, naanzaje?
Njia nzuri ya kujifunza kwa vitendo ni kufanya makosa kwa vitendo na sio ushauri huu nadharia. Mkuu nakushauri fanya hivi, baada ya kukata ticket wewe nenda kapande ndege kama ulivyozoea kupanda mabasi ya mikoani. Hapo ndipo utakapojifunza murua kabisa tena waambie wakupe na instruction note baada ya kujifunza kutokana na makosa natumai utaushughulikia ushauri wangu 100%
 
Wakuu habari za leo.
Kichwa kinajieleza, sasa nataka kuvunja rekodi hii, naomba kufahamu A to Z, nikitaka kwenda Mwanza toka Dar, naanzaje?
Mbona kuna ambao hawajawahi hata kupanda basi la mkoani wao ni ndege tu mwanzo mwisho na wanatamani sana siku moja wabahatike kupanda basi la mkoani kama vile wewe unavyotamani upande ndege.
 
Mimi hii imenishinda kuizoea, hasa napotua DSM Airport kwa safari za humu ndani.

Yaani masikio yanaziba, kichwa kinagonga balaa.
Nilishawahi kwenda mafia mara mbili na hivi vindege vidogo nilifika masikio yameziba sisikii kitu, bahati mbaya hii safari ya mwisho nilitakiwa nitoe mada kwenye taasisi flani, kufika natakiwa niende moja kwa moja ukumbini nikatoe mada maana watoa mada wengine walikuwa tayari nilikuwa nasubiriwa mm tu, aisee ilibidi niingie chooni kwanza nikawa nalazimisha miayo nakupanua mdomo nilirudia zoezi hilo kwa mida km dakika 10 hali ikawa afadhali.
 
nilitaka kumwambia kuwa Huduma za vyakula na vyakunywa ni buree ila nikaona aibu.

maana nasikia ndege za kwenda nje wanatoa vyakula bure sasa iweje fastjet waniuzie Maji? ndo maana walinizuia nisiingie na Maji yangu hili ninunue yao .siku hizi nishawajulia sinunue chochote
Na wewe safari ya nusu saa au one hour unataka ule,unywe kisa umepanda ndege?

Budget airline nyingi wanauza refreshments.
 
Back
Top Bottom