Sijawahi kupanda ndege

Kwenye physics tulifundishwa dirisha la ndege halifunguliwi mkuu.
Mkuu halifunguliwi kwa minajili ya kama vile unavyofungua au kushusha kioo cha gari, linafunguliwa kwa maana ya kwamba madirisha ya abiria hasa kwenye ndege kubwa yana cover flani linalozuia kuona nje; Kama mtu huitaji kutazama nje au chini ardhini unaweza kushusha cover la dirisha, ila kama unapenda kutizama nje ardhini na kupiga picha wakati ndege ipo juu unaweza kupandisha hilo cover na kuweza kuona nje kupitia kwenye kioo. Katu madirisha au vioo vya ndege hayafunguki na haviwezi funguliwa ndege ikiwa angani. Vioo vinavyoweza kufunguka ni vya mbele kwa marubani tu na vinaweza funguliwa ndege inapokuwa imetua chini pekee.
 
Back
Top Bottom