Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 34,675
- 40,926
Nadhani wote sio wageni wa kilichomkuta waziri wa utalii Nd. Kigwangala, namtakia afya njema apone haraka.
Wakati tukiendelea kumuombea ndugu yetu apone haraka, sio vibaya tukaulizana, kama ndugu zetu wa vyama shindani, nikimaanisha Chadema, NCCR, CUF na wengineo wamekwenda hospitali kumjulia hali na kumpa pole waziri.
Kwa bahati nzuri sana, Chadema wanaye Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Huyu ni Mtu mkubwa sana katika mhimili wa Bunge. Hivyo kwa nafasi yake tulitarajia kumuona akiwa mstari wa mbele katika hili.
Labda nimepitwa , ila mpaka sasa, sijaona katika habari wala mitandao ya kijamii, viongozi wa juu toka upinzani, wakienda kumuona waziri hospitali na kumpa pole.
Kama inatokana na kutingwa na majukumu ya kijamii, sawa ila kama hawajatingwa ila ni maamuzi tu, basi napata mashaka sana na weledi wao katika kufanya maamuzi ya kitaifa. Hii ilikuwa nafasi nzuri sana ya wao kuonyesha kuwa ni wanasiasa wa aina gani, ila naona kama vile wameipoteza bila kujali jamii itawaonaje, jamii ambayo ndio wapiga kura wao.
Mpaka sasa jamii inawatazama kwa jicho la mshangao. Muda bado upo.
Wakati tukiendelea kumuombea ndugu yetu apone haraka, sio vibaya tukaulizana, kama ndugu zetu wa vyama shindani, nikimaanisha Chadema, NCCR, CUF na wengineo wamekwenda hospitali kumjulia hali na kumpa pole waziri.
Kwa bahati nzuri sana, Chadema wanaye Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Huyu ni Mtu mkubwa sana katika mhimili wa Bunge. Hivyo kwa nafasi yake tulitarajia kumuona akiwa mstari wa mbele katika hili.
Labda nimepitwa , ila mpaka sasa, sijaona katika habari wala mitandao ya kijamii, viongozi wa juu toka upinzani, wakienda kumuona waziri hospitali na kumpa pole.
Kama inatokana na kutingwa na majukumu ya kijamii, sawa ila kama hawajatingwa ila ni maamuzi tu, basi napata mashaka sana na weledi wao katika kufanya maamuzi ya kitaifa. Hii ilikuwa nafasi nzuri sana ya wao kuonyesha kuwa ni wanasiasa wa aina gani, ila naona kama vile wameipoteza bila kujali jamii itawaonaje, jamii ambayo ndio wapiga kura wao.
Mpaka sasa jamii inawatazama kwa jicho la mshangao. Muda bado upo.