Sijajiuzulu uongozi CHADEMA-Prof.Baregu

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA Prof. Mwesiga Baregu amekanusha vikali taarifa za kujiuzulu nafasi za uongozi ndani ya CHADEMA zilizozagaa kwenye mitandao, asema hana mpango wa kufanya hivyo.

Professa Baregu amesema uvumi huo unaenezwa na CCM na vibaraka wake na kuendelea kusisitiza kwamba Chadema itaendelea kuwa moja na Imara zaidi.

Source:Mwananchi Breaking News
 

Mwananchi breaking news??? kama ni kweli kibaraka wa CCM anayemsema ni nani kama siyo yeye aliyeteuliwa na MWENYEKITI WA CCM kuingia tume ya Katiba?
 
Yatasemwa mengi ila ndiyo wanawakomaza na kuwaandaa kisaikolojia kuchukua nchi.
 
Jambo la kushangaza.....zamani vyama vya upinzani vilidoea wanaojitoa CCM lakini naona formula imebadilika....

Nilichosoma toka kwa wanaCCM toka jana ni kwamba wao ndo wanatamani wapinzani hawa wajiunge kwao......

Je kuna watu wanajiandaa kuwa wapinzani baada ya 2015?
 
CCM wanahaha lakini wapi,CDM ndo kila kitu mazee wao magamba yameishia viunoni lakini huku kwetu unafanya upuuzi tunainama kwenye katiba tunaona inasemaje tunachukua hatua ...CDM haina mtu fulani bali ina viongozi na wanachama na wote ni sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…