Sifa kumi za mpenzi wa kweli

Bora mara elfu ukutane n utapeli wa mjini kuliko wa kijijini. Manake wanaparamia hao! Wa mjini anakuchuna kwa akili wala hauchakai. Kama hauamini agiza parcel ya mke umlete town, wauza maji na mboga watakuonea hadi ukome.
Mimi nipo mjini!
 
Mpenzi msomaji wangu, ni wakati mwingine ambao tunakutana katika uwanja huu wa maisha na mapenzi, kwa lengo la kujifunza namna ya kuwa wapenzi bora na kuepukana na tatizo la kuachana ambako kumekuwa fasheni siku hizi.

Vijana wengi ambao wanapendana leo mapenzi yao hayadumu kiasi cha kubatishwa jina la utamu wa bazoka. Lakini yote hii inatokana na ukweli kwamba elimu ya mapenzi ambayo ni muhimu kwa binadamu haitolewi ipasavyo.

Ipo zana potofu kwamba kumfundisha motto mapenzi ni kumharibu, jambo ambalo si kweli bali inategemea mtoto huyo anafundishwa nini na kwa wakati gani. Lakini cha kushangaza zaidi hata watu wazima ambao ni wadau wa mapenzi hawayajui, matokeo yake wanajiingiza kwenye uhusiano wakiwa bumbumbu na hivyo kuteshwa na changamoto za mepenzi.

Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu. Sifa hizo hizi zifuatazo.

1. Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.


2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .

3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatojali umeongea baya au zuri .
4. Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha. Hatakuacha mtu wa kuvizia vizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha.

5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatopenda kuwa nyuma na kukuacha bila msaada .

6.Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani (pesa au mali)

7.Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine

8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.

9. Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini, asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya maamuzi magumu .

10.Atakuwa tayari kuvumilia, hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe.


Naomba kujua jibu la swali hili fupi tu.

Kupenda ni nini? (base katika mapenzi ya jinsi mbili tofauti)
 
Back
Top Bottom