SOKETI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2010
- 206
- 50
Waswahili wanasema bora kukosea kujenga kuliko kukosea kuoa. Msemo huu unarihidhisha wazi kuwa swala la kuoa linahitaji busara na hekima ya hali ya juu. Ni kitu gani hasa kinachomwezesha mwanaume kutambua muda muafaka wa kuoa, Je ni fedha na hali ya kiuchumi, uzuri wa mwanamke unayetaka kumuoa, tabia yake, uhitaji wa kuwa na watoto, kutaka kuishi na mwanamke, shinikizo toka kwa wazazi na jamii nzima au swala la kuoa limekua ni fasheni(la kuiga).