Siendi Arusha

Siendi Arusha

waende makomredi,NCHEMBA
LUSINDE
NKAMIA
SERUKAMBA.
wakipiga matusi kidogo tu CHADEMA chaliii!!!

Wakija hawa CCM imekosa ushindi 100% na ukitoa hawa sijui utaleta akina nani??
Yetu macho.
 
Vuta Nikuvute Bhana ! ushaharibu sasa , ungewaacha waingie kwenye 18 kwanza ! hakuna Ccm Arusha ! Kama unabisha muulize Chatanda .
 
nenda jombaa ukale nyama kwa Mrombo na Kisongo then uwaambie kua unaumwa
 
Kwa aibu hii ya jana,ningejisikiaje. Wenzangu wa CCM pia muwe mnaangalia mbali.
 
Tumepokea ujumbe toka Makao Makuu ya CCM kuwa tunatakiwa kwenda Arusha kuhakikisha kuwa Wagombea wetu wa Udiwani katika Kata zinazorudia uchaguzi hapo Juni 16 wanaibuka na ushindi. Eti,tutoke hapa Dodoma mapema ili tuwahi Arusha kuanza 'kuwalisha sumu' wapigakura wa Arusha katika Kata husika. Eti,chama chetu kimejipanga kuibuka washindi dhidi ya wapinzani wetu hasa CHADEMA.

Mimi siendi Arusha. Tumeshashindwa kabisa uchaguzi huo wa Madiwani Arusha. Arusha CCM haiuziki,haiaminiki. Tulijitahidi kuwalaghai Madiwani wa zamani wa Kata hizo ili wahamie CCM. Wakakataa kuhama lakini wakaahidi kuwa 'kiburi' kwa CHADEMA. Wakafanya kweli.Wakafukuzwa. Sasa wanajiandaa kuhamia rasmi CCM na kusimamishwa kama Wagombea wetu.

Hatahivyo, siendi Arusha. Hao Madiwani wote wa zamani sasa hawaaminiki Arusha.Ni wasaliti kwa CHADEMA na wapigakura wao. Hawataweza kuiepusha aibu ya CCM pale Arusha. Nani atapambana jukwaani na Lema? Nani atamzidi kete Mawazo wa Sombetini? Sipo tayari kwenda kujidhalilisha. Arusha si mahali pa kwenda.

Pamoja na Tume ya Uchaguzi kupanga uchaguzi mwezi wa sita ili 'kuwazuia' akina-Lema Bungeni,bado niwajuavyo CHADEMA,wana timu kabambe ya kampeni hata bila Lema wa Arusha. Kwa hili la kwenda Arusha kusimamia harakati za uchaguzi wa Madiwani,nipo tayari kulaumiwa.Mimi siendi. Nitabaki hapa Dodoma kushuhudia 'vituko' vya Wabunge wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nieleweke kuwa: Arusha siendi.

VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)
mzee Tupatupa wewe ni noma!! uliona mbali maana hii ilikuwa aibu ya mwaka!! 4-0 sijui zingine ungezificha wapi kwenye koti... Nasikia jamaa aka savimbi alitoka nduki usiku wa manane bila kuaga -- vijana wakamwambia hii siyo singida ni A-Town.
 
Wanakudharau sana mzee vuta vuta lakini ukweli ni kwamba wangekuweka uwe mshauri wao wa karibu
 
mzee Tupatupa wewe ni noma!! uliona mbali maana hii ilikuwa aibu ya mwaka!! 4-0 sijui zingine ungezificha wapi kwenye koti... Nasikia jamaa aka savimbi alitoka nduki usiku wa manane bila kuaga -- vijana wakamwambia hii siyo singida ni A-Town.
Ilikuwa iwe 5-0 wamshukuru refa.
 
Arusha sio iramba, watu wanakamua kikwelikweli kavukavu tena live huku wanakuangalia usoni unavyosikilizia maumivu, wapi Shonza?
 
Back
Top Bottom