....ni marufuku kuwinda tembo eneo la Arusha....
Lema kachuja, the so called makamanda wameshamchoka na vituko vyake, wanadai kachemka sana, CCM ina nafasi ya kushinda Arusha, hata Lema akiwepo, mbowe, kibabu na wengineo, mje wote, ili tushinde fair and square, tutakuwepo sisi, chama si mtu mmoja, na haijawahi tokea hivyo,
Tumepokea ujumbe toka Makao Makuu ya CCM kuwa tunatakiwa kwenda Arusha kuhakikisha kuwa Wagombea wetu wa Udiwani katika Kata zinazorudia uchaguzi hapo Juni 16 wanaibuka na ushindi. Eti,tutoke hapa Dodoma mapema ili tuwahi Arusha kuanza 'kuwalisha sumu' wapigakura wa Arusha katika Kata husika. Eti,chama chetu kimejipanga kuibuka washindi dhidi ya wapinzani wetu hasa CHADEMA.
Mimi siendi Arusha. Tumeshashindwa kabisa uchaguzi huo wa Madiwani Arusha. Arusha CCM haiuziki,haiaminiki. Tulijitahidi kuwalaghai Madiwani wa zamani wa Kata hizo ili wahamie CCM. Wakakataa kuhama lakini wakaahidi kuwa 'kiburi' kwa CHADEMA. Wakafanya kweli.Wakafukuzwa. Sasa wanajiandaa kuhamia rasmi CCM na kusimamishwa kama Wagombea wetu.
Hatahivyo, siendi Arusha. Hao Madiwani wote wa zamani sasa hawaaminiki Arusha.Ni wasaliti kwa CHADEMA na wapigakura wao. Hawataweza kuiepusha aibu ya CCM pale Arusha. Nani atapambana jukwaani na Lema? Nani atamzidi kete Mawazo wa Sombetini? Sipo tayari kwenda kujidhalilisha. Arusha si mahali pa kwenda.
Pamoja na Tume ya Uchaguzi kupanga uchaguzi mwezi wa sita ili 'kuwazuia' akina-Lema Bungeni,bado niwajuavyo CHADEMA,wana timu kabambe ya kampeni hata bila Lema wa Arusha. Kwa hili la kwenda Arusha kusimamia harakati za uchaguzi wa Madiwani,nipo tayari kulaumiwa.Mimi siendi. Nitabaki hapa Dodoma kushuhudia 'vituko' vya Wabunge wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Nieleweke kuwa: Arusha siendi.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)
Tumepokea ujumbe toka Makao Makuu ya CCM kuwa tunatakiwa kwenda Arusha kuhakikisha kuwa Wagombea wetu wa Udiwani katika Kata zinazorudia uchaguzi hapo Juni 16 wanaibuka na ushindi. Eti,tutoke hapa Dodoma mapema ili tuwahi Arusha kuanza 'kuwalisha sumu' wapigakura wa Arusha katika Kata husika. Eti,chama chetu kimejipanga kuibuka washindi dhidi ya wapinzani wetu hasa CHADEMA.
Mimi siendi Arusha. Tumeshashindwa kabisa uchaguzi huo wa Madiwani Arusha. Arusha CCM haiuziki,haiaminiki. Tulijitahidi kuwalaghai Madiwani wa zamani wa Kata hizo ili wahamie CCM. Wakakataa kuhama lakini wakaahidi kuwa 'kiburi' kwa CHADEMA. Wakafanya kweli.Wakafukuzwa. Sasa wanajiandaa kuhamia rasmi CCM na kusimamishwa kama Wagombea wetu.
Hatahivyo, siendi Arusha. Hao Madiwani wote wa zamani sasa hawaaminiki Arusha.Ni wasaliti kwa CHADEMA na wapigakura wao. Hawataweza kuiepusha aibu ya CCM pale Arusha. Nani atapambana jukwaani na Lema? Nani atamzidi kete Mawazo wa Sombetini? Sipo tayari kwenda kujidhalilisha. Arusha si mahali pa kwenda.
Pamoja na Tume ya Uchaguzi kupanga uchaguzi mwezi wa sita ili 'kuwazuia' akina-Lema Bungeni,bado niwajuavyo CHADEMA,wana timu kabambe ya kampeni hata bila Lema wa Arusha. Kwa hili la kwenda Arusha kusimamia harakati za uchaguzi wa Madiwani,nipo tayari kulaumiwa.Mimi siendi. Nitabaki hapa Dodoma kushuhudia 'vituko' vya Wabunge wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Nieleweke kuwa: Arusha siendi.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam(sasa Dodoma)
Hamuwatakii mema hao wawakilishi wa wananchi wao? Nina wasiwasi Arusha bado wana kumbukumbu za matusi ya Lusinde kule Arumeru.waende makomredi,NCHEMBA
LUSINDE
NKAMIA
SERUKAMBA.
wakipiga matusi kidogo tu CHADEMA chaliii!!!
Mkuu POMPO huku usipate shida........................... ni kama unamsukuma mlevi.......
Kumbuka kata ya Daraja II ccm yote ilihamia kule, ukizingatia ilikuwa kata yao, lakini baada ya matokeo walikimbia kila moja njia yake.
Arusha hata Nape hatapoteza muda kuchungulia, ataishia Moshi.
Nina hamu kubwa na Mwigulu na Lusinde waje Arusha, wataaibika vilivyo.