Sielewi kwanini watu husherekea siku ya kuzaliwa

Sielewi kwanini watu husherekea siku ya kuzaliwa

Ushawahi kufikiria kujiua usiwepo duniani? Ukifariki dunia itapata hasara gani?

Ushawahi kuona movie inaitwa "It's A Wonderful Life" ?

It's a Wonderful Life - Wikipedia

Mkuu kufikiria kujiua sijawahi kwa kuwa ni lazima nife kwa nini nijiharakishe? Ila kwa nini nisherehekee wakat napita halafu hamna ukombozi au u free wa kuwepo hapa duniani?
 
Mkuu ulionalo wewe la kijinga kwa mwingine haoni kama ni la kijinga hata kwa sekunde. Hivyo binadamu hapa duniani KAMWE hawawezi kufanana. Wale ambao wanaona umuhimu wa kusherehekea siku zao za kuzaliwa waachwe washerehekee kwa raha zao na wale ambao hawaoni umuhimu wa kufanya hivyo pia ni haki yao kutosherehekea.

Kweli mkuu hili jambo ni la kijinga sana.
 
Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?

Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.

Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.

Sikushangai hata kidogo mkuu ila ulishawahi juiliza . Isingekuwepo ile siku uliyo zaliwa , Je Ungeufamu umuhimu wa uwepo wako hapa duniani? Ni watoto wangapi huwa hawajafikisha hata mwaka mmoja katika maisha yao.? Watu wanasherekea kwasabbu ndo siku ya maazimisho ya siku ya kwanza kwao ulimwenguni..
Watu wanasherekea sababu wanakuwa wamepata sababu zilizofanya wapate kuzaliwa na kuishi..
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Sikushangai hata kidogo mkuu ila ulishawahi juiliza . Isingekuwepo ile siku uliyo zaliwa , Je Ungeufamu umuhimu wa uwepo wako hapa duniani? Ni watoto wangapi huwa hawajafikisha hata mwaka mmoja katika maisha yao.? Watu wanasherekea kwasabbu ndo siku ya maazimisho ya siku ya kwanza kwao ulimwenguni..
Watu wanasherekea sababu wanakuwa wamepata sababu zilizofanya wapate kuzaliwa na kuishi..

Mkuu kwani nisingezaliwa kuna chochote ambacho kinge haribika hapa duniani? Uwepo wetu hauna mantiki tupo kama tupo ndo mana tunakufa.
 
Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?

Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.

Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.


Ungeanza na Krismasi kwanza kwa maana ndiyo chimbuko la kusherehekea siku ya kuzaliwa!
 
Kwenye maisha kuna maamuzi milioni kibao kila mtu anafanya maamuzi ya maisha yake hakuna mtu anaefanana maisha na mtu mwingine ndio maana wewe ukienda kulala kuna mtu anaamka wakati unaoa yupo anaetoa talaka mwingine anakufa yule anazaliwa nakushauri usipate wazimu na maamuzi ya watu maisha hayako uniform kwamba tutapenda au kuchukia wote waache wanasheherekea waendelee sidhani kama wanagusa maisha yako usishangae pamoja kufanya kila kitu kwetu ila wapo wanaomkataa Mungu,Tunaishi mara moja ni vema kuitumia hii nafasi kwa kila namna.
 
Alipozaliwa yesu watoto wengi wa kiume walio na umri chin ya miaka 2 walikufa, siku Herode alipokuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa Yohana mbatizaji alikufa kwa kukatwa kichwa. Yesu anasema afadhali siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.
 
Mkuu kufikiria kujiua sijawahi kwa kuwa ni lazima nife kwa nini nijiharakishe? Ila kwa nini nisherehekee wakat napita halafu hamna ukombozi au u free wa kuwepo hapa duniani?
Wanasherehekea maisha, kwamba wameweza kuishi na hawajafa, kwamba wamefanya mambo fulani na fulani.

Si lazima kusheherekea, ila hata ukiamua kutojiua tu ushasheherekea maisha, maana umeyapenda maisha kuliko kifo.

Kwa hiyo, kila siku ambayo hujaamua kujiua unasherehekea maisha bila kujijua.

Si lazima siku ya birthday.

Ukila chakula kizuri na kusema "chakulahiki kizuri kweli", hapo umesheherekea maisha.Kwenye kifo kadiri ya tunavyojua, huwezi kupata ladha ya chakula kizuri. Unapofurahia chochote, unasheherekea maisha. Hata unapopata mabaya, maadam unaishi, unasheherekea maisha, kwa sababu una nafasi bado ya kubadilisha hayo mabaya kuwa mazuri.

Kwa hiyo hata wewe kuja hapa JF kujumuika na waja wenzako ni kusheherekea maisha, ukifariki hutaweza kujibizana nami hapa JF.

Kwa hivyo, maisha yanasherehekewa kila siku, iwe ya birthday au si ya birthday.

Inawezekana ulikuwa hujui kwa sababu umeangalia kusheherekea kwa mtazamo finyu.

Mimi hapa kuanza kukuelezea habari hizi nasherehekea maisha, maana habari ya mimi kukaa mbali na wewe halafu tukabadilishana mawazo bila kuonana ni neema ya maisha, so far ninavyojua wafu hawawezi kubadilishana mawazo nasi hapa JF.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Alipozaliwa yesu watoto wengi wa kiume walio na umri chin ya miaka 2 walikufa, siku Herode alipokuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa Yohana mbatizaji alikufa kwa kukatwa kichwa. Yesu anasema afadhali siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa.

Naunga mkono hoja mkuu
 
Kusheherekea hii siku ni dalili ya ubinafsi, ila mimi naipendaga tu!
 
Wanasherehekea maisha, kwamba wameweza kuishi na hawajafa, kwamba wamefanya mambo fulani na fulani.

Si lazima kusheherekea, ila hata ukiamua kutojiua tu ushasheherekea maisha, maana umeyapenda maisha kuliko kifo.

Kwa hiyo, kila siku ambayo hujaamua kujiua unasherehekea maisha bila kujijua.

Si lazima siku ya birthday.

Ukila chakula kizuri na kusema "chakulahiki kizuri kweli", hapo umesheherekea maisha.Kwenye kifo kadiri ya tunavyojua, huwezi kupata ladha ya chakula kizuri. Unapofurahia chochote, unasheherekea maisha. Hata unapopata mabaya, maadam unaishi, unasheherekea maisha, kwa sababu una nafasi bado ya kubadilisha hayo mabaya kuwa mazuri.

Kwa hiyo hata wewe kuja hapa JF kujumuika na waja wenzako ni kusheherekea maisha, ukifariki hutaweza kujibizana nami hapa JF.

Kwa hivyo, maisha yanasherehekewa kila siku, iwe ya birthday au si ya birthday.

Inawezekana ulikuwa hujui kwa sababu umeangalia kusheherekea kwa mtazamo finyu.

Mimi hapa kuanza kukuelezea habari hizi nasherehekea maisha, maana habari ya mimi kukaa mbali na wewe halafu tukabadilishana mawazo bila kuonana ni neema ya maisha, so far ninavyojua wafu hawawezi kubadilishana mawazo nasi hapa JF.

Basi mkuu nimeishia kucheka tu bado sijapata jibu sahihi naiman ntalipata tu kwa nini tusherehekee siku ya kuzaliwa anaachwa alieteseka?
 
Basi mkuu nimeishia kucheka tu bado sijapata jibu sahihi naiman ntalipata tu kwa nini tusherehekee siku ya kuzaliwa anaachwa alieteseka?
Kama hujaliona jibu, labda hujataka kuliona.

Unakubali kwamba tunasherehekea maisha kila siku kwanza? Tuanzie hapo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kama hujaliona jibu, labda hujataka kuliona.

Unakubali kwamba tunasherehekea maisha kila siku kwanza? Tuanzie hapo.

Hapana mkuu kwenye suala la kusherehekea maisha kila siku bado kila uchwao ni changamoto tu bora ya jana.
 
Ni upumbavu tu, Birthday party! What for!
 
I second you. Ni kama kuiga mambo ya ajabu utakua watu wanafanya hadi mambo ya ajabu kisa birthday
 
Miye kila Mwaka nasahau, juzi namtembelea rafiki yangu ndiyo wanasema laza laza Leo siku yako ya kuzaliwa umekumbuka.
 
Tuwaulize Wakatoliki maana History inasema wao ndio walianzisha jambo hili la kijinga
Mimi mkatoliki lakini tangu nijitambue sijawahi kukumbuka kama kuna siku nilishawahi fanya au fanyiwa mambo ya hivyo ni kwa kuwa sijawahi kuona umuhimu wake
 
Back
Top Bottom