Sielewi kwanini watu husherekea siku ya kuzaliwa

Sielewi kwanini watu husherekea siku ya kuzaliwa

radika

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2014
Posts
20,450
Reaction score
32,291
Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?

Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.

Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.
 
Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?

Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.

Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.
Huwa wanasherehekea siku yao ya kuzeeka.
 
Mkuu hata mm huwa simtakii mtu heri ya siku ya kuzaliwa wala sitakagi mambo ya kuwishiwa hzo mambo, hamna chochote cha maana
 
Haramu Yako halali ya mwenzako mradi hawamker mtu acha washerekee.

Sijakataa mkuu ila huwa ina maana gani hiyo sherehe ktk maisha yake? Ni kipi hasa kinachomfanya asheherekee uwepo wake ikiwa tunapita?
 
Originally binadamu aliumbiwa kila siku iwe maisha ya furaha/sherehe..Kutokana na mabadiliko ya kidunia (tangu Siku alikula tunda katazwa), imekuwa vigumu kushereheka kila Siku. Hata hivyo, hii haimzuii kubuni siku kadhaa katika maisha yake..kupumzika na kustarehe..mojawapo birthday. Kuna sherehe nyingi sana na ukitafakari waweza ona hazina maana..huko vijijini hata ukijenga kibanda cha nyasi, kikikamilika unaangusha sherehe..mziki mzito..mradi mwili na roho vinaburudika maisha yanasonga. In short, whatever aina ya sherehe.. Lengo kuu ni kupumzika na kuburudika. Ni muhimu sana jambo hili litokee..tena mara nyingi. Lini unaamua kupumzika kila MTU na hoja yake. Kwamba kila nafsi itaonja mauti haizuii kufurahia uwepo wa MTU duniani. Kumbuka wengine huamini watapata mema/vitamu zaidi baada ya kufa..hawaogopi kifo kihivyo.
 
Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?

Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.

Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.
Ushawahi kufikiria kujiua usiwepo duniani? Ukifariki dunia itapata hasara gani?

Ushawahi kuona movie inaitwa "It's A Wonderful Life" ?

It's a Wonderful Life - Wikipedia
 
Vyote feki mkuu hapo
siku ya kuzaliwa ni muhimu kwa KUMKUMBUKA Muumba aliyekufinyanga kwenye tumbo la mama, kujipongeza na kusherekea kokote binafsi huwa siungi mkono. sherehe yangu huwa ni kusema maneno machache kwa Muumba na kutoq chochote kwa waja wake ambao ni wahitaji kama nikiwa na kitu. Ila mwaka mpya huwa haunihusu wala sisherekei maana mwaka mpya wangu ni siku ya kuzaliwa ule mwingine huwa siujali sana.
 
Haramu Yako halali ya mwenzako mradi hawamker mtu acha washerekee.
Sawa, ila mambo ya kulaumiana eti hujaniwishi au sijui nini siku yangu ya kuzaliwa yasiwepo. Na kuna pumbavu wengine eti wanadai na michango kama harusi vile!! Pita mbali kuleeee kwa hayo mambo kwangu.
 
Back
Top Bottom