Nakwambia hivi, maadam unaishi, na hujafa,na hujajiua, unasherehekea maisha kila siku.Hapana mkuu kwenye suala la kusherehekea maisha kila siku bado kila uchwao ni changamoto tu bora ya jana.
Binafsi huwa nasherehekea japo kimya kimya, sifanyi sherehe ila huna ni siku ya furaha kwangu.Katika maisha yangu hili jambo naona la ajabu sana pale mtu anapoandaa sherehe kubwa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa maswali ninayojiuliza kuna umuhimu gani wa hii sherehe kwa yeye kuwepo hapa duniani ambayo inamfanya aifurahie ikiwa tunakufa?
Kama hukuzaliwa dunia inapata hasara gani? Kama hamna hasara basi hakuna umuhimu wa uwepo wako hapa duniani kwa kuwa sherehe yako ya kuzaliwa haina manufaa yoyote na ni batili ikizingatiwa aliekuzaa kapata maumivu makali sana kuna muda ananusurika hata kupoteza maisha yake, angalau wakina mama wao ndo wangefanya sherehe ya kukuleta duniani kwa kuwa kaokoka kifo wakati wa kujifungua hapo kidogo ingeleta maana.
Mimi huwa sihangaiki kumtumia mtu salamu ya eti hongera kwa siku yako ya kuzawaliwa au kumchangia mtu katika sherehe ambazo zinanikera basi ni hii ya siku ya kuzaliwa.
unaf.i.r.w.a wewe sio bureTuwaulize Wakatoliki maana History inasema wao ndio walianzisha jambo hili la kijinga
Mkuu sio umasikini haina mantiki tuNilichojifunza hapa kutokana na watu wanavyocomment nimegundua Umaskini wa kutokuwa na hela ni mbaya sana!
Binafsi naona rika sahihi la kufanya "Birthday Party" ni miaka 0 hadi 12, huyu ni mtoto na furaha yake kubwa ni kusherekea siku yake ya kuzaliwa sambamba na watoto wenzie maana hajui chochote.
Umri mwingine wa kusherekea siku ya kuzaliwa ni miaka 50 na kuendelea , hapa unakuwa kama unamshukuru Mungu wako kwa mabonde na milima uliyovuka mpaka kufikia hapo maana wanasema ukifikia huo umri akili inarudi tena kwenye utoto.
Kijana Wa miaka 20 hadi 40 ni ngumu sana kukumbuka siku zake za kuzaliwa hivyo huwa tunaona kama haina umuhimu na ni kweli sio ya muhimu.