Sidney Sheldon Novels: Wale waliomsoma huyu Mwamba

Sidney Sheldon Novels: Wale waliomsoma huyu Mwamba

GuDume

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2015
Posts
6,700
Reaction score
14,633
Moja ya vitu ambavyo mpaka leo sijafanikiwa kuacha ni usomaji wa vitabu mbalimbali Fiction na Non- Fiction. Nimekutana na waandishi mbalimbali ndani na nje ya Tanzania kwa kupitia Vitabu vyao na leo hii ngependa kushare nanyi Mwandishi Nguli Sidney Sheldon.

Huyu mwandishi ni mmoja ya waandishi ninaowakubali nakumbuka mara nyingi nmekuwa hata nikikesha kusoma Novels za huyu Mwandishi.

Leo hii napenda nikupatie baadhi ya Vitabu vyake.

Screenshot_20200621-110951~2.png
Screenshot_20200621-111000~2.png
Screenshot_20200621-111008~2.png
Screenshot_20200621-111016~2.png
 

Attachments

Naona kaamua kumchafua Gwiji. Anamfahanisha na sijui Shigongo? Huyo Shigongo ni nani? Maana kama hata sijawahi kumsikia basi jamaa naona anafanya juhudi za kumchafua SIDNEY SHELDON.

Kama hujawahi kumsoma Sidney Sheldon ni bora ukanyamaza hana wa kufananishwa hapa duniani ukimfananisha na shigongo unamdhalilisha
 
Nimesoma kitabu chake The other side of me nikipata muda nitakimalizia nadhani kitakua kitabu bora miongoni mwa vitabu nilivyosoma.
 
Sidney Sheldon kipenzi cha roho yangu ❤
Nilianza kusoma vitabu vyake nikiwa std 5, cha kwanza kilikuwa The Stars Shine Down. Hicho ndo kitabu cha kwanza kusoma cha watu wazima. Mpaka namaliza hicho kitabu nilisema aiseee kumbe kuna vitu vizuri namna hii kwenye fasihi?
Mpaka sasa nimesoma vitabu vyake karibia vyote lakini nilichokipenda zaidi kilikuwa cha masista waliotoroka convent (nimekisahau jina mnikumbushe).
Huyu babu ndio alinifanya nisome vitabu mpaka nikawa na hisi kuchanganyikiwa kila nikipita bookshop.
Nimesoma vitabu mpaka nimefikia hatua ya kuweza kusoma kitabu cha kurasa 200+ chini ya masaa mawili.
Long live Sidney Sheldon!
 
Sidney Sheldon kipenzi cha roho yangu ❤
Nilianza kusoma vitabu vyake nikiwa std 5, cha kwanza kilikuwa The Stars Shine Down. Hicho ndo kitabu cha kwanza kusoma cha watu wazima. Mpaka namaliza hicho kitabu nilisema aiseee kumbe kuna vitu vizuri namna hii kwenye fasihi?
Mpaka sasa nimesoma vitabu vyake karibia vyote lakini nilichokipenda zaidi kilikuwa cha masista waliotoroka convent (nimekisahau jina mnikumbushe).
Huyu babu ndio alinifanya nisome vitabu mpaka nikawa na hisi kuchanganyikiwa kila nikipita bookshop.
Nimesoma vitabu mpaka nimefikia hatua ya kuweza kusoma kitabu cha kurasa 200+ chini ya masaa mawili.
Long live Sidney Sheldon!
Nothing Lasts Forever cha wale kina dada madaktari wa Embacadero County Hospital nacho ni kizuri sana. Windmills of the gods kitakuweka kwenye suspense to the very end of the book kukiwa na Argentine professional assassin Angel

Ila kwangu mimi the best kazi ya Sheldon ni The Doomsday Conspiracy cha Commander Robert Bellamy, akitumwa kuwa identify witnesses walioshuhudia ajali ya "weather baloon" kwenye kijiji kidogo cha Uterndof pale Sweden. Kitabu kile kina mambo meengi sana mazuri

Kwa wanaopenda sheria na mizungu yake ya kubwagana mahakamani basi apitie The Other Side of Midnight amuone wakili Napoleon Chotas ambaye hajawahi kushindwa kwenye kesi yoyote ya maana na kubwa anavyoigeuza sheria na wanasheria kwa kadri atakavyo. Sheldon is the best
 
Moja ya vitu ambavyo mpaka leo sijafanikiwa kuacha ni usomaji wa vitabu mbalimbali Fiction na Non- Fiction. Nimekutana na waandishi mbalimbali ndani na nje ya Tanzania kwa kupitia Vitabu vyao na leo hii ngependa kushare nanyi Mwandishi Nguli Sidney Sheldon.

Huyu mwandishi ni mmoja ya waandishi ninaowakubali nakumbuka mara nyingi nmekuwa hata nikikesha kusoma Novels za huyu Mwandishi.

Leo hii napenda nikupatie baadhi ya Vitabu vyake.

View attachment 1484952View attachment 1484953View attachment 1484954View attachment 1484955

Du unenigusa sana. Nimemalizana naye huyu Mwamba. Sasa naenda na David Baldacci, Tom Clancy - Jack Ryan. Robert Ludlum na wanachokuwa nembo yake. Ila Sheldon alikuwa kiboko. Unanua jina kabla hata ya kusoma. Reading Novels Ni Hobby yangu ya toka Form 2. hela nayonunua vitabu inaweza fanya makubwa. Ila ndo addiction yangu.
 
Du unenigusa sana. Nimemalizana naye huyu Mwamba. Sasa naenda na David Baldacci, Tom Clancy - Jack Ryan. Robert Ludlum na wanachokuwa nembo yake. Ila Sheldon alikuwa kiboko. Unanua jina kabla hata ya kusoma. Reading Novels Ni Hobby yangu ya toka Form 2. hela nayonunua vitabu inaweza fanya makubwa. Ila ndo addiction yangu.
Robert Ludlum naye ni habari nyingine
 
Back
Top Bottom