Siasa za Mbeya 2005-2010


Acha kujikweza umeongea na RCO, wakati hata humjui kwa jina.
 
Jamani na wewe ni mtanzania au mganda??? haya maneno nime ya highlight vipi???
Unaona ulivyo mjinga? Wewe ndio unasema hauko standard moja na Bambumbile? Naona ni kweli standard yako iko chini mno.

Masatu ameshaandika kitu hicho hicho, mtu mwenye akili huwezi kurudia kitu hicho hicho.

Wenye akili au uwezo wanasoma kwanza kabla ya kujibu. Wajinga huwa na papara na kukimbilia kujibu utafikiri kuna mashindano ya kuwahi.
 

Nashukuru hilo kosa nimeliona na nimefuta contribution yangu.

Ukweli wa mengine unabaki kama ulivyo kwamba msijikweze eti mnaongea sijui na RCO, sijui na kuku, yote haya hayajengi. Mteteeni mwakalinga kwa hoja zingine siyo kurekodi mikutano ya Dk. Mwakyembe na mnampelekea mwakalinga ili ajue atamu-attack vipi mpizani wake.
 

Nakumbuka hata kihiyo alikuwa engineer.
 
We mwana wa pateli Engineer Mshukuru sana Invisible anavyowakingia kifua humu sijui kwa sababu ni mwanachama mwenzenu wa CCM? Angeturudishia ile thread yetu iliyokuwa na hoja za kujadiliwa hii thread imekaa kikushoto sana.

Harafu mnamwita ndugu yenu kibarua mbona ata Mtanzania ni kibarua (kanusha) na ameweza kujenga majumba ila huyo dogo yeye hawezi kujenga au mpaka awe kibarua UK tu?
 
Acha kujikweza umeongea na RCO, wakati hata humjui kwa jina.

Magezi,

Wewe ni kilaza mno! Hapo ulipoweka nyekundu panasema "nimeongea na ofisi ya RCO", wewe unaongelea kumjua RCO kwa jina. Hivi unaelewa na maana ya ofisi ya RCO kwamba sio sawa na kusema nimeongea na RCO?

Bambumbile naona amekuweza kweli kweli. Inaelekea unakurupuka maana posts zako hizi mbili zimekuumbua.

Kwa taarifa tu ni kwamba kijana ambaye angetaka kumchoma Mwakyembe kwa kisu asingetolewa siku ya pili tena bila dhamana. Labda kama humjui Mwakyembe; angezunguka magazeti yote na TV zote kuelezea jinsi polisi walivyo wazembe.

Ukweli ni kwamba hata yeye anajua wamepika habari, sasa, wanasubiri waone kama wamelikoroga kwa kiasi gani. Wale vijana wake watatu matumbo yako moto; hata hapa mjini wamepotea na kujifungia. Walifikiri jambo dogo sasa limegeuka kubwa kweli kweli.

Aafadhali mwanzoni wangelikuwa na kosa moja tu la kumteka nyara huyo kijana. Lakini la kumzushia kwamba alitaka kumchoma kisu mbunge ndilo limeshutua watu wengi hapa. Inakuwaje mbunge anashirikiana na vijana wajinga kiasi hicho? Jamaa wenyewe jobless tu, kula yote inategemea mheshimiwa apate majungu afurahi na ndio na wenyewe washibe.
 
engineer wa mvua take a brake
sahau habari za mwakyembe for a month or so
mwakyembe chati yake inapanda siku hadi siku
na watu waliokutuma wamekuchuza kwa ajili huwezi kuanza kampeni wakati mwenzako ndio kwanza ametoka hospitali baada ya ajali ya utata, na sasa hivi chati yake ndio inakuwa kubwa....
na sisi watanzania hatuwapendi mafisadi sasa hivi, kwa hiyo kwa mwendo huu unaoendelea nao inaelekea mwakyembe atakumaliza kisiasa kabla hata ujachomoka
 

Kaka Shalom,

Wale wawekezaji uliosema unawaleta huku wako wapi? Achaa usanii wako. Kuwa Marekani na kujuana na wazungu sio sababu ya kuja kutudanganya vijana hapa.

Mbona toka uandike hapa JF kwamba wewe unaleta wawekezaji siku zinaenda tu.

Jamaa zako Kinanasi, Mwamlinge na Kilumbu wamepotea hapa mjini kwa aibu. Walichofanya ni kitendo cha unyama na ujinga mno na hata huyo rafiki yako mbunge kakosea kweli kuruhusu kijana akafungiwe nyumbani kwake.

Sasa tusubiri kinachofuata wiki kesho, wote watatu watakuwa charged kwa kosa la kuteka nyara. Mbunge amepona kwasababu ni mwanasiasa na polisi wanamwogopa shauri ya kelele zake.

Msalimie Malafyale. Mwambie harakati za kuwa mkwe zimefanikiwa, sitamshambulia tena, maana nilipokuwa mtoto nilifundishwa adabu.
 

Mkuu wewe uko upande upi hapo?? Wewe unamshahara kweli? hahaha... ila nimefurahi kwamba ukielimishwa unaelewa na huo ndo uungwana.
 
Mkuu wewe uko upande upi hapo?? Wewe unamshahara kweli? hahaha... ila nimefurahi kwamba ukielimishwa unaelewa na huo ndo uungwana.

Hapo umefulia bro! Engineer ni fundi na hata siku moja huwezi kumlinganisha na hao jobless akina Kinanasi, Mwamlige na Kilumbu.

Hivi ni wangapi jobless wa wilayani wanaweza kuwa na uwezo wa kusoma na kuchangia JF?

Hapa JF ukiwa na uwezo mdogo tu wa kufikiri unaweza kujua mambo mengi kuhusu wachangiaji bila hata kuwajua wao kwa sura.

Kama ninayehisi mimi ndiye engineer; basi mambo yake sio mabaya kabisa kule Kyela.
 

Asante kiongozi nimekupata ila mwakalinga lazima tumshinde tu.
 


Mwana wa Pateli? Shalom kwahiyo Engineer ni Mhindi?..au mi sijakuelewa?..Ila Mwambieni jamaa yenu bana hii sio nzuri kabisa,ameanza kuvuruga kampeni,au ameona maji shingoni?
 
Engineer,

Nina wasi wasi kama kwenye hizo milioni 400 huna mgao kidogo kwa sababu naona una nguvu kweli ya kampeni....kwi..kwi...kwi
 

Sikonge,

Weye umechelewa wapi ndugu yangu? Kisu chenyewe si hiki hapa ambacho kishapigwa picha na ni cha Kigeni mitaa ya Uajemi? Sasa si Uunganishe nukta



Kwi kwi kwi au ni Bwa ha ha ha
 
Sasa mwakalinga akifulia utakula wapi mkuu, make hadi simu za kufanyia kazi anawanuulia??

Engineer,

Nina wasi wasi kama kwenye hizo milioni 400 huna mgao kidogo kwa sababu naona una nguvu kweli ya kampeni....kwi..kwi...kwi

Huyu George Mwakalinga kweli bahiri saana. Yaani kapewa milioni 400 na mafisadi na kaenda kununua simu mbili za Ericsson. Halafu silaha ya kumuuwa Mwakyembe kanunua kisu cha kukunja?

Nilitegemea ataenda kuwapa akina Zombe wamuondoe Dr. loo, kumbe kaenda kununua kisu cha kukunja. Yaani Mwakalinga na kusoma kote kule na kuishi Poland, ameshindwa kuagiza Wauwaji wa kulipwa kutoka Ukraine au Russia na kaja na kakisu ka kukunja? Huyu jamaa MPARE sana.

Hiki kisa kinanikumbusha kituko kimoja cha Kijasusi. Baada ya ndege kugonga WTC pale New York, basi na Wanyamwezi nao wakaamua kufanya kufuru kwa kugonga gorofa refu Tabora. Jengo hilo la Mkuu wa Mkoa lilishambuliwa na Gaidi hao na nilipofika pale nikakuta jamaa wawili wako uchi na nyungo zao. Alikuwepo Mzungu mmoja ambaye alicheka saaana na kusema "Huu Mkoa wa Tabora, hata magaidi wake wamechoooka!!"

Naanza kupata wasiwasi kama hizo milioni 400 alizopewa Mwakalinga zinaweza kuwa ni Dola za Mughabe (Zimbabwe Dollar).
 
Sikonge,

Weye umechelewa wapi ndugu yangu? Kisu chenyewe si hiki hapa ambacho kishapigwa picha na ni cha Kigeni mitaa ya Uajemi? Sasa si Uunganishe nukta



Kwi kwi kwi au ni Bwa ha ha ha

Duu, Mchungaji, ngoja nifunge na JF maana hii imekamilisha weekend yangu. Hii kisu inachinja hata Tembo ha hahaa hahaa.
 

Huyu jamaa bila shaka anatoka Uganda, nadhani tunatakiwa kuwakarimu watu kama huyu. Jamaa anaonyesha kabisa kiswahili siyo lugha yake, lakini anajitahidi sana. Mkuu Said usikate tamaa, karibu na uendelee kuchangia, tutakuwa tunakuelewa. Karibu sana.
 
Harafu mnamwita ndugu yenu kibarua mbona ata Mtanzania ni kibarua (kanusha) na ameweza kujenga majumba ila huyo dogo yeye hawezi kujenga au mpaka awe kibarua UK tu?
Shalom,

Naona hata yule Mandeleni wa Kyela akisikia ulichoandika hapo juu atakucheka sana. Atasema kumbe Kyela kuna kichaa kuliko yeye?

Labda ndio ule ule wivu wa maneno ya Mkapa, "Mitanzania mingine ina wivu wa kijinga"

Nimesoma posts zako nyingi juu ya Mwakalinga, nafikiri una wivu wa kijinga.
 
lazima waende na kisu maana yake walijaribu ajali wakashindwa, siunajua mwakalinga ndio alikuwa mzamini wa ile ajali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…