Siasa za Mbeya 2005-2010

Mutwa,

Mbona hizo paragraph ulizowekea red zinaongelea watu wawili tofauti?

Ya mwisho nafikiri ina maana ya Mwakalinga aka Mtanzania kama wengine tunavyoamini japo yeye hajathibitisha nasikia for legal reasons.

Mmoja ni mwakalinga huyo kibarua na mwingine Mwakalinga aka Mtanzania.
 

Mutwa,

Naelewa una maana gani lakini ungesoma vizuri baada ya hiyo paragraph inayomwongelea huyo kijana kibarua, inayofuata kwa vyovyote inaongelea Mwakalinga mwingine. Soma hiyo ya kwamba hizo zilikuwa sms za Mwakalinga na vijana wake wa Kyela. Sidhani kama huyo kijana mwenyewe angeweza kuwa na vijana wake tena Kyela.

Of course uandishi wa hapa JF ni wa haraka haraka na wakati mwingine hata kwa msomaji ambaye hujasoma thread nzima ni rahisi kuelewa tofauti.
 

Sasa unataka tusome gazeti la mtanzania?? Lakini tusubiri tu mwisho wa haya yote ni 2010, tusiwe na haraka ya kuhukumiana. Swali hapa ni kwa nini alikuwa anarekodi mkutano??
 
Sikonge,

Habari nilizozinasa sasa hivi hapa ni kwamba Mheshimiwa mbunge ana haha kumtafuta IGP Mwema asaidie. Sijui atamsaidia nini wakati ukweli wote uko wazi.

Pia alikuwa anamgombeza mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Kyela na kudai kwanini amemtoa kijana Dan nje tena bila masharti yoyote. Akaambiwa hawaweki rumande watu ambao hawana makosa. Pia akamwambia case hii yote inasimamiwa na RCO na RPC na akitaka awaulize wao.

Police wanasema hawataki kukurupuka na kufanya makosa ya wale wenzao wa Iringa. Wanaenda taratibu na kila ushahidi kuuweka sawa. Mtu hawezi kutumia uongo ule ule mara mbili.

Nasikia RCO ni moto wa kuotea mbali, jamaa akaamua ampigie IGP ambaye naye kamkaushia, akaishia kuongea na wasaidizi.

Amelikoroga mwenye wacha alinywe, sisi watoto wa kijuweni tunasema amefulia.

Jumatatu kuna mkutano wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na huenda hili jambo likajadiliwa maana tayari viongozi kadhaa wa mkoa wametuhumiwa na mheshimiwa kwamba eti kuna sms zao. Watataka waonyeshwe hizo sms.

Kama kawaida mimi nitawaletea habari. Engineer kwa breaking news za Kyela ni hatari tupu, mwache Masanilo apasuke bichwa!
 
Sasa unataka tusome gazeti la mtanzania?? Lakini tusubiri tu mwisho wa haya yote ni 2010, tusiwe na haraka ya kuhukumiana. Swali hapa ni kwa nini alikuwa anarekodi mkutano??

Kwasababu kwenye mikutano yake vijijini anatoa majungu kwamba Mwakalinga kahongwa milioni 400 na akina Lowassa. Huo ulikuwa ni ukusanyaji wa ushahidi wa hizo tuhuma.

Ku record mkutano wa hadhara sio kosa.
 
kwasababu kwenye mikutano yake vijijini anatoa majungu kwamba mwakalinga kahongwa milioni 400 na akina lowassa. Huo ulikuwa ni ukusanyaji wa ushahidi wa hizo tuhuma.

Ku record mkutano wa hadhara sio kosa.

hivi una wasiwasi kuwa lowasa na rostam hawajahonga kumwondoa mwakyembe? Hivi lowasa kukumsikia pale bungeni alivyolalamika kuhusu ripoti ya mwakyembe, na je hukumwona mama regina lowasa akiangua kilio kule kwenye gallery ya nunge?

wewe umehongwa na nani mpaka unaandika haya hapa? Sisi tunakaa mbeya na tunaifahamu mbeya acha kujidanganya
 

Na wewe umehongwa na nani kuandika hapa? Acha upumbafu wako.

Kwahiyo kila anayegombea ubunge na Mwakyembe basi kahongwa na Lowassa?

Mwakalinga mwenyewe ana miradi yake ya kutosha wala hahitaji kuhongwa na mtu.

Mbona yeye Mwakyembe anapewa pesa na Mengi? Nani kalalamika kuhusu yeye kudhaminiwa na Mengi?

Mpambano utaamuliwa na wananchi kwa kupima maendeleo ya Kyela na wala sio pesa. Huyu jamaa yenu anagombana na kila mtu hapa wilayani, anafikiri watu ni wajinga? Mtashangazwa kweli 2010.

Sasa anaanza hata kuteka vijana, huyo ni mwanasiasa kweli?
 
You college boys shut up, Dr. Mwakyembe is there to stay, we have seen how strong is against fisadis. We need more MPs like him now why campaigning against? Ni mbunge wa wanyonge, achane njaa ya vyeo.
 

Nilicho kigundua hapa wewe ni mmoja wa hao vijana, na kama unatumwa na mwakalinga sijui amekulipa ngapi. Nashangaa unaanza oh...mara kijana alikamatwa saa 8...mara oh...alifikishwa polisi saa 2 mara saa 3, yote hayo uliulizwa na nani?? Mara unasema safari hii mtu atafungwa!! ah... angalia unaweza kufungwa wewe kwa sababu huna immune na kifungo.

Hata kama humpendi mwakyembe mwache afanye shughuli zake za siasa, na 2010 atawashinda tu labda mfanikiwe kumuua lakini msisahau Mungu yupo na anawaona.
 

Kwanza wewe ni mchanga sana hapa JF so huwezi kumpasua kichwa Mkuu masanilo. Isitoshe wewe ni limbukeni wa masuala ya siasa na hujui vyema Dr. Mwakyembe anavyoendesha siasa zake. Unasema anamtafuta IGP amsaidie, wewe unachukua vimaneno kwenye vijiwe ndo unaleta hapa.

Unajipa sifa eti kwa breaking news wewe ni hatari?? tangu lini? wewe wa juzi, na hata kama, subiri upewe sifa siyo unajipa visifa!!! Kuna watu wanatoa michango constructive hapa JF na huwa hawajawahi jisifu hata siku moja, sasa wewe baada ya kupata jani ndo unaibuka eti na breaking news, nyoo!
 
Niseme tu kwamba mtu yeyote anayebeza juhudi za akina mwakyembe et al. ana matatizo ya akili.
 
Niseme tu kwamba mtu yeyote anayebeza juhudi za akina mwakyembe et al. ana matatizo ya akili.

Wewe nafikiri ndiye una matatizo ya akili. Nani anabeza kazi ya Mwakyembe kwenye Richmond?

Kwasababu alifanya kazi nzuri Richmond basi ndio ajichukulie sheria mkononi mpaka kuanza kuteka vijana?

Soma hotuba zake, hata sehemu moja haongelei maendeleo ya Kyela. Kama anataka kuwa rais wa nchi si agombee urais?

Kyela watamwajibisha kwa kushinda kufanya kazi za kusukuma maendeleo wilayani kwake na badala yake ni migogoro tu.

Mbona Dr. Slaa anafanya kazi na RC wa CCM? Yeye kila siku ni malalamiko tu RC ananikwamisha. Hivi kazi za RC na mbunge mbona ni tofauti sana?

Tatizo lake ni kutokukaa Kyela; sasa baada ya kutokea Mwakalinga ndio anajifanya kukaa Kyela lakini badala ya kuunganisha watu analeta vituko vya kuteka vijana na uwongo eti simu ina sms za vigogo. Nimeongea na ofisi ya RCO wanasema ni usanii tu wa Kyela. Kweli Kyela inahitaji mbunge wa namna hiyo?
 
ebanae, wewe Mkama unatoka Mara? mbona watu wa huko hawana ukabila? duh! upo kikabila kinoma mzee. Mbona unaondoa muunganiko wa vita dhidi ya ufisadi? acha hizo bro.

Mkuu nemesis,

Nimeipenda sahihi yako. Kibaya ni kuwa naona hata Kyela hiyo sahihi ndiyo imefika na kuwakolea haswaaaa!!!!

Mwaka 2010 kazi ipo. AHADI HEWA itabidi wabunge wakome kutowa.

Mjinga akierevuka mwerevu mdanganyifu yupo mashakani.
 
MkamaP,

Hapo umekandamiza kinoma. Eti Kimaro mpinga ufisadi, hiyo vichekesho ya mwaka.

Si angalia wanavyomsifia Mengi wakati yeye mwenyewe fisadi tu.

Tumewagundua, huku kusini wasahau, hawatapata kitu.

Hivi kweli Mbowe anaweza kuwa rais? Hii ni pure joke! CHADEMA tuletee mtu mwingine sio huyo bomu lenu.
 
Lakini kwa nini wewe unataka tukuamini kila unachosema juu ya issues hizi ? Inajulikana weye ni nani, na kuna kila sababu za kuamini kuwa mafisadi wamekupandikiza !

No wonder kila kukicha mmekuwa mkijifanya kuanzisha matawi na mashina huko UK ! Janja yenu ilishashtukiwa siku mingi, na yule "nyoka mkuu" Mr. O si alikuwa huko kabla ya kuteuliwa...?
 
Nani amuue Mwakyembe? kamuharibia nani?

Hii tesa tesa hii, Mwakyembe anaona Sifa sasa, anaona inamuongezea chati, lakini si vizuri, just imagine wewe ni yule kijana!
 
Ng'wanza Madaso;
Join Date: Mon Aug 2009
Posts: 11
Thanks: 0
Thanked 5 Times in 4 Posts
Rep Power: 0
MLIKUWA MKISOMA KAMA WAGENI SASA MMEJIUNGA

Mh Ng'wanza Madaso,
Uko sawa hapo juu kuwa mimi ni mugeni humu ndani mwa JF. Kwa kuwa wewe unahelekea kuwa ni mwenyeji humu JF hebu nielimishe, sisi hambao tulikuwa tunasomaga kama WAGENI kwani ni makosa kuhamua kujiunga na kuchangia? Au unanishambulia kwa kuwa nimesema kitu hambacho wewe hakikupendezea? Kama ni hivyo si ungeshambuliaga tu pointi nilizotoa badala ya kunishambulie eti mimi nilikuwa nasoma na baadaye nikahamua kujiunga. Usemi wa kizungu unaosemaga kuwa "attack the message not the messenger" nadhani inabidi kuutafakari kama unapenda kufanya hivyo kwa faida yako.
 

Mkuu, nothing personal nimeona niweke sawa kidogo hapo juu
 

You are not of my standard so I can not argue with you in this platform.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…