Siasa za matukio sio japo zinakutoa kwa muda! Wapi shangazi?

Titicomb

JF-Expert Member
Jan 27, 2012
11,334
17,835
Popote ulipo Shangazi kipenzi cha watu nakusalimu na kukujulia hali.

Kwanza unisamehe shangazi kwa uandishi wangu mbovu unao chosha wasomaji.
Hii yote sababu nilimkosa kwenye simu anko Pascal Mayalla anipe 'shoti kozi' ya uandishi.

Nauliza mbona kimya kingi na huku matukio uliyo kuwa unayapinga yanaendelea mfano domo la krasia linaingia luba kule mjengoni?

Mwenye kinga mjengoni anaambiwa hauko huru kiasi hicho kwa utakacho ongea dhidi ya mjengo wenyewe na wakazi wake.

Anaambiwa ukijifanya unajua tunakukatia mrija wa chakula ktk makongamano mawili na atakae kutetea tunamkatia makongamano matatu ashindwe kulipa madeni yake ya chakula aliyokopa akitegemea chakula cha makongamano ya mjengoni. Tuone atapata wapi nguvu za kuongea akiwa na njaa.

Anapewa adhabu ya kumkumbusha kinga yako ipo kwa ajili ya kukulinda utakapo ongea unachohisi 'ukweli' dhidi ya walio nje ya mjengo.

Waulize binamu zangu Haah Lima wa 'Cow way' na Godie(Godii) chalii wa arachuga tupo nao kijiwe hapa wanapiga mihayo njaa kali. Hawa wanajua vizuri kadhia hii ya mjengoni.

Babu Kifimbo cheza mzee wa kazi (Job) na Bibi mdogo wa Ku-Tulia wamechachamaa kukagua lugha za kushusha hadhi na kukiuka haki na madaraka ya mjengo.

Nimemuita kifimbocheza sababu pale mjengoni ana lifimbo likubwaaa la ule udogo wa kung'aa ulioleta kizaa zaa cha makinikia.

Sasa Shangazi kipenzi cha watu unajua mimi na wapwa zako wengine hapa kijijini hatujui sheria tunaomba kauli yako.

Sema japo neno dogo tu na nafsi zetu zita suuzika.

Tunaomba neno lako lifafanue haki, hadhi na madaraka ya mjengo na wakazi wake ni zipi?
Zinaishia wapi na zinamhusu nani wakati gani?

Je mjengo ukiwa una lega lega ktk kusimamia wapishi wa keki ya kijiji cha 'matanga na nyika ' kilicho sheheni kinywaji cha 'zanzi na bar' za kutosha' nani anawakumbusha?

Na lugha gani imerusiwa kutamkwa au kukatazwa mjengoni?
Maana dhohofu au dhaifu ni sifa sio tusi, japo ni sifa ya aibu kwa uzembe.

Sasa kwa mfano mzembe anatakaje aheshimiwe au apewe hadhi na haki huku hatekelezi wajibu wake?

Au tumesahau kanuni hii ya "Haki na Wajibu"?

Hadhi inakuja kwa kuwajibika ktk majukumu yako kwa kijiji na jamii unayo iwakilisha.

Kwanza ngoja niulize hizo kanuni zipo kurasa nyingi kama za vitabu vya baibo na msahafu?

Kama kurasa chache kwanini usituwekee hapa au utusomee wanakijiji tujue kabisa tuwafundishe wawakilishi wetu wakienda huko mjengoni wajue wako huru kuukosoa mjengo kwa maneno haya na haya ni mwiko, au wasi ukosoe kabisa mjengo wala babu pekee mwenye fimbo ya dhabu kubwa sana mjengoni na hapa kijijini? Maana hii kinga hadhi na madaraka ya mjengo yanaonekana ni makubwa sana kuliko hata aliyowekewa kumlinda kiongozi wa kijiji asikosolewe.

Na mjengo wenyewe upo ndani yakijiji lakini una kinga na haki kubwa sana au madraka ya mjengo ni makubwa sana kukataa kukosolewa, huku mkulu wa kijiji amepewa kinga ya shitakiwa tu kwa makosa ambayo anafanya akiwa kakalia ukulu wa kijiji lakini kanyimwa haki au hadhi kubwa kama ya mjengo ya kuto kukosolewa. Ina maana mjengo ni wa siri za ajabu sana ukuu wake umezidi wa mkulu wa kijiji kuhusu kukosolewa?

Kwani humo mjengoni kuna siri kali kama za mjengo wa wahashi huru (freemasons) na ndio maana mliobdoa mlizima virusha sauti na picha mtembeo(radio na TV)?

Kwanza naomba nitoke nje ya mada kidogo, naomba umkumbushe babu hiyo fimbo ikifika Geita soko la vipande vya kung'aa ni pesa chafu, aimarishe ulinzi huku kijijini kuna ukame sana wa vipande vya fedha. Au kama vipi tuuze tukanunue dawa maana naona fimbo yenyewe ipo ipo tu haina kazi wakati huku kijijini tunakesha kutafuta pesa ya matibabu ya wakazi wa mjengoni.

Sasa turudi kwako shangazi kipenzi cha watu, ule ukali ulikuwa dhidi ya kiongozi mkuu wa kijiji tu? Au idara zote zinazo finyanga domo la krasia?

Ukimya huu tujiongeze tutambue hasira zilikuwa ni kisasi na kiongozi mkuu pekee au mambo yako kibiashara hayaendi sasa umekata moto?

Shangazi, nakumbuka tulikuonya siasa za matukio ni upepo unaovuma na kufifia kisha kutokomea kabisa baada ya muda mfupi huku nyuma ukikuachia madhara makubwa sana.

Shangazi ile kasi ya kuwasimanga wana nzengo wazee wa kimila wa kijiji ilikuwa kujaribu kukimbia kabla ya kusimama na kutembea kwanza.

Kuwatukana wa kabila la kisiasa wa babu na baba yako ilikuwa sawasawa na mjukuu anae kwenda kumtukana bibi yake eti ni mchawi mla watu wakati amelelewa na huyo bibi mla watu. Ina maana wakati bibi anapika nyama za watu mlikuwa mnakula wote. Alikuwa anakulisha na haukukataa. Umekulia kwa chakula cha nyama ya watu. Hiyo ndio tafsiri ya kelele zako.

Ungetuacha tuwatukane sisi ambao hatukuonja japo mchuzi wa nyama hiyo haramu kupitia ktk maziwa ya mama zetu.

WOSIA KWA SHANGAZI NA BABU:-

"SHANGAZI USIACHE KUCHIMBA CHOO KWA MSALA UPITAO"

"BABU KIFIMBO CHEZA CHA DHAHABU, MUNGU ANAKUONA UJUE KUNA SIKU UKIFIKA KWAKE UTAJIBU KAMA ULIKITETEA KIAPO CHAKO CHA KULINDA KATIBA KWA KUISIMAMIA SERIKALI YA KIJIJI CHETU KUTEKELEZA WAJIBU WAKE NA KULINDA KATIBA.
NI BORA USINGE APA KWA JINA LAKE"
 
Back
Top Bottom