Siasa na dini

Ulimbo

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
3,767
4,035
Kuna baadhi ya viongozi wa vyama na serikali wamekuwa waki toa maneno, wakiwataka viongozi wa dini wasijiingize kwenye siasa.

La ajabu hao viongozi ni waumini wa hizo dini, na walipoapishwa, waliapa kwa kushika vitabu vya dini zao.
Pia wanapokuwa kweny matukio mbalimbali, wanawashirikishia viongozi wa dini kufanya dua.

Sasa wanaposhauriwa na hao viongozi wa dini, wanawaambia mambo ya siasa wawaachie wanasiasa, na wao wabakie kwenye mambo ya dini.

1692997215938.png
 
Kuna baadhi ya viongozi wa vyama na serikali wamekuwa waki toa maneno, wakiwataka viongozi wa dini wasijiingize kwenye siasa...
Wimbo wa Taifa hili wanaloliongoza unaanza na dini."MUNGU IBARIKI TANZANIA" Wakiwa kwenye kupewa Ofisi inaanza Ibada na kutaka waombewe ila Wakitenda Maovu wanasema msituingilie sasa tuwaulize nyie Hamuogopi Mungu sasa kwenye majumba ya Ibada mnakwenda kufanya nini?

Waambie tu wawajibu viongozi wa dini kitaalamu inawezekana labda hawajaelewa .
 
Wimbo wa Taifa hili wanaloliongoza unaanza na dini."MUNGU IBARIKI TANZANIA" Wakiwa kwenye kupewa Ofisi inaanza Ibada na kutaka waombewe ila Wakitenda Maovu wanasema msituingilie sasa tuwaulize nyie Hamuogopi Mungu sasa kwenye majumba ya Ibada mnakwenda kufanya nini?

Waambie tu wawajibu viongozi wa dini kitaalamu inawezekana labda hawajaelewa .

Wanawapenda tu viongozi wa dini pale wanapowaombea na kuwatamkia baraka, wakionyo au kukosolowa, hawataki kua hilo.
 
Back
Top Bottom