Siasa inavyoua U - Tanzania wetu

Siasa inavyoua U - Tanzania wetu

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
1,126
Reaction score
2,658
Siasa zimekuwa sumu inayoua utaifa wetu kimya kimya kuja kushituka tutajikuta mateka kati yetu wenyewe

Leo vyuo vikuu vimekuwa wazalishaji wakubwa wa machawa badala ya wataalamu

Vijana wengi wameamua kuingia kwenye siasa za vyama kwa ajili ya kulinda kesho yao. Hawana uhakika wa kuishi bila kuwa machawa wa kijani na njano

Kutwa kucha wanahangaika kutafuta kumbukumbu za picha wakiwa wamevaa magwanda ya kijani na njano au fulana za "Mama asemewe" ilimradi tu akimaliza chuo atumie kama sehemu ya kujitetea kusaka tonge lake

Ajira za serikali haziangalii uwezo bali itikadi. Wengi wameajiriwa kwa "kudhani" ni kwasababu wa kujiweka kimbelembele katika siasa

Wale wanaoachwa wakihangaika mtaani wanaamini kadi za chama ni sehemu ya kigezo cha ajira

Walioko kwenye utumishi wa umma wamefunga midomo kukemea makosa, kukosoa hata kushauri wakihofia ulimi ukiteleza watakosa ugali wao

Wale wanaotaka vyeo hawawezi kuongea bila kumtaja asiyewafahamu wale asiyehiyehitaji kutajwa kila muda. wanadhani kufanya hivyo ndio kulinda vyeo vyao

Maskini ya Mungu kila program utawakuta hata kwa kujilazimisha

Marathoni wapo, mchakamchaka wapo, makongamano wamo, mwenge wapo...haijalishi wanaumwa wala wanamajukumu mengine ya kifamilia, wanaamini wasipoonekana watasemwa

Mungu tuepushe na hii dhambi ya siasa kula utu wetu
 
Taifa linazidi kupoteza wataalamu kila kukicha kwa sababau ya itikadi.
 
Mpuuzi wewe unaanzisha nyuzi za madeni yako ila uchawa huoni kuwa ni tatizo la taifa that's y uko indepted harlot wewe.
Mkuu hapa umemshambulia pasipo kumuelewa, nadhani lengo lake alitaka kujifunza jambo kutoka kwenye hii mada.

Ila the way umemu-attack inashangaza sana.
 
Siasa zimekuwa sumu inayoua utaifa wetu kimya kimya kuja kushituka tutajikuta mateka kati yetu wenyewe

Leo vyuo vikuu vimekuwa wazalishaji wakubwa wa machawa badala ya wataalamu

Vijana wengi wameamua kuingia kwenye siasa za vyama kwa ajili ya kulinda kesho yao. Hawana uhakika wa kuishi bila kuwa machawa wa kijani na njano

Kutwa kucha wanahangaika kutafuta kumbukumbu za picha wakiwa wamevaa magwanda ya kijani na njano au fulana za "Mama asemewe" ilimradi tu akimaliza chuo atumie kama sehemu ya kujitetea kusaka tonge lake

Ajira za serikali haziangalii uwezo bali itikadi. Wengi wameajiriwa kwa "kudhani" ni kwasababu wa kujiweka kimbelembele katika siasa

Wale wanaoachwa wakihangaika mtaani wanaamini kadi za chama ni sehemu ya kigezo cha ajira

Walioko kwenye utumishi wa umma wamefunga midomo kukemea makosa, kukosoa hata kushauri wakihofia ulimi ukiteleza watakosa ugali wao

Wale wanaotaka vyeo hawawezi kuongea bila kumtaja asiyewafahamu wale asiyehiyehitaji kutajwa kila muda. wanadhani kufanya hivyo ndio kulinda vyeo vyao

Maskini ya Mungu kila program utawakuta hata kwa kujilazimisha

Marathoni wapo, mchakamchaka wapo, makongamano wamo, mwenge wapo...haijalishi wanaumwa wala wanamajukumu mengine ya kifamilia, wanaamini wasipoonekana watasemwa

Mungu tuepushe na hii dhambi ya siasa kula utu wetu
Mimi nawafahamu watu walioajiriwa pasipo kuwa wanachama wa chama chocote cha siasa.
Nawafahamu waliojiriwa na hawajawahi kupost picha ya Samia hata kwa dkika moja.
 
Mimi nawafahamu watu walioajiriwa pasipo kuwa wanachama wa chama chocote cha siasa.
Nawafahamu waliojiriwa na hawajawahi kupost picha ya Samia hata kwa dkika moja.
Nakubaliana na wewe, ni kweli kabisa watu wa hivyo lazima wapo na lazima kila ajira zinapotolewa watakuwepo

Hoja ni kwamba wa aina hiyo wako wa ngapi na wa aina ile nyingine wako wangapi?
Na sifa za hao wa aina iliyotajwa kulinganisha na wanaokosa wakati mwingine unakuta wanaoachwa wana sifa nzuri zaidi
 
Nakubaliana na wewe, ni kweli kabisa watu wa hivyo lazima wapo na lazima kila ajira zinapotolewa watakuwepo

Hoja ni kwamba wa aina hiyo wako wa ngapi na wa aina ile nyingine wako wangapi?
Na sifa za hao wa aina iliyotajwa kulinganisha na wanaokosa wakati mwingine unakuta wanaoachwa wana sifa nzuri zaidi
Sawa.
 
Back
Top Bottom