Siamini kama nimepatwa na kukoroma

Siamini kama nimepatwa na kukoroma

Itakua hapo kwenye issue ya uzito, sio utani nimeongezeka kutoka kg 68 mwaka 2022 mpaka 81 kg mpaka hivi sasa.

Ngoja nifanye mpango wa kupungua uzito.

Shukrani sana mtaalamu.!
Sijawahi penda kuwa mwembamba issue ya KG Mbona una uzito wa kawaida Sana..

Mimi mwenyewe ndio KG zangu 80,81,82,83 kg kwa consecative 5years
Labda sabab iwe ingine sio uzito
 
Sijawai penda kua mwembamba issue ya KG Mbona una uzito wa kawaida Sana..

Mimi mwenyewe ndio KG zangu 80,81,82,83 kg kwa consecative 5years
Labda sabab iwe ingine sio uzito
B.M.I yangu inanitaka niwe na uzito wa 62 kg sasa huenda uzito wangu kulingana na urefu wako upo normal au over weight kidogo ukilinganisha na mimi.!
 
Nilikua nawashangaa wanaolala halafu wanakoroma, sasa juzi nilipata fursa ya kuwa jirani na mwenzangu opposite sex.
Nilishangaa ananiambia eti usiku nilikua nakoroma, nikabisha Kwa ujasiri wote, siku inayofuata ikabidi anirekodi nikiwa nakoroma.! Dah sikuamini kama ndo mimi.

Hivi hii kitu inasababishwa na nini na nini tiba yake!??

Kibaya zaidi mpaka mchana nikijilaza kidogo tu, naanza korooo korooo.! Dah yamenikuta.!
hahahahahah a kata rufaa bro!
 
C & P

Habari za kazi mheshimiwa Michuzi,
nilipitia hapa kwenye blog yako nikakuta bwana Chumaka wa Korogwe akiomba msaada wa namna ya kutatua tatizo lake la kukoroma ambalo linamnyima mkewe usingizi.Majibu mengine niliyoyasoma yalikua ya ajabu na pia hayakuweza kumsaidia bwana Chumaka.

Na vifaa vingi vilivozungumzwa kwa mtu aliyopo Korogwe sidhani angevipata kwa urahisi. Kwakua kulikua na comments zaidi ya 35 nikahisi nikiweka na yangu pale wengi hawataiona,naomba uiweke peke yake ili iweze kusaidia watu kama mimi ilivyonisaidia.

Niliwahi kusafiri na mzee wa kijapani kwenda mikoani kikazi na katika safari zetu kuna siku ilibidi tulale kwenye mji mdogo ambao tulikosa vyumba na kupata kimoja tu ambacho kilikua na vitanda viwili.Watu wengi walishaniambia kuwa nakoroma sana nilalapo usiku.Siku ya pili tulipokua tunapata kifungua kinywa yule mzee akaniambia nina tatizo la kukoroma na atanifundisha namna ya kulitatua bila kutumia dawa,mbinu ambayo wanaitumia kwao.

Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho,rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20.

Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma.Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.

Mzee huyu aliniambia mtu anaekoroma mwili wake haupati mapumziko ya kutosha na mara nyingi huamka huku bado akihisi uchovu na husababisha watu wengine kunenepa sana na wengine kukonda ikitegemea mwili wa muhusika na homoni zake.

Tatizo langu liliisha kabisa baada ya wiki 2 lakini naendelea na mazoezi hata mara mbili kwa wiki ili misuli isilegee tena.Kwakua naishi peke yangu ilibidi nimchukue waifu wa siku 2-3 anihakikishie sikoromi kabisa.Nikiamka siku hizi sihisi uchovu ule wa zamani.

Mdau Ibrahim,D'salaam.
 
Aisee umenivunja mbAvu
Mkuu, walioimba ule wimbo wa "wanaume tumeumbwa matesooo" hawakukosea.
Mateso ni mengi.
Starehe zote tulizonazo zinaanza na K, i.e kula, kulala, kunya na kquma.
Sasa usingizi na wenyewe anataka auwekee masharti?
Ni mwendo wa kuvuta resi tu kama scania inapanda sekenke
 
Back
Top Bottom