Siafu wameua vifaranga shambani

Siafu wameua vifaranga shambani

funzadume

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2010
Posts
13,650
Reaction score
21,485
Usiku wa kuamkia leo siafu wamevamia shambani kwangu na kuua vifaranga vya wiki tatu 56 na vya miezi miwili na nusu 31 vilivyokuwa kwenye banda maalum la kukuzia
Kwa wenye uzoefu nifanye nini kudhibiti siafu shambani

Nisaidieni wataalam
 
Ili kuzuia siafu kwenye banda la kuku, hasa lililopo shambani, tumia mbinu hizi salama kwa kuku:

Njia Asili & Salama za Kuzuia Siafu
1. Chenga za Mkaa au Majivu
- Zungusha banda au sehemu wanapopitia siafu kwa kuweka majivu au changa za mkaa. Hii huwakera na huwazuia kupita.

2. Limao au Ndimu
- Menya limao au ndimu na uweke maganda pembezoni mwa banda. Harufu yake haipendwi na siafu.

3. Pilipili ya unga au Karafuu
- Tumia pilipili ya unga au karafuu zilizopondwa sehemu zinapopitia siafu. Wanaepuka harufu hii.

4. Kutengeneza Mtaro wa Maji
- Kama inawezekana, tengeneza mtaro mdogo wenye maji kuzunguka banda. Siafu hawapiti kwenye maji.

5. Sima nzito ya unga wa mahindi
- Mwaga unga wa sembe uliochomwa kidogo kwenye njia zao. Huwa wanaukula lakini hushindwa kuumeng’enya, na huangamia.

---

⚠️ Kumbuka:
  • Usitumie dawa kali za kuua wadudu ndani au karibu na banda — zinaweza kuua kuku au kuharibu mayai/nyama.
  • Hakikisha chakula cha kuku hakimwagiki hovyo — harufu ya chakula huvutia siafu.
 
Pole sana mkuu,nilikuwa mbeya kuna mradi wangu fulani.
Nilishuhudia msafafara wa siafu ukienda kwenye mabanda ya mifugo.

Screenshot_20250808-122251.png

Wadau wakaniambia ni miezi ya misafara yao,so cha kufanya mwagia oili chafu kwenye njia zao.nilifanya hawajarudi tena
 
Sikitiko la kwanza kutoka kwa ephen_

Kuna mwamba alinitonya kuwa sabuni ya unga inasaidia kufukuza siafu, nilishajaribu mara kadhaa nikafanikiwa, japo hawakuwa wengi sana, fanya kumwaga sabuni ya unga ya kutosha kuzunguka nyumba ya vifaranga, hawatakatiza hapo.
 
4. Kutengeneza Mtaro wa Maji
- Kama inawezekana, tengeneza mtaro mdogo wenye maji kuzunguka banda. Siafu hawapiti kwenye maji.

5. Sima nzito ya unga wa mahindi
- Mwaga unga wa sembe uliochomwa kidogo kwenye njia zao. Huwa wanaukula lakini hushindwa kuumeng’enya, na huangamia.

---

⚠️ Kumbuka:
  • Usitumie dawa kali za kuua wadudu ndani au karibu na banda — zinaweza kuua kuku au kuharibu mayai/nyama.
  • Hakikisha chakula cha kuku hakimwagiki hovyo — harufu ya chakula huvutia siafu.
Asante sana nitajaribu mbinu hizi
 
Sikitiko la kwanza kutoka kwa ephen_

Kuna mwamba alinitonya kuwa sabuni ya unga inasaidia kufukuza siafu, nilishajaribu mara kadhaa nikafanikiwa, japo hawakuwa wengi sana, fanya kumwaga sabuni ya unga ya kutosha kuzunguka nyumba ya vifaranga, hawatakatiza hapo.
Asante sana kwa ushauri. Kweli JFC ni kisima cha maarifa
 
Usiku wa kuamkia leo siafu wamevamia shambani kwangu na kuua vifaranga vya wiki tatu 56 na vya miezi miwili na nusu 31 vilivyokuwa kwenye banda maalum la kukuzia
Kwa wenye uzoefu nifanye nini kudhibiti siafu shambani

Nisaidieni wataalam
chukua chaki ya ii wanayotumia mashulen kisha koleza skwa kuchora msitar sehem penye matobk siafu wanapopenda kupitia.
 
Yaani jana Ijumaa nilienda shamba nikakuta mifugo inaendelea vizuri sana. Saa nane usiku napigiwa na kijana wa shamba siafu wameua kuku wadogo
 

Attachments

  • IMG_2050.jpeg
    IMG_2050.jpeg
    545.5 KB · Views: 33
  • IMG_2053.jpeg
    IMG_2053.jpeg
    1.2 MB · Views: 26
Hao said wadogo kwenye picha wote wamekufa kwa kuumwa na siafu
 
Nunua dawa inaitwa Akheri Powder kopo kubwa ua Bakiller, pia mwaka oil chafu kuzunguka eneo lote la banda
 
Ili kuzuia siafu kwenye banda la kuku, hasa lililopo shambani, tumia mbinu hizi salama kwa kuku:

Njia Asili & Salama za Kuzuia Siafu
1. Chenga za Mkaa au Majivu
- Zungusha banda au sehemu wanapopitia siafu kwa kuweka majivu au changa za mkaa. Hii huwakera na huwazuia kupita.

2. Limao au Ndimu
- Menya limao au ndimu na uweke maganda pembezoni mwa banda. Harufu yake haipendwi na siafu.

3. Pilipili ya unga au Karafuu
- Tumia pilipili ya unga au karafuu zilizopondwa sehemu zinapopitia siafu. Wanaepuka harufu hii.

4. Kutengeneza Mtaro wa Maji
- Kama inawezekana, tengeneza mtaro mdogo wenye maji kuzunguka banda. Siafu hawapiti kwenye maji.

5. Sima nzito ya unga wa mahindi
- Mwaga unga wa sembe uliochomwa kidogo kwenye njia zao. Huwa wanaukula lakini hushindwa kuumeng’enya, na huangamia.

---

⚠️ Kumbuka:
  • Usitumie dawa kali za kuua wadudu ndani au karibu na banda — zinaweza kuua kuku au kuharibu mayai/nyama.
  • Hakikisha chakula cha kuku hakimwagiki hovyo — harufu ya chakula huvutia siafu.
FANYA HAYA YOTE ILA ZAIDI HIYO YA KWANZA MAJIVU NI MAZURI SANA UNAZUNGUSHIA BANDA LOTE

AU OIL CHAFU MWAGA KWA KUZUNGUSHIA ENEO LOTE HAWATAVUKA.

KWENYE NYUMBA YA SIAFU UA KINYONGA KISHA MPELEKE UKAMTUPIE HAPO WATAHAMA MILELE AU CHOMEAPO MATAILI AU YEBOYEBO/MALAPA.



ahsante sana ephen_ nimejifunza hizo za pilipili
 
Back
Top Bottom