SIAFIKI utaratibu wa watu kula msibani

SIAFIKI utaratibu wa watu kula msibani

Hili suala la kula misibani jamii ziliigana likaenea na kuwa kawaida ila kwa sasa limeanza kuwa mzigo kwa wafiwa. Kuna misiba ukihudhuria usitegemee sana kula chakula, kula wali/pilau, utakula ugali kwa maharage plus mlenda/mchicha/matembele/chainizi. Ukikataa kula utaonekana unaringa na huna ushirikiano msibani, bora ule tu. Misiba mingine tunatangaziwa chakula ni cha wageni tu nyie wengine mtafute pa kwenda kula. Misiba mingine huandaa chakula kidogo kinaishia kwa watu wachache tu wa mwanzo kwenye foleni ya bufee! Usiende msibani ukitegemea utashibia huko, nenda na hela ya kula migahawani kabisa ili usije ukaumia njaa. Chakula cha msibani si cha kutegemea sana, kikiwepo kula kama dharura tu
 
salaam,

Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.

Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.

Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.

Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.

Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.

Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA

Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa
watu ni sehemu ya faraja katika msiba. aidha, nijuavyo, kwa jamii ya Afrika hususan Nchini, chakula zaidi ya shibe pia ni njia/platform ya kuwafanya watu kujumuika pamoja, kuzungumza au kushikamana. Achilia chakula, watu pia hujitoa kwa namna kadhaa katika kufanikisha msiba. Hivyo, changamoto ya eneo moja isichukuliwe kama ndio udhaifu wa jambo kwa ujumla wake.
 
Hela si zinachangwa ?
Kwenye jamiii yangu huwa hela zinachangwa, na watu wanajitoa sana ! Hiyo hela kunakuwa na kamati ya kutatibu mambo yote kuanzia mazishi, vinywaji na vyakula .....

Then salio linalobaki wanapewa wafiwa !!!!
Kuna vyama vingi vya kijamii vya kusapotiana sana , sijajua unatoka ukanda gani ama hamshiriki matukio ya wenzenu mwisho wa siku mzigo unawaelemea !
 
Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.
Mkuu hii issue kwa ninavyoelewa mboni inafanywa na majira wana-organize wanafanya kila kitu kuanzia kupika na mengineyo sana sana ni kupewa tu ratiba na nini kitafanyika mwanzo mpaka mwisho au hao wao hua hawana ushirikiano na majirani zao wanaowazunguka?

Ingawa kuna msiba mmoja ulitokea sehemu fulani nikaona watu hawakwenda kwanini kwa sababu msiba umetokea mbali ila huyu mtu sababu aliekufa kule mbali ni Baba yake na yeye huku kafungua milango kafungua mapazia kaweka msiba majirani kuuliza kunanini wanaambiwa kuna msiba msiba wa nani wanaambiwa kafiwa na Baba yake kwa hio msiba upo wapi wanaambuwa haupo hapa ila mtoto hapa kaamua kuweka matanga ushaelewa?

Kwa hio ni majirani ndio wanashughulika kwenye msiba hususani kwa watu wa hali ya chini sababu huo mzigo familia haitoweza kwa hio linapita daftari donee donee mwenye 500 mwenye 1000 wanaunganisha kinapatikana chochote hivyo maisha yanaenda ndio inavyokua,

Sasa hapo wewe imekuaje? Maana hata wewe hapo naona kijana anahangaika na pikipiki baada ukasaidie kuchimba kaburi msiba upite salama wewe umekuja kuandika JF inakuaje hapo mkuu?
 
Kula hakuwezi kuepukika kwenye Mambo ya Msiba au matukio yanayochukua karibu Siku nzima.

Zamani kwenye msiba watu walikuwa wanaenda na vikapu vya mchele, unga, maharage, mahindi, na mafuta, kuni n.k.

Siku hizi kuna rambirambi.

Ishu hapa isemwe sio vizuri mtu uende kwenye msiba mikono Mitupu na wewe ni mtu mzima.
Hii ndio hoja
 
Utaratibu wenu wa ovyo. Misibani wafiwa hawafanyi kazi. Majirani, Marafiki, vikundi mbalimbali, ndio wanafanya. Mfano hapo wewe inabidi uweke simu chini umsaidie mfiwa kuchimba mashimo ya kusimamisha tents.
Nijuavyo Mimi wafiwa wana coordinate mazishi nyuma ya pazia lakini kazi zote zinafanywa na wanakijiji.

Nimemzika baba yangu mwaka juzi (Mungu amrehemu), sisi wanafamilia ilikua ni vikao tu, kazi kupika, kuleta vitu, sijui Nini ni wanakijiji wanafanya.
 
Jamii zinatofautiana na watu pia kama huoni haja ya kula ama kunywa msibani usile waache waliopikiwa wale.

Sasa mtoa mada dunia ya leo mfiwa unafànya kazi za kuchimba matent n.k alikuwa hashiriki misiba na wenzie? Huyo kijana ama baba ??

Dunia ya Leo watu wana vikundi kulingana na ukanda hasa wakiwa mikoa hii ambapo sio nyumbani

Hata nyumbani wazee wana vikundi lukuki

Sasa sijajua ninyi ni jamii gani ???

Ety bwashee wageni kutoka Dar es salaam, Arusha, Moshi na Nairobi wapite nyuma ya nyumba ya ng''ombe cc min -me
 
salaam,

Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.

Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.

Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.

Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.

Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.

Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA

Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa
Msiba ni gharama - Yes. Ila bro. umeongeza kchumvi kidogo e.g. nakunukuu: "......aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah....."
Wapi hiyo mkuu??! Kwa kawaida katika msiba wanaochakarika zaidi ni majirani, marafiki(Washkaji) na shughuli au mchakato mzima hadi marehemu aweze kusitirishwa zinaeleweka. Wakubwa hushughulika na maandalizi nyeti e.g. Utoaji wa Taarifa; utunzaji wa michango kutoka kwa wahudhuriaji, sanda n.k. Vijana huwajibika kuandaa kaburi n.k. Mfiwa huwajibika kutoa Maelekezo ya Ushauri nini kifanyike n.k.
Hoja ya kula ni muhimu kwani sio wote waliohudhuria msibani wanaishi karibu na hapo palipotokea msiba. By the way, kiasi fulani cha gharama hupunguzwa kwa michango iliyokusanywa.
 
salaam,

Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.

Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.

Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.

Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.

Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.

Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA

Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa
Uongo unakusaidia nini Sheikh? Sema kama watu wamemsusia labda huwa haendi kwenye msiba ya wengine? Huko hakuna ndugu na jamaa mpaka mwenye msiba achimbe mashimo?
 
Jamii zinatofautiana na watu pia kama huoni haja ya kula ama kunywa msibani usile waache waliopikiwa wale.

Sasa mtoa mada dunia ya leo mfiwa unafànya kazi za kuchimba matent n.k alikuwa hashiriki misiba na wenzie? Huyo kijana ama baba ??

Dunia ya Leo watu wana vikundi kulingana na ukanda hasa wakiwa mikoa hii ambapo sio nyumbani

Hata nyumbani wazee wana vikundi lukuki

Sasa sijajua ninyi ni jamii gani ???

Ety bwashee wageni kutoka Dar es salaam, Arusha, Moshi na Nairobi wapite nyuma ya nyumba ya ng''ombe cc min -me
Mpaka sasa hivi bado namshangaa huyu mleta mada!
 
We mtoa mada sema tu hao majirani zako hawashiriki kwenye misiba basiii, lakini msiba ukitokea majirani na marafiki ndio wanaohusika kufanya hizo shughuli, na unasema tusile? Hiyo ni big no kula ni sehemu ya ushirika wetu kama wanajamii husika, kwamba huyu marehemu na hawa walibaki ni washirika wenzetu after all chakula huwa kidogo sana huwezi sema naenda kushibia msibani no, wanaohangaika kufanya michango ni hao hao majirani na ndugu wengine, wanaochimba kaburi ni hao hao majirani
 
Chakula bali wao ndio wanatakiwa wapikiwe na waandaliwesalaam,

Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.

Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.

Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.

Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.

Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.

Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA

Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa
Hata Kiislamu haifai wafiwa kupika na kuandaa chakula bali inataki wapikiwe na wapewe chakula , shida Waislamu wengi hawalijui hili na kupelekea kufanya makosa kutengemeacwafiwa wafanye kazi na wawape chakula
 
Back
Top Bottom