The unpaid Seller
JF-Expert Member
- Oct 27, 2019
- 2,353
- 6,916
salaam,
Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.
Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.
Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.
Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.
Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.
Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA
Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa
Huenda wazo lilikua jema watu wanapofika kuwafariji wafiwa pia wale hapo ili kuweka mshikamano.
Lakini utaratibu huu binafsi naona haufai sana maana ni kama umekua mzigo kwa wafiwa hasa misiba ya familia za hali ya chini.
Kuna msiba umetokea hapa mtaani kwetu (Mungu awafariji wafiwa pia amrehemu marehemu) aise wafiwa hapa wanahangaika mara kijana anachimba mashimo ya kuweka mahema mara kapanda pikipiki amefuata kuni akirudi anaingia chumbani kwake analia uchungu wa kufiwa baba mzazh akitoka nje awahudumie wageni jamani daaah.
Nimeshuhudia misiba mingi ya familia za chini wafiwa ni kama huwa wanapata mzigo kwa watu kuja kutoa faraja.
Mara nyingi utaona wanapika chakula kikiiva wao ndio watazunguka kugawa chakula kwa wageni yote hii pia ni kutokana waTanzania tumezoea ukarimu kuwakarimu wageni jambo linalowafanya wafiwa kupewa mzigo wakati wanapitia kipindi kigumu.
Na hapo utakuta mimtu inaenda msibani inarundikana vikundi na kupiga story za siasa au simba na yanga huku wafiwa wakitarajiwa wawe wakarimu kwa kuwahudumia wageni hawa eti wamekuja "kufariji". HII SIO SAWA
Mara nyingine msiba ukiisha kuna vitu viliazimwa kama masufuria, sahani, maturubai, viti, na kutokana na ustaarabu mbovu wa "wageni wafariji" labda vimepotea au vimeharibika mzigo hua unaachwa kwa familia ya wafiwa