Si salama kujenga juu ya makaburi

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,845
723dbc7262cc2b870745e01e34bf17f5.jpg


Pale ndipo penye makazi ya wafu, watu waliokuwa hai na kuishi juu ya ardhi sasa wameshuka na kupumzika pale ! Ile ni miili tupu lakini tusisahau kuwa roho zao hazichezi mbali hata kama zitaenda kutangatanga huko na huko lakini ile energy ipo pale

Kujenga chochote juu ya makaburi ni kutafuta bifu na marehemu ni kuwaingilia kwenye makazi yao rasmi! Kwani huna pengine pa kujenga?
Makaburi ya zamani yalikuwa makubwa sana, mengi yalijengwa mfano wa nyumba milima nk angalia ma pyramid ya Misri nk...makaburini ni sehemu iliyoheshimika mno na kwa namna fulani kuogopwa

0ff5815e92266564cfac029359b38645.jpg


Wengi wetu tunajua kabisa kule vijijini tuna maeneo rasmi ya kifamilia ya kuwazika waliotutangulia na makabila mengi hufika makaburini mara moja au mbili kwa mwaka kuyafagilia kufanya ibada na matambiko! Kwa baadhi yetu hata mambo yanapoharibika kifamilia au kiukoo hurudi makaburini na kuomba rehema ulinzi na hata msamaha kwa wakubwa Waliolala pale

Kuna visa vingi vya makaburini vingine vya kweli vingine vya uongo na vingine vipo lakini vimekuzwa mno...pamoja na hayo yote bado makaburini panabaki mahali maalum penye kustahili faragha na heshima yake
Tunavyo visa vingi kwenye maeneo yote ambayo makaburi yaliondolewa ama kuhamishwa kiholela kwa ajili ya kufanya mambo mengine kama ujenzi wa shule hospitali barabara nk nk...maeneo hata yamekuwa yakikumbwa na matukio mbalimbali hasa ajali na vifo

Dunia yetu ya kisomi na maendeleo ya kiteknolojia inatupumbaza na kutufundisha ujinga mwingi...tusitekwe na mambo ya kisasa na kisayansi...makaburini kuna maisha ya wafu paheshimiwe

419695739090b4454eaddc0d49ac8524.jpg
 
nakumbuka niliwahi ingia skymark mall vingunguti kipindi inajengwa, yaani makaburi yapo kushoto mafundi wanajenga kulia tena yana misalaba kabisa sio kwamba hayaonekani
Inasemekana hata mwananyamala hospital ilijengwa juu ya makaburi ndio maana ile hospital pamoja na juhudi zote za kuiboresha lakini wahudumu wote kwa nyanja zote ni vichwa maji
nenda ile stand ya daladala ya zamani ya arusha mjini pale usiku kuanzia saa 6 ujionee mambo ya ajabu.lile eneo nalo walihamisha makaburi
 
Huo wa leo afadhali Mkuu, kuna mwingine aliuanzisha juzi sikumbuki jina lake. Nikajua tu ule uzi utakuwa unatisha nikaamua niufungue kulikuwa na mapiccha ya ajabu ajabu nikaachana nao haraka sana. Threads za mshana jr siku hizi naziangalia mara mbili mbili kabla ya kuamua nizipotezee au nizifungue.

Najuta kwann nmeisoma hii mada saa hizi. Naogopa hatar.
 
mshana jr umemfunika MziziMkavu siku hizi kwa habari za kiroho
Mimi Tabia yangu huwa sishindani na mtu katika kuweka Topic humu jamvini niko busy sasa na wagonjwa wa Ukimwi, wagonjwa wa Hepatiti B Virus na wagonjwa wa Saratani ndio maana sijaweka siku nyingi Topic mpya. Nimemuachia Mkuu.@Mshana jr aendelee kuweka vitu vyake hongera.
 
Mim Tabia yangu huw asishindanina mtu katika kuweka Topic humu jamvini niko busy sasa an wagonjwa wa Ukimwi, wagonjwa wa Hepatitib Virus na wagonjwa wa Saratani ndio maan sijaweka siku nyingi Topic mpya. Nimemuachia Mkuu.@Mshana jr aendelee kuweka vitu vyake hongera.
Nimekumic mm bhana, ebu tuletee ya Vidonda vya Tumbo bhana watu huku mitaani wanatapeliwa na Herbal Clinics/Hospitali hawaponi.

Tafadhali sn, shule yako huwa ni nzr sn. Japo mm sina ila naweza jifunza kujikinga.
 
Huo wa leo afadhali Mkuu, kuna mwingine aliuanzisha juzi sikumbuki jina lake. Nikajua tu ule uzi utakuwa unatisha nikaamua niufungue kulikuwa na mapiccha ya ajabu ajabu nikaachana nao haraka sana. Threads za mshana jr siku hizi naziangalia mara mbili mbili kabla ya kuamua nizipotezee au nizifungue.
Mkuu.@Bak usiogope Thread za mshana ni za kawaida tu hazitishi hivyo. Au kuna zinazo tisha Topic zake mkuu.@Mshana jr? nionyeshe nipate kuziona basi.
 
Binadamu tunatofautiana Mkuu. Mie sipendi kuangalia picha za wafu ni picha ambazo zinakukosesha raha na silazimishwi kuziangalia hivyo hakuna tatizo pale ninapoamua kuepuka kuziangalia. (Au kusoma story za wafu)

Mkuu.@Bak usiogope Thread za mshana ni za kawaida tu hazitishi hivyo. Au kuna zinazo tisha Topic zake mkuu.@Mshana jr? nionyeshe nipate kuziona basi.
 
Back
Top Bottom