Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.

Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.

Pascal Mayalla Hivi Katiba inaposema "... kwa kufuata utaratibu uliwekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria" ina maana ngani?? Usitufanye wote humu JF ni nyumbu??!!
Anachokisema Pasco ni kwamba hivyo vipengere vya katiba na vya kwenye sheria ya vyama vya siasa ndiyo vibadilishwe. Katiba siyo Amri toka mbinguni kwamba haibadilishiki!
 
Makala nyingine ndeeefu, hv Paschal huwezi kufanya summary na ukaeleweka!! Hoja zako nyingi zimejurudia rudia bila sababu. Nirudi kwenye mada yako, kweli kama ulivyosema umeandika mawazo yako lkn mimi nayapinga mawazo yako na nayaona dhaifu sana. Kwanza unapaswa ujue kuwa kila mchezo una sheria na kanuni zake. Mfano kwenye mpira wa miguu, mpira ukitoka ubavuni mwa uwanja utarushwa kwa mikono japo mpira wenyewe ni wa miguu na kipa anaruhusiwa kutumia mikono yake kudaka mpira eneo maalumu. Sasa hata siasa zina sheria zake, mbunge, diwani au kiongozi yeyote wa kuchaguliwa ana haki na hiari ya kujiunga na chama chochote cha siasa na pia ana haki ya kuondoka kwenye chama alichopo. Katiba inaruhusu hali hiyo ambayo hata Nyalandu na Lowasa waliitumia. Kusema sheria ya uchaguzi inapingana na katiba na wakati huo huo unasema kipengele cha katiba kilibadilishwa ili kulazimisha uwakilishi utokane na chama, inapnesha ni namna gani unaandika kwa hisia badala ya ukweli ulivyo. Kumbe kipengele kilibadilishwa kisheria kuzuia mgombea huru sasa hoja zako zote ulizoandika zinaonekana za kipuuzi. Unaposema kikundi cha watu wachache kiliamua kutunga sheria hiyo una maana gani? Kwangu mm kikundi cha watu ni CCM, lkn CCM si ndio yenye ridhaa ya wananchi na ndio maana nakuambia rule of the game ktk siasa ni kupata ushindi mkubwa hasa wa wabunge ili kuweza kufanya maamuzi. Na mnapo taka kufanya hivyo, ni lazima mwombe ridhaa hiyo kwa wananchi na hivyo mkipata ridhaa mnatekeleza. Unaposema chaguzi za marudio zinaigharimu nchi na wananchi, nikuulize umethamisha marudio ya uchaguzi in terms of money, je, unaweza kutupa gharama za kutokuwa na uwakilishi? Maana inavyo elekea unalalamika viongozi kuhamia CCM na sio kuacha nafasi zao ingewezekana hata wangeamua kujiondoa kwenye chama, napo ungeitishwa uchaguzi. Kwa hiyo ndugu Paschal, uamuzi wa kuhama chama ni haki ya kikatiba na kuomba uongozi wa kisiasa kupitia chama cha siasa ni haki ya kikatiba iliyotolewa ufafanuzi kisheria na Mahakama ilizingatia hilo na wako sahihi kabisa. Kabla ya sheria hiyo, haki ya mgombea huru ilikiukwa nakubali lkn baada ya marekebisho, hakuna ukiukwaji tena wa katiba. Kwa hiyo ndugu Paschal, maandiko yako yanajengwa na hisia na chuki dhidi ya CCM ambayo yanakutoa kwenye weledi wa kudadavua mambo.
ficha upumbavu wako mkuu, unapinga maelezo marefu nawe unarudia kuandika kwa urefu na bora ungeandika mambo ya msing ni upumbavu mtupu.
 
Anachokisema Pasco ni kwamba hivyo vipengere vya katiba na vya kwenye sheria ya vyama vya siasa ndiyo vibadilishwe. Katiba siyo Amri toka mbinguni kwamba haibadilishiki!
Soma heading ya mada ya Mayalla ndiyo utaelewa alikuwa ana maana gani!!
 
Hawa ndio hoja wanazojijenga. Anashindwa kuzungumzia katiba ambayo inafanya uchaguzi uwe mchezo wa kuigiza! Anashindwa kuongelea Tume ya Uchaguzi ambayo viongozi wanachaguliwa na Rais na wapo pale kwa discretion ya Rais kitu ambacho kinapelekea kuwa na mgongano wa maslahi. mwandishi makini angei-attack hii sheria kwani sio constitutional
.
Hapa nimezungumzia katiba
P

Wanabodi,

Shurti la Mgombea Uongozi wa Umma, Kudhaminiwa na Chama cha Siasa ni Sheria Mbovu, ni...
Kinyume cha Katiba,
Kinyume cha Universal Declaration of Human Rights
Kinyume cha The United Nations Human Rights Committee,
Kinyume cha African Chatter of People and Political Rights
Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.

Declaration of Interest
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wazalendo wa nchi yangu, ambaye sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa sababu siasa za vyama za vingi Tanzania, hazichezwi katika uwanja ulio sawa, hivyo ushindi hupatikana kwa mbinu Zaidi kuliko kwa kura, ninaziita ni siasa za demokrasia change, hivyo kwenye mada hii, haya ni mawazo yangu, kila mtu anao uhuru wa mawazo yake, ambao unapaswa kuheshimiwa hata kama hukubaliani na mawazo hayo. Kwa wale ambao hawakubaliani na mawazo yangu, tutofautiane kwa hoja, kwa kupangua hoja zangu na kuleta hoja mbadala.

Watanzania Tufanye Siasa za Ukweli, Tuachane na Siasa za Hovyo Hovyo.
Tufike mahali sisi Watanzania, wazalendo, wenye nia njema na maendeleo ya kweli ya taifai letu hili masikini, hatuwezi kukaa kimya kwa kuendelea kukumbatia sheria mbovu, za uchaguzi, na kuendelea kuwawabesha masikini wa Tanzania, mzigo wa gharama za uchaguzi wa marudio, ulnaosababishwa na kwa sababu za kijtakia, zinazotokana na siasa za hovyo hovyo.

Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo wa kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!.

Kwa Nini Sheria Yetu ya Uchaguzi ni Sheria Mbovu, Bad Law.
Kifungu 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.

Sheria hiyo inasema hivi na hapa ninanukuu

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukatokea kikundi fulani cha watu, kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho kaiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993 Rev. Mtikila alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.


Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au wa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheri”.

Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali maombo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, Kiukweli kabisa, uamuzi huu sio utii wa Mhimili wa Mahakama kwa Bunge, bali ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baddhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo la jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.

2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.

4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.

5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.

6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.

7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.

Nawatakia Ijumaa Njema.

Paskali
pascomayalla@gmail.com
Rejea.
Rev. Mtikila ashida kesi ya kuruhusu mgombea binafsi mahakama ya ...
Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa ...
Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini? | Page 9 | JamiiForums ...

Hukumu ya mgombea binafsi hii hapa (AG vs Mtikila)
 
Mkuu Pascal, umeongea kitu ambacho mimi naona ni tatizo kubwa sana Tanzania, kufikia mahali nimsema sana kwamba tatizo tulilo Tanzania na nchi masikini ni kuwa na watu wenye akili ndogo kama viongozi, eidha kwa kuteuliwa au kuchaguliwa kwa kura.

Frankly speaking, msimamo unaouweka wazi hapa mie naona kama ni political illiteracy, kwamba tuko tayari hata kumuunga mkono mwendawazimu ambae hataweza kuisaidia Tanzania katika maendeleo yetu, ili mradi tu ni mwanachama wa chama tunachoshabikia?

Hii ni partisanship of the stupidest order, ambayo mimi naona kama tunakuwa hivyo basi hatuna akili sawasawa na tunapaswa kuhurumiwa sana. Ni lazima watu tuelewe kwamba Tanzania is so much bigger than our Mickey Mouse political parties ili tuweze kuendelea, la sivyo tuondoe mfumo wa vyama vingi maana unakuwa counter productive, hautimizi objectives za kuuanzisha. What Nyerere had in mind aliposema tuanzishe mfumo wa vyama vingi sichi hiki kinachoendelea Tanzania.

Ni lini tutawachagua watu kutokana na sifa zao za kuwa voingozi badala ya kuwachagua kwa kuwa wako kwenye chama tunachoshabikia, no matter kiwe kinafanya upumbavu gani?

Ni lini tutaona maoni mazuri juu ya nchi yetu ni mazuri regardless yanatolewa na mtu wa chama tunachoshabikia au la?

NI lini upumbavu kwetu utakuwa ni upumbavu hata kama unafanywa na chama cha siasa tunachoshabikia?

Ni lini tutaacha kumshabikia na kumtetea Lowasa kwa kuwa yuko chama chetu, kumtukana kwa kuwa kahamia upinzani, na kumshabikia kwa kuwa karudi chama chetu? Huu ni unafiki ambao mtu yeyote mwenye akili ataelewa.

Ideallly, ningependa kuona Magufuli na Lissu wote wakiwa viongozi wa serikali ya Tanzania, kwa kuwa wao kuwa katika vyama tofauti ni missed opportunities kwa maendeleo ya nchi yetu. Ndio maana nakuambia it is better tuondoe mfumo wa vyama vingi. Watanzania we are just too immature, politically illiterate kuwa na siasa za vyama vingi. Hata nikiwa mbele ya Magufuli nitamwambia hata yeyey yuko too immature kuwa raisi katika mfumo wa vyama vingi. Hata Ndugai, Tulia, Kabudi nk. Majaliwa ana nafuu. Sijui Lissu, I may not be able kum-judge kwa sasa.
Karibu, soma point no. 6 kwenye mapendekezo yangu.
P
 
Karibu, soma point no. 6 kwenye mapendekezo yangu.
P
MKuu Pascal, sijui kama point namba sita ndio inaoongelea yafuatao;

6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.

Sasa huu ndio ulevi, uendawazimu na upumbavu niliokuwa nausema, na baya hata zaidi ni wananchi wa Tanzania kuukubali, kuukumbatia na kuushangilia. Ndio maana nikasema ni watu walio politically illiterate tu wanaweza kufanya hivyo, na tupende tusipende, Watanzania zaidi ya 70% ni politicall illiterates!

Chama chako cha siasa kikiamua kuweka mgombea asiyefaa kuwa kiongozi na wewe ukaliona hilo, na bado ukaamua kumuunga mkono mgombea wa chama chako kwa kuwa tu unataka kuunga mkono chama chako, basi wewe unakuwa mpumbavu kuliko hata hao wapumbavu waliokuwekea mgombea asiyefaa. Hao waliokuwekea mgombea asiyefaa wanaweza kuwa walifanya upumbavu katika ujinga wao, na hilo jamii inaweza kulisamehe, lakini wewe utakuwa unafanya upumbavu katika uelewevu wako. Jamii hatuwezi kulisamehe hilo.

Na zaidi ya hapo, kuna hii point;

Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au wa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria

Siwezi kupingana na mambo yaliyo kwenye Katiba, la labda pale ninapoona mambo yalio kwenye katiba hayafai, basi option niliyonayo ni kuapigia kelele yabadilishwe.

Hata hivyo, kipengele hicho cha katika hakitoi maana kwamba kwa kuwa kila mtu anayo haki a kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, haina maana kila mtu anao uwezo wa kuwa mtawala wa nchi. Lazima uelewe hiyo tofauti, na point yangu ni kwamba Watanzania wengi katika political iliiteracy yao hawaelewi tofauti ya kuwa na haki ya kufanya jambo fulani, na kuwa na uwezo wa kufanya jambo hilo.

Sasa haki ya kushiriki inapatikana kupitia kugombea nafasi za utawala (au kuteuliwa), na kuwa qualified kwamba unaweza kushiriki kuwa mtawala kunafanywa na wananchi. NI sawa na kusema kila mtu ana haki ya kuendesha gari, lakini si kila mtu ana uwezo wa kuendesha gari. Sasa huwezi kuruhusu kila mtu aendeshe gari barabarani kwa kuwa ni haki yao. Kuna process a ku-qualify madereva ambao inafanywa na trafiki. Sasa vipi kama tuna trafiki walevi tu, wasio na uwezo wa ku-qualify madereva, nini kitatokea barabarani?

Sasa hao trafiki ndio sawa na raia wetu ambao wana qualify au kupitisha wale walio na haki ya kushiriki katika shughuli za utawala. Tatizo ni kwamba ni walevi tu na political illiterates ambao wanapitisha madereva wasio na uwezo wa kuendesha gari barabarani japo wana haki ya kimsingi kufana hivyo. Matokeo ni kwamba katika barabara zetu kunakuwa na vurugu tupu
 
Wanabodi,

Shurti la Mgombea Uongozi wa Umma, Kudhaminiwa na Chama cha Siasa ni Sheria Mbovu, ni...
Kinyume cha Katiba,
Kinyume cha Universal Declaration of Human Rights
Kinyume cha The United Nations Human Rights Committee,
Kinyume cha African Chatter of People and Political Rights
Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.

Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

Paskali
Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili anapotoa maoni yake ambayo ni ya ukweli mtupu, kisha makada wa chama chake wakamshukia, kwa maoni hayo kwenda kinyume cha Mkuu wa mhimili mwingine, kilichomfanya Mkuu huyu wa mhimili kuomba radhi, sio kwasababu anajuta, ajute kwa lipi wakati hoja zake ni hoja za ukweli mtupu. Kilichomnyenyekeza Mkuu wa mhimili mmoja kumuomba radhi Mkuu wa mhimili mwingine ni kipengele hiki nilichokitaja humu. Mkuu wa mhimili ameogopa kumwaga unga.
Kiukweli kitendo cha Mkuu wa mhimili ambaye huwa na sauti authoritative na makeke, kuwa mdogo kama piriton na kuomba msamaha, kimemdogosha sana na kuudhalilisha mhimili.

Strong leaders ni yule anayesimama with what s/he is believe in, kwa upande wa Mkuu wa mhimili, leo kusema hivi halafu kesho kuomba msamaha ni kuudhalilisha mhimili, jee mtu kama huyu anatufaa au hatufai?. Jee apishe au aendelee?.
P
 
Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili anapotoa maoni yake ambayo ni ya ukweli mtupu, kisha makada wa chama chake wakamshukia, kwa maoni hayo kwenda kinyume cha Mkuu wa mhimili mwingine, kilichomfanya Mkuu huyu wa mhimili kuomba radhi, sio kwasababu anajuta, ajute kwa lipi wakati hoja zake ni hoja za ukweli mtupu. Kilichomnyenyekeza Mkuu wa mhimili mmoja kumuomba radhi Mkuu wa mhimili mwingine ni kipengele hiki nilichokitaja humu. Mkuu wa mhimili ameogopa kumwaga unga.
Kiukweli kitendo cha Mkuu wa mhimili ambaye huwa na sauti authoritative na makeke, kuwa mdogo kama piriton na kuomba msamaha, kimemdogosha sana na kuudhalilisha mhimili.

Strong leaders ni yule anayesimama with what s/he is believe in, kwa upande wa Mkuu wa mhimili, leo kusema hivi halafu kesho kuomba msamaha ni kuudhalilisha mhimili, jee mtu kama huyu anatufaa au hatufai?. Jee apishe au aendelee?.
P

Kilichosikitisha zaidi ni kusingizia wengine kuwa ndio wanaotaka kumfarakanisha. Au hawakumuelewa!!

Anaomba msamaha but he owns not his actions or words. There was not misunderstanding on listeners’ part, neither misrepresentation on his!! Anabaki kuwa dhaifu. Angekuwa imara angepima madhara na faida za yeye kuzungumzia mambo na namna alivoyazungumzia.

Kusema “ ….taifa litapigwa mnada…..” haliwezi kueleweka tofauti na kuuzwa kwa watu tutaja bei huku wakitafuta best offer!!
 
Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili anapotoa maoni yake ambayo ni ya ukweli mtupu, kisha makada wa chama chake wakamshukia, kwa maoni hayo kwenda kinyume cha Mkuu wa mhimili mwingine, kilichomfanya Mkuu huyu wa mhimili kuomba radhi, sio kwasababu anajuta, ajute kwa lipi wakati hoja zake ni hoja za ukweli mtupu. Kilichomnyenyekeza Mkuu wa mhimili mmoja kumuomba radhi Mkuu wa mhimili mwingine ni kipengele hiki nilichokitaja humu. Mkuu wa mhimili ameogopa kumwaga unga.
Kiukweli kitendo cha Mkuu wa mhimili ambaye huwa na sauti authoritative na makeke, kuwa mdogo kama piriton na kuomba msamaha, kimemdogosha sana na kuudhalilisha mhimili.

Strong leaders ni yule anayesimama with what s/he is believe in, kwa upande wa Mkuu wa mhimili, leo kusema hivi halafu kesho kuomba msamaha ni kuudhalilisha mhimili, jee mtu kama huyu anatufaa au hatufai?. Jee apishe au aendelee?.
P
Mkuu hivi kwa hapo alipofikia Unga ukimwagika atashindwa kweli kuishi tukizingatia alizozichanga since time immemorial??
 
Wanabodi,

Shurti la Mgombea Uongozi wa Umma, Kudhaminiwa na Chama cha Siasa ni Sheria Mbovu, ni...
Kinyume cha Katiba,
Kinyume cha Universal Declaration of Human Rights
Kinyume cha The United Nations Human Rights Committee,
Kinyume cha African Chatter of People and Political Rights
Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.

Declaration of Interest
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wazalendo wa nchi yangu, ambaye ni mwanachama wa chama cha siasa, kwa sababu ni lazima uwe mwanachama ndipo ushiriki siasa za vyama za vingi Tanzania, zinaendeshwa na Tume ama sio huru, na kama ni huru, sio shirikishi. Siasa zetu hazichezwi katika uwanja ulio sawa, zinachezwa katika uwanja tenge, wa kugombea kisu cha makali kuwili, huku mmoja ameshika mpini!. Hivyo ushindi katika chaguzi zetu, hupatikana kwa mbinu zaidi kuliko kwa kura, ninaziita ni siasa za demokrasia changa, au demokrasia ya Kiafrika, African Democracy. Hivyo kwenye mada hii, haya ni mawazo yangu, kila mtu anao uhuru wa mawazo yake, ambao unapaswa kuheshimiwa hata kama hukubaliani nayo. Kwa wale ambao hawakubaliani na mawazo yangu, rukhsa tutofautiane kwa hoja, kwa kupangua hoja zangu na kuleta hoja mbadala.

Watanzania Tufanye Siasa za Ukweli, Tuachane na Siasa za Uongo, Ulaghai na Siasa za Hovyo Hovyo!.
Tufike mahali sisi Watanzania, wazalendo, wenye nia njema na maendeleo ya kweli ya taifai letu hili masikini, tuwe wakweli kwa kuusema ukweli wa siasa zetu sio siasa za ukweli, ni siasa za hadaa, ulaghai na siasa za hovyo hovyo. Hatuwezi kukaa kimya kwa kuendelea kukumbatia Tume ya Uchaguzi isiyo tume huru kwa kutokuwa shirikishi, huku tukiendesha uchaguzi wetu kwa kutumia sheria mbovu za uchaguzi, na kuendelea kuwawabesha masikini wa Tanzania, mzigo mkubwa wa gharama za uchaguzi wa marudio, unaosababishwa kwa sababu za kujitakia, ambazo mimi nimeziita ni sababu za kijinga, zinazotokana na siasa za hovyo hovyo!.

Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo mkubwa wa gharama za kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kijinga na kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!.

Kwa Nini Sheria Yetu ya Uchaguzi ni Sheria Mbovu, Bad Law.
Kifungu 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.

Sheria hiyo inasema hivi na hapa ninanukuu

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Lakini kukatokea kikundi fulani cha watu, kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona karibu vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho katiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii, hivyo baada ya mabadiliko hayo ya mlango wa nyuma, kipengele hicho sasa kinasomeka hivi

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.


Ule uhuru uliotolewa na Katiba wa kila mtu kuwa huru kushiriki shughuli za uongozi, kupitia ibara ya 21, umekuja kunyofolewa na ibara ya 39 na 67 (b)(c) kwa kuweka sherti, ili mtu kuweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma, ni lazima awe ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa hivyo lazima adhaminiwe na chama cha siasa!, Haki zinatolewa na ibara moja halafu zinaporwa na ibara nyingine ya katiba hiyo hiyo!.

Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi

Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.

Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au wa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria”.

Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”

Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.

Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.

Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu

(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.

(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.

Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali mambo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)

Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or not such [independent] candidates are suitable. We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the people. That is the property of elected Members of Parliament”.

Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.

Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.

“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction. The decision on whether or not to introduce independent candidates depends on the social needs of each State based on its historical reality. Thus the issue of independent candidates is political and not legal However, we give a word of advice to both the Attorney General and our Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25 of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21: The right of persons to stand for election should not be limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties. Tanzania is known for our good record on human rights and particularly our militancy for the right to self determination and hence our involvement in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a Committee of the United Nations, that is, the whole world.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”


Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, uamuzi huu sio utii wa mhimili wa Mahakama kwa mhimili Bunge, bali huu ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.

Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baadhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.

Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.

Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.

Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.

Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.

1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.

2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.

3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.

4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.

5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.

6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.

7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.

8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.

9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.

10. Tuibadili Tume yetu ya Uchaguzi iwe Tume Huru zaidi na Shirikishi, tujenge uwanja sawa wa ushindani wa haki kwa vyama vyote, uchaguzi uendeshwe kwa transparency ya hali ya juu kwa kuruhusu mawakala hadi kwenye tallying, na vyama au taasisi zozote ziwe free kuwa na tallying centers zake, kitu ambacho hakitaruhusiwa na talling centers hizo ni kutangaza matokeo, kama matokeo yote ya uchaguzi hadi wa rais yanahesabiwa kituoni na kubandikwa ukutani, kama hakuna jambo lolote la kificho, yaani nothing to hide, kwanini uzuie independent tallying?!. Uchaguzi wa 2020, kila mwenye uwezo wa kufanya tallying aruhusiwe afanye ila sitangaze matokeo, hii itazuia bao la mkono!

Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.

Nawatakia Ijumaa Njema.

Paskali
pascomayalla@gmail.com
Rejea.
Rev. Mtikila ashida kesi ya kuruhusu mgombea binafsi mahakama ya ...
Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa ...
Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini? | Page 9 | JamiiForums ...

Hukumu ya mgombea binafsi hii hapa (AG vs Mtikila)
Enzi hizo kabla ya njaa
 
Bunge ni mhimili, Mkuu wa mhimili anapotoa maoni yake ambayo ni ya ukweli mtupu, kisha makada wa chama chake wakamshukia, kwa maoni hayo kwenda kinyume cha Mkuu wa mhimili mwingine, kilichomfanya Mkuu huyu wa mhimili kuomba radhi, sio kwasababu anajuta, ajute kwa lipi wakati hoja zake ni hoja za ukweli mtupu. Kilichomnyenyekeza Mkuu wa mhimili mmoja kumuomba radhi Mkuu wa mhimili mwingine ni kipengele hiki nilichokitaja humu. Mkuu wa mhimili ameogopa kumwaga unga.
Kiukweli kitendo cha Mkuu wa mhimili ambaye huwa na sauti authoritative na makeke, kuwa mdogo kama piriton na kuomba msamaha, kimemdogosha sana na kuudhalilisha mhimili.

Strong leaders ni yule anayesimama with what s/he is believe in, kwa upande wa Mkuu wa mhimili, leo kusema hivi halafu kesho kuomba msamaha ni kuudhalilisha mhimili, jee mtu kama huyu anatufaa au hatufai?. Jee apishe au aendelee?.
P
Wewe pasco unaamini ni mwanaccm au ni njaa ilikupeka ukapata aibu,

We myewe hapa juzi Kati umeyumba sana

Ukayakana maandiko Yako uliiyo yaandika humu, tukabaki tunakushangaa,

We na job hamna tofauti
 
Back
Top Bottom