Kibanga Ampiga Mkoloni
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 19,020
- 9,177
Mtikila alishinda kesi,
kabla Bunge alijatekeleza likaenda kukazia sheria.
Umesahahu?
kabla Bunge alijatekeleza likaenda kukazia sheria.
Umesahahu?
Makala nyingine ndeeefu, hv Paschal huwezi kufanya summary na ukaeleweka!! Hoja zako nyingi zimejurudia rudia bila sababu. Nirudi kwenye mada yako, kweli kama ulivyosema umeandika mawazo yako lkn mimi nayapinga mawazo yako na nayaona dhaifu sana. Kwanza unapaswa ujue kuwa kila mchezo una sheria na kanuni zake. Mfano kwenye mpira wa miguu, mpira ukitoka ubavuni mwa uwanja utarushwa kwa mikono japo mpira wenyewe ni wa miguu na kipa anaruhusiwa kutumia mikono yake kudaka mpira eneo maalumu. Sasa hata siasa zina sheria zake, mbunge, diwani au kiongozi yeyote wa kuchaguliwa ana haki na hiari ya kujiunga na chama chochote cha siasa na pia ana haki ya kuondoka kwenye chama alichopo. Katiba inaruhusu hali hiyo ambayo hata Nyalandu na Lowasa waliitumia. Kusema sheria ya uchaguzi inapingana na katiba na wakati huo huo unasema kipengele cha katiba kilibadilishwa ili kulazimisha uwakilishi utokane na chama, inapnesha ni namna gani unaandika kwa hisia badala ya ukweli ulivyo. Kumbe kipengele kilibadilishwa kisheria kuzuia mgombea huru sasa hoja zako zote ulizoandika zinaonekana za kipuuzi. Unaposema kikundi cha watu wachache kiliamua kutunga sheria hiyo una maana gani? Kwangu mm kikundi cha watu ni CCM, lkn CCM si ndio yenye ridhaa ya wananchi na ndio maana nakuambia rule of the game ktk siasa ni kupata ushindi mkubwa hasa wa wabunge ili kuweza kufanya maamuzi. Na mnapo taka kufanya hivyo, ni lazima mwombe ridhaa hiyo kwa wananchi na hivyo mkipata ridhaa mnatekeleza. Unaposema chaguzi za marudio zinaigharimu nchi na wananchi, nikuulize umethamisha marudio ya uchaguzi in terms of money, je, unaweza kutupa gharama za kutokuwa na uwakilishi? Maana inavyo elekea unalalamika viongozi kuhamia CCM na sio kuacha nafasi zao ingewezekana hata wangeamua kujiondoa kwenye chama, napo ungeitishwa uchaguzi. Kwa hiyo ndugu Paschal, uamuzi wa kuhama chama ni haki ya kikatiba na kuomba uongozi wa kisiasa kupitia chama cha siasa ni haki ya kikatiba iliyotolewa ufafanuzi kisheria na Mahakama ilizingatia hilo na wako sahihi kabisa. Kabla ya sheria hiyo, haki ya mgombea huru ilikiukwa nakubali lkn baada ya marekebisho, hakuna ukiukwaji tena wa katiba. Kwa hiyo ndugu Paschal, maandiko yako yanajengwa na hisia na chuki dhidi ya CCM ambayo yanakutoa kwenye weledi wa kudadavua mambo.
Nimeyaelewa mengi, lakini kaka Pascal Mayala nimekufahamu toka enzi zile upo pale mbezi beach kwenye nyumba yako na Honda lako kubwa...hahaha ila sasa kusema hapa kuwa wewe ni mtanzania mzalendo na hauna chama chochote mh yani kikutokacho mdomoni tofauti na fikra, falsafa na maandiko yako mimi hata nikiamshwa usingizini nikiulizwa Pascal Mayala ana mlengo wa chama gani? NITAJIBU KWA KUJIAMINI your not NEUTRAL.Wanabodi,
Shurti la Kudhaminiwa na Chama ni Sheria Mbovu, Inakiuka Katiba, Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.
Declaration of Interest
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wazalendo wa nchi yangu, ambaye sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa sababu siasa za vyama za vingi Tanzania, hazichezwi katika uwanja ulio sawa, hivyo ushindi hupatikana kwa mbinu Zaidi kuliko kwa kura, ninaziita ni siasa za demokrasia change, hivyo kwenye mada hii, haya ni mawazo yangu, kila mtu anao uhuru wa mawazo yake, ambao unapaswa kuheshimiwa hata kama hukubaliani na mawazo hayo. Kwa wale ambao hawakubaliani na mawazo yangu, tutofautiane kwa hoja, kwa kupangua hoja zangu na kuleta hoja mbadala.
Watanzania Tufanye Siasa za Ukweli, Tuachane na Siasa za Hovyo Hovyo.
Tufike mahali sisi Watanzania, wazalendo, wenye nia njema na maendeleo ya kweli ya taifai letu hili masikini, hatuwezi kukaa kimya kwa kuendelea kukumbatia sheria mbovu, za uchaguzi, na kuendelea kuwawabesha masikini wa Tanzania, mzigo wa gharama za uchaguzi wa marudio, ulnaosababishwa na kwa sababu za kijtakia, zinazotokana na siasa za hovyo hovyo.
Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo wa kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!.
Kwa Nini Sheria Yetu ya Uchaguzi ni Sheria Mbovu, Bad Law.
Kifungu 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Sheria hiyo inasema hivi na hapa ninanukuu
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Lakini kukatokea kikundi fulani cha watu, kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho kaiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii.
Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993 Rev. Mtikila alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea uongozi
Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.
Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au
kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa
hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au
kwa mujibu wa sheri”.
Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya
Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya
kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”
Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.
Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.
Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu
(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sheria
No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.
(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.
Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali maombo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.
Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Pemoni)
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or
not such [independent] candidates are suitable.
We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the
people. That is the property of elected Members of Parliament”.
Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.
Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.
“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be
settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution
and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction.
The decision on whether or not to introduce independent candidates
depends on the social needs of each State based on its historical reality.
Thus the issue of independent candidates is political and not legal
However, we give a word of advice to both the Attorney General and our
Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of
its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25
of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly
worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21:
The right of persons to stand for election should not be
limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties.
Tanzania is known for our good record on human rights and particularly
our militancy for the right to self determination and hence our involvement
in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a
Committee of the United Nations, that is, the whole world.
Each party is to bear its own costs both in this Court and below.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”
Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, Kiukweli kabisa, uamuzi huu sio utii wa Mhimili wa Mahakama kwa Bunge, bali ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.
Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baddhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo la jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.
Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.
Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.
Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.
Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.
2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.
3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.
4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.
5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.
6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.
7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.
8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.
9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.
Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.
Nawatakia Ijumaa Njema.
Paskali
Rejea.
Rev. Mtikila ashida kesi ya kuruhusu mgombea binafsi mahakama ya ...
Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa ...
Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini? | Page 9 | JamiiForums ...
Swali kwa Wana UKAWA: Is UKAWA for Real or Just A Marriage of ...
Pascal Mayalla
Media Consultant
PPR Media
Posta House, Ohio Street
4 Floor, Room No. 403
Mob. +255 784 270403
umesahau moja mkuu domokaya .....
.....kama mbunge anajihudhuru kwa kumuunga mkono kiongozi na unaitishwa uchaguzi anagombea tena!
CCM ilishakufa kitambo kilichobaki ni polisi na tumeHili la kutoruhusu mgombea binafsi linawanufaisha sana CCM na ni moja ya nguzo yao kuu. Ukiruhusu hilo chama kitakufa kesho yake asubuhi.
Nasema walaaniwe majaji waliopitisha maamuzi kwa manufaa yao bila kuangalia maslahi ya taifa huku wakijua ni kinyume cha sheria za kimataifa.
Ila mkuu hongera kwa uzi ulioandika kitaalamu sana.
Hili la kutoruhusu mgombea binafsi linawanufaisha sana CCM na ni moja ya nguzo yao kuu. Ukiruhusu hilo chama kitakufa kesho yake asubuhi.
Nasema walaaniwe majaji waliopitisha maamuzi kwa manufaa yao bila kuangalia maslahi ya taifa huku wakijua ni kinyume cha sheria za kimataifa.
Ila mkuu hongera kwa uzi ulioandika kitaalamu sana.
hivi ndiyo vitu vya msingi kabisa ambavyo wanajamvi tunapashwa kuvijadili kila iitwapo leo kwani kwa kurudia uchaguzi sio tu wana siha na kinondoni wanaolipa hizi gharama.Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo wa kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!
hivi ndiyo vitu vya msingi kabisa ambavyo wanajamvi tunapashwa kuvijadili kila iitwapo leo kwani kwa kurudia uchaguzi sio tu wana siha na kinondoni wanaolipa hizi gharama.
kuna sehemu mpaka leo watanzania hawana maji
kuna sehemu mpaka leo watanzania hawana shule
kuna sehemu mpaka leo watanzania hawana hospital
kuna sehemu mpaka leo watanzania hawana barabara
Hujaona kifungu kilichonukuliwa hapo juu? Au hukuelewa?Sheria za kimataifa? Tuone haya kuyazungumzia tusiyoyafahamu. Kujifanya tunajua ndiko kunakotufanya tuwe hivi.
Kama una internet si usome ujiridhishe na upate ufahamu?
Tusilaumu watu wengine, tuko katika hali hii kwa kuwa sisi ndivyo tulivyo!
Akili yako haina tofauti na ya Prof Bana aliesema, katiba mpya haina maana wala sio tiba ya matatizo yetu kwani watawala wanaweza kuivunja wala hatuna la kuwafanya! Nilimsamehe bure kwani najua alikuwa amepanda kuwa profesa hivi majuzi kwa hisani ya CCM.Makala nyingine ndeeefu, hv Paschal huwezi kufanya summary na ukaeleweka!! Hoja zako nyingi zimejurudia rudia bila sababu. Nirudi kwenye mada yako, kweli kama ulivyosema umeandika mawazo yako lkn mimi nayapinga mawazo yako na nayaona dhaifu sana. Kwanza unapaswa ujue kuwa kila mchezo una sheria na kanuni zake. Mfano kwenye mpira wa miguu, mpira ukitoka ubavuni mwa uwanja utarushwa kwa mikono japo mpira wenyewe ni wa miguu na kipa anaruhusiwa kutumia mikono yake kudaka mpira eneo maalumu. Sasa hata siasa zina sheria zake, mbunge, diwani au kiongozi yeyote wa kuchaguliwa ana haki na hiari ya kujiunga na chama chochote cha siasa na pia ana haki ya kuondoka kwenye chama alichopo. Katiba inaruhusu hali hiyo ambayo hata Nyalandu na Lowasa waliitumia. Kusema sheria ya uchaguzi inapingana na katiba na wakati huo huo unasema kipengele cha katiba kilibadilishwa ili kulazimisha uwakilishi utokane na chama, inapnesha ni namna gani unaandika kwa hisia badala ya ukweli ulivyo. Kumbe kipengele kilibadilishwa kisheria kuzuia mgombea huru sasa hoja zako zote ulizoandika zinaonekana za kipuuzi. Unaposema kikundi cha watu wachache kiliamua kutunga sheria hiyo una maana gani? Kwangu mm kikundi cha watu ni CCM, lkn CCM si ndio yenye ridhaa ya wananchi na ndio maana nakuambia rule of the game ktk siasa ni kupata ushindi mkubwa hasa wa wabunge ili kuweza kufanya maamuzi. Na mnapo taka kufanya hivyo, ni lazima mwombe ridhaa hiyo kwa wananchi na hivyo mkipata ridhaa mnatekeleza. Unaposema chaguzi za marudio zinaigharimu nchi na wananchi, nikuulize umethamisha marudio ya uchaguzi in terms of money, je, unaweza kutupa gharama za kutokuwa na uwakilishi? Maana inavyo elekea unalalamika viongozi kuhamia CCM na sio kuacha nafasi zao ingewezekana hata wangeamua kujiondoa kwenye chama, napo ungeitishwa uchaguzi. Kwa hiyo ndugu Paschal, uamuzi wa kuhama chama ni haki ya kikatiba na kuomba uongozi wa kisiasa kupitia chama cha siasa ni haki ya kikatiba iliyotolewa ufafanuzi kisheria na Mahakama ilizingatia hilo na wako sahihi kabisa. Kabla ya sheria hiyo, haki ya mgombea huru ilikiukwa nakubali lkn baada ya marekebisho, hakuna ukiukwaji tena wa katiba. Kwa hiyo ndugu Paschal, maandiko yako yanajengwa na hisia na chuki dhidi ya CCM ambayo yanakutoa kwenye weledi wa kudadavua mambo.
Mahakama ya Afrika Mashariki ilitengua uamuzi wa mahakama ya rufaa na serikali iliahidi kurekebisha katiba kabla ya uchaguzi 2015 na baadae wakasema wataliweka kwenye katiba mpya.Hili la kutoruhusu mgombea binafsi linawanufaisha sana CCM na ni moja ya nguzo yao kuu. Ukiruhusu hilo chama kitakufa kesho yake asubuhi.
Nasema walaaniwe majaji waliopitisha maamuzi kwa manufaa yao bila kuangalia maslahi ya taifa huku wakijua ni kinyume cha sheria za kimataifa.
Ila mkuu hongera kwa uzi ulioandika kitaalamu sana.
paschalWanabodi,
Shurti la Kudhaminiwa na Chama ni Sheria Mbovu, Inakiuka Katiba, Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.
Declaration of Interest
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wazalendo wa nchi yangu, ambaye sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa sababu siasa za vyama za vingi Tanzania, hazichezwi katika uwanja ulio sawa, hivyo ushindi hupatikana kwa mbinu Zaidi kuliko kwa kura, ninaziita ni siasa za demokrasia change, hivyo kwenye mada hii, haya ni mawazo yangu, kila mtu anao uhuru wa mawazo yake, ambao unapaswa kuheshimiwa hata kama hukubaliani na mawazo hayo. Kwa wale ambao hawakubaliani na mawazo yangu, tutofautiane kwa hoja, kwa kupangua hoja zangu na kuleta hoja mbadala.
Watanzania Tufanye Siasa za Ukweli, Tuachane na Siasa za Hovyo Hovyo.
Tufike mahali sisi Watanzania, wazalendo, wenye nia njema na maendeleo ya kweli ya taifai letu hili masikini, hatuwezi kukaa kimya kwa kuendelea kukumbatia sheria mbovu, za uchaguzi, na kuendelea kuwawabesha masikini wa Tanzania, mzigo wa gharama za uchaguzi wa marudio, ulnaosababishwa na kwa sababu za kijtakia, zinazotokana na siasa za hovyo hovyo.
Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo wa kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!.
Kwa Nini Sheria Yetu ya Uchaguzi ni Sheria Mbovu, Bad Law.
Kifungu 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Sheria hiyo inasema hivi na hapa ninanukuu
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Lakini kukatokea kikundi fulani cha watu, kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho kaiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii.
Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993 Rev. Mtikila alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi
Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.
Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au
kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa
hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au
kwa mujibu wa sheri”.
Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya
Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya
kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”
Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.
Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.
Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu
(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.
(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.
Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali maombo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or
not such [independent] candidates are suitable.
We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the
people. That is the property of elected Members of Parliament”.
Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.
Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.
“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be
settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution
and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction.
The decision on whether or not to introduce independent candidates
depends on the social needs of each State based on its historical reality.
Thus the issue of independent candidates is political and not legal
However, we give a word of advice to both the Attorney General and our
Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of
its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25
of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly
worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21:
The right of persons to stand for election should not be
limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties.
Tanzania is known for our good record on human rights and particularly
our militancy for the right to self determination and hence our involvement
in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a
Committee of the United Nations, that is, the whole world.
Each party is to bear its own costs both in this Court and below.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”
Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, Kiukweli kabisa, uamuzi huu sio utii wa Mhimili wa Mahakama kwa Bunge, bali ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.
Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baddhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo la jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.
Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.
Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.
Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.
Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.
2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.
3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.
4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.
5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.
6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.
7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.
8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.
9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.
Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.
Nawatakia Ijumaa Njema.
Paskali
Rejea.
Rev. Mtikila ashida kesi ya kuruhusu mgombea binafsi mahakama ya ...
Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa ...
Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini? | Page 9 | JamiiForums ...
Swali kwa Wana UKAWA: Is UKAWA for Real or Just A Marriage of ...
Pascal Mayalla
pascomayalla@gmail.com
Wanabodi,
Shurti la Kudhaminiwa na Chama ni Sheria Mbovu, Inakiuka Katiba, Inaminya Haki na Kulitia Hasara Taifa, Ibadilishwe!.
Declaration of Interest
Mimi ni miongoni mwa Watanzania wazalendo wa nchi yangu, ambaye sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa sababu siasa za vyama za vingi Tanzania, hazichezwi katika uwanja ulio sawa, hivyo ushindi hupatikana kwa mbinu Zaidi kuliko kwa kura, ninaziita ni siasa za demokrasia change, hivyo kwenye mada hii, haya ni mawazo yangu, kila mtu anao uhuru wa mawazo yake, ambao unapaswa kuheshimiwa hata kama hukubaliani na mawazo hayo. Kwa wale ambao hawakubaliani na mawazo yangu, tutofautiane kwa hoja, kwa kupangua hoja zangu na kuleta hoja mbadala.
Watanzania Tufanye Siasa za Ukweli, Tuachane na Siasa za Hovyo Hovyo.
Tufike mahali sisi Watanzania, wazalendo, wenye nia njema na maendeleo ya kweli ya taifai letu hili masikini, hatuwezi kukaa kimya kwa kuendelea kukumbatia sheria mbovu, za uchaguzi, na kuendelea kuwawabesha masikini wa Tanzania, mzigo wa gharama za uchaguzi wa marudio, ulnaosababishwa na kwa sababu za kijtakia, zinazotokana na siasa za hovyo hovyo.
Kitendo hiki cha wananchi masikini wa kutupwa wa Tanzania, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea wa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, halafu kuja kubebeshwa mzigo wa kugharimia chaguzi za marudio zinazotokana na sababu za kisiasa za kujitakia ikiwemo wawakilishi halali wa wananchi, waliochaguliwa na wananchi wa eneo husika, kupoteza uwakilishi halali wa wananchi kwa sababu tuu ya kuhama vyama, halafu kuwagharimisha wananchi wote wa taifa hili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio wa kujitakia, sio kuwatendea haki masikini hawa wa nchi hii. Kuwalipisha masikini gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kujitakia, ni kuwatendea dhambi masikini hawa!.
Kwa Nini Sheria Yetu ya Uchaguzi ni Sheria Mbovu, Bad Law.
Kifungu 21 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinatoa haki ya kila Mtanzania mwenye sifa, kuwa huru kushiriki katika siasa na uongozi kuanzia serikali za mtaa hadi serikali kuu, bila ubaguzi wowote.
Sheria hiyo inasema hivi na hapa ninanukuu
Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4
21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Lakini kukatokea kikundi fulani cha watu, kwa maslahi yao, na kwa vile serikali ni yao, wakaipindua katiba kwa kuinyofoa haki hiyo ya kila mtu kushiriki siasa, iliyotolewa na katiba, na kupachika shurti la kudhaminiwa na chama, hivyo kujenga ubaguzi katika kushiriki shughuli za uongozi umma kwa watu kulazimishwa kwanza kujiunga na vyama vya siasa, ndipo upate haki ya kugombee nafasi yoyote ya uongozi wa umma, huku sio kuwatendea haki Watanzania wengine wote, wasiotaka kujiunga na vyama vyovyote vya siasa, kutokana na kuviona vyama vyote ni vyama vya hovyo hovyo, lakini wana uwezo wa uongozi. Hii ni haki muhimu iliyotolewa na katiba, kitendo cha kuingiza shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa ni kinyume cha katiba. Hivyo sheria hii ibadilishwe ili kukidhi kile ambacho kaiba ilidhamiria ilipoitoa haki hii.
Mchungaji Mtikila (Mungu amuweke mahala pema peponi), mwaka 1993 Rev. Mtikila alifungua kesi No. 5 ya 1993, alifanya kuhudi kubwa kukipinga kifungu hiki na Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi
Baada tuu ya Mtikila kushinda kesi serikali ikafanya mambo mawili makubwa ya ajabu!, kwanza ilikata rufaa!. Hivi kwa uamuzi kama huu, serikali ilikata rufaa kwa maslahi ya nani?. Pili serikali ilipeleka bungeni kwa hati ya dharura, sheria No. 34 ya mwaka 1994, kufanya marekebisho ya 8 ya Katiba ya JMT na kukichomeka kipengele hicho ndani ya katiba, hivyo kuibatilisha ile hukumu ya Jaji Lugakingira!. Hapa ndipo ujinga unapoanzia katika siasa zetu kwa serikali kufanya kazi kwa maslahi ya kisiasa ya watu fulani, hivyo kupoteza haki ya wengi kwa ajili ya kuwanufaisha wachache.
Kuhusu haki ya kila Mtanzania kugombea nafasi yoyote, ibara ya 21 ya Katiba ya Tanzania ilisema hivi na hapa nina nukuu
“Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au
kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa
hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au
kwa mujibu wa sheri”.
Lakini baada ya kufanywa marekebisho, ibara hiyo ilisomeka hivi, na hapa ninanukuu
“ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 39, ya 47 na ya 67 ya
Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya
kuchaguwa na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi”
Hiki kilichofanyika, mimi nakiita ni kitendo cha kihuni!, Watanzania tulifanyiwa uhuni na serikali yetu, kwa kuinajisi katiba yetu!, kitu kimeelezwa ni kinyume cha katiba, kinatoa haki zilizotolewa na katiba, halafu serikali hiyo inakuja kuihalalisha haramu hiyo kwa kuiingiza rasmi kwenye katiba!, huku ni kuinajisi katiba yetu!.
Mchungaji Mtikila, licha ya kuwa ni mwanasiasa, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, (Democratic Party), lakini alikuwa ni mtu wa Mungu kiukweli kabisa, kwa sababu hakukubali kabila yetu inajisiwe!, hivyo akafungua kesi nyingine No. 10 ya mwaka 2009 kupinga marekebisho hayo ya 8 ya katiba na kuyaita ni ubatili!.
Katika kesi hiyo, Mchungaji Mtikila aliomba mambo mawili makuu
(a) Mahakama itamke ibara 39 na 67 za katiba zilizorekebishwa na marekebisho ya 8 kwa sharia No. 34 ya mwaka 1994, ni batili na kinyume cha katiba.
(b) Kutamka wazi kuwa Kila Mtanzania ana haki ya kugombea kwa mujibu wa ibara ya 21 ya Katiba, bila kulazimishwa kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo mtu anaweza kugombea kama mgombea binafsi.
Mahakama Kuu chini ya majaji watatu, (majaji watatu kisheria inaitwa Half Bench), Manento, Masati na Mihayo, wakayakubali maombo yote ya Mchungaji Mtikila na kumpa ushindi tena kwa kutamka marekebisho hayo ya katiba ni batili!. Lakini serikali yetu ilivyo ya ajabu, ikakata tena rufaa, na safari hii Mahakama Kuu ikakaa Full Bench ya majaji 7, chini ya Jaji Mkuu Mwenyewe, Agustino Ramadhani, akisaidiwa na Jaji Munuo, Jaji Msoffe, Jaji Kimaro, Jaji Mbarouk, Jaji Luanda, na Jaji Mjasir, ambapo tarehe 17 mwezi June, mwaka 2010 ikatoa hukumu ya ajabu kabisa kuwa kutokea Tanzania!. Tena Mahakama haikuwa peke yake, bali iliwaita mabinga wabobezi wa sheria na katiba kuisaidia, hawa ni wanaitwa marafiki wa mahakama, kwa kiingereza ni friends of the Court, kisheria wanaitwa Amicus Curiae, hivyo ma Amicus Curiae hawa, Mr. Othman Masoud, Prof. Palamagamba Kabudi, na Prof.Jwan Mwaikusa(Mungu Aiweke Roho yake Mahala Pema Peponi)
Uamuzi wa Mahakama Kuu ya Rufaa uliamua kitu cha ajabu sana na hapa naomba ninanukuu
“So as to let the will of the people prevail as to whether or
not such [independent] candidates are suitable.
We are definite that the Courts are not the custodian of the will of the
people. That is the property of elected Members of Parliament”.
Hii kiukweli ni kauli ya ajabu sana kutolewa na mahakama yetu kwenye jambo zito na muhimu kama hili!. Kitendo cha Mahakama kujivua jukumu la kuwa the custodian of the will of the people!, ni kitendo cha ajabu sana na kushangaza sana!. Hakuna will of the people kubwa kuliko katiba!, kama katiba imetoa haki Fulani, halafu Bunge likatunga sheria ya ajabu kabisa kuifuta haki hiyo, halafu mahakama ikatamka haiwezi kuliingilia Bunge!, where is the doctrine of separation of powers, checks and balance?.
Kwa ajili ya kulinda heshima ya Mahakama Kuu, naomba niweke ilichokisema bila kukitafsiri.
“In our case, we say that the issue of independent candidates has to be
settled by Parliament which has the jurisdiction to amend the Constitution
and not the Courts which, as we have found, do not have that jurisdiction.
The decision on whether or not to introduce independent candidates
depends on the social needs of each State based on its historical reality.
Thus the issue of independent candidates is political and not legal
However, we give a word of advice to both the Attorney General and our
Parliament: The United Nations Human Rights Committee, in paragraph 21 of
its General Comment No. 25, of July 12, 1996, said as follows on Article 25
of the International Covenant on Civil and Political Rights, very similarly
worded as Art 23 of the American Convention and our Art 21:
The right of persons to stand for election should not be
limited unreasonably by requiring candidates to be members of
parties or of specific parties.
Tanzania is known for our good record on human rights and particularly
our militancy for the right to self determination and hence our involvement
in the liberation struggle. We should seriously ponder that comment from a
Committee of the United Nations, that is, the whole world.
Each party is to bear its own costs both in this Court and below.
DATED at DAR ES SALAAM this 17th day of June, 2010”
Mahakama Kuu ya Rufaa ikaamua kuwa Mahakama haina mamlaka ya kuliingilia Bunge, katika vipengele vya katiba, kumaanisha kwa vile marekebisho hayo ya 8 yamefanywa na Bunge, hivyo ni Bunge ndio lirekebishe kipengele hicho!, Kiukweli kabisa, uamuzi huu sio utii wa Mhimili wa Mahakama kwa Bunge, bali ni ukondoo wa hali ya juu kwa Mhimili wa Mahakama kwa serikali kwa manufaa ya watu wachache!.
Uchaguzi wa Mwaka 2015 ukalithibitisha hili, kumbe baddhi ya majaji wetu ni makada!, Jaji Mkuu Mstaafu aliyeongoza jopo la jopo hilo, alichukua fomu kugombea urais!, for what my God?!. Baadhi ya wale ma amicus curiae naamini tunawajua na tunawaona na ukada wao!. Unategemea nini kama sheria za nchi hii zitafinyangwa finyangwa kwa manufaa ya wachache?!. This must stop!.
Japo Lengo la Kudhaminiwa na Chama ni Nini, Huu Sii Ujinga Tuu?!.
Katiba ilisema kila Mtanzania ana haki ya kushiriki uongozi, hili sherti la kudhaminiwa na chama lilitoka wapi, na kwa kwa nini watu walazimishwe kuwa wanachama wa vyama ili wadhaminiwe, ndipo waweze kugombea?. Mfano mimi, sina chama kwa sababu naziona siasa za vyama ni za hovyo hovyo, ikitokea nina uwezo wa kuwatumikia wananchi wa eneo langu na kuwaletea maendeleo bila kupitia chama chochote, kwa nini nizuiliwe?!. Kiukweli kabisa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga!, it is nonsense!.
Watanzania tusikubali ujinga huu uendelee hadi 2020!, tupiganie milango ya wagombea binafsi ifunguliwe, 2020, watu wenye nia ya kugombea, kuwaletea wananchi maendeleo, bila kupitia hizi nonsense za vyama waingie, washindane kwa hoja na sio kushindana kuhonga, kama hali inavyoendelea sasa!. Hili shurti la vyama likiondolewa, mnaweza kushangaa watu wazalendo wa kweli wan chi hii, kama kina Reginald Mengi, Ali Mfuruki, Yogesh Manek, SS Bakhresa, Pascal Mayalla, and the like, wenye uchungu wa dhati na umasikini wa taifa hili, wakajitokeza kuwatumikia wananchi!.
Kiongozi Akiishachaguliwa, Anakuwa ni Kiongozi wa Watu, na Sio Kiongozi wa Chama, Kwa Sababu Anachaguliwa na Watu na Sio Chama!.
Kiukweli kwenye hili jambo, kuna ujinga mwingi!, ujinga mwingine mkubwa kabisa ni huu, hata kama mgombea amedhaminiwa na chama cha siasa kugombea, akiishapitishwa na Tume ya Uchaguzi kuwa Mgombea, japo anatambulika kama ni mgombea wa chama fulani, lakini akiishachaguliwa, mwenyekiti wa mtaa, diwani, mbunge au rais, anakuwa sio kiongozi tena wa chama kilichomdhamini, bali sasa anakuwa ni kiongozi wa umma, kiongozi wa wananchi. Mfano baada ya rais Magufuli kuchaguliwa kuwa rais kwa tiketi ya CCM, lakini hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote, yeye anakuwa sio kiongozi wa CCM bali kiongozi wa Watanzania wote, vivyo hivyo kwa wabunge, madiwani na viongozi wa serikali ya mtaa, kitendo cha mtu ambaye ni kiungozi wa umma, kujitoa chama na kupoteza ubunge, udiwani au uongozi wa umma, ni ujinga ambao haupaswi kuvumiliwa. Nini muhimu kati ya umma na chama?. Kuukosesha umma kiongozi wao waliemchagua kwa sababu za chama, sio tuu sio haki kwa wananchi waliomchagua, bali pia ni dhambi, kuwalipisha masikini hawa gharama za uchaguzi wa marudio kwa sababu za kijinga!.
Nini Kifanyike, A Way Forward.
Kama nilivyowahi kushauri humu, ukosoaji wenye kujenga, huandamana na ushauri wa nini kifanyike kurekebisha kasoro hizi ili kuundoa ujinga huu unaoendelea nchini mwetu kwa sasa kwa viongozi wa umma kuhama vyama na kupoteza uongozi wa umma.
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dr. John Pombe Magufuli, akemee huu mtindo wa kuhama vyama unasababisha hasara kwa taifa, kwa kuwashukuru kumuunga mkono na kuunga mkono juhudi zake, lakini wabaki huko huko kwenye vyama vyao, hadi 2020, wakiishamaliza muhula wao, ndipo wajitoe na kuhama vyama.
2. Rais wa Nchi, akili Ikulu yetu, atenganisha kofia zake mbili za rais wa nchi na Mwenyekiti wa chama cha CCM. Ikulu ni mahali patakatifu, akiwa ikulu, rais wetu afanye kazi takatifu, hili la kuwaita watu ikulu yetu na kuwaomba wajiunge CCM, asilifanyie patakatifu pale, hili akalifanyie ofisi ya CCM Lumumba. Halileti picha nzuri kwa rais wetu, kwa sababu yeye sio rais wa CCM ni rais wa Watanzania wote.
3. Iwekwe faini maalum kwa kila kiongozi wa umma, atakayejiuzulu nafasi yake kwa sababu za kuhama chama, ikiwemo kukatwa mafao yake na ikibidi kufilisiwa ili kugharimia gharama za uchaguzi wa marudio kwa kulitia hasara taifa.
4. Viongozi wote wanaojiuzulu, wasiruhusiwe tena kugombea nafasi walizojiuzulu,kitendo cha kujiuzulu, kasha kugombea tena nafasi hiyo hiyo uliojiuzulu, ni kuwafanya wajinga, wale waliokuchagua.
5. Na kama vyama vimewaruhusu watu hawa waliotufanya wajinga kugombea tena, then natoa wito kwa Watanzania wenzangu, tusikubali kufanywa wajinga!. Tutangulize mbele maslahi ya taifa kwa kuwakataa, kama adhabu ya kutukataa na kulitia taifa letu hasara ya uchaguzi wa marudio.
6. Ila kama mapenzi yako kwa mgombea wa chama chako ni kitu cha muhimu zaidi kwako kuliko kutanguliza mbele maskahi ya taifa, hivyo chochote unacholetewa na chama chako hata kama ni ujinga, wewe utakichagua tuu, hivyo hapo, utakuwa umefanya chaguo lako, hivyo ni kuthibitisha Watanzania bado tunaweza kuletewa ujinga wowote na sisi tukauchagua ujinga huo!, na labda ndio maana mpaka sasa Watanzania tuko hapa tulipo!.
7. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kufuta chaguzi zote ndogo, na tuanzishe proportional representation kwa mwenye kura nyingi ndiye mshindi, lakini likitokea lolote, akasita kuwa rais, mbunge au diwani, yule aliyemfuatia katika uchaguzi uliopita ndio anatangazwa mbunge, kama hayupo anachuliwa mtu wa tatu, hadi wa mwisho, kama wote hawapo, ndipo uchaguzi mdogo unafanyika.
8. Kile kipengele cha kudhaminiwa na chama kiishie kwenye uteuzi tuu, kiongozi akiishachaguliwa, anakuwa kiongozi wa watu, anaweza kuhama chama bila kupoteza uongozi wake kama ilivyo nchini Kenya na nchi nyingine zenye kuheshimu demokrasia ya kweli na sio hii demokrasia fake ya vyama!.
9. Tubadili sheria yetu ya uchaguzi, kwa kuondoa kipengele cha kudhaminiwa na vyama ili kila Mtanzania mwenye sifa za kugombea uongozi wa nafasi yoyote, aruhusiwe, ila kwenye urais, tuweke vigezo vya ziada, ili asijetokea tajiri mmoja mwenye ukwasi wa kuwanunua watanzania wote, tukajikuta tuna rais wa kununuliwa. Ila kwenye ubunge, udiwani na serikali za mtaa, kila mtu awe free kugombea, hivyo tuwe na wagombea huru, na hili likifanyika hata sisi tusio na vyama tutashiriki, mfano mimi, naweza kabisa kugombea jimbo fulani na kulitwaa kama kuokota embe dodo lililojiangukia, ambapo mbunge wa hapo, nitamsukuma kama nimesukuma mlevi!.
Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.
Nawatakia Ijumaa Njema.
Paskali
Rejea.
Rev. Mtikila ashida kesi ya kuruhusu mgombea binafsi mahakama ya ...
Mtikila: Shujaa wa Demokrasia, Mwanamapinduzi halisi na Shujaa ...
Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini? | Page 9 | JamiiForums ...
Swali kwa Wana UKAWA: Is UKAWA for Real or Just A Marriage of ...
Pascal Mayalla
pascomayalla@gmail.com
Ufisadi wa kutisha mlikuwa hampigi kelele"Hitimisho.
Tanzania is too poor spend billions on by elections for foolish and nonsense reasons, nikimaanisha nchi yetu Tanzania ni masikini wa kutupwa, kuhalalisha matumizi ya mabilioni haya ya fedha kuendesha chaguzi ndogo kwa sababu za kuhama vyama. Ili Taifa letu lipate maendeleo ya kweli, ni lazima sisi Watanzania tukubali kuwa wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa na kufanya siasa za ukweli, tusiukubali huu ujinga wa kuhama vyama, uendelee kutugharimisha sisi masikini wa kutupwa, tunaishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, halafu kuendelea kugharimishwa.
Nawatakia Ijumaa Njema."
Paskali
Rejea.
Hili neno ni la maana sana "We are too Poor to play this stupid Game we are in now" kuna Binadamu pale kijijini anamaisha ya kutisha kuliko hata mbuzi wa Binadamu mwingine hapa mjini
....Sema kikundi fulani cha watu wanawaogopa wagombea binafsi na siyo nchi hairuhusu...Tukitoa hilo, maana yake huyo mtu ajidhamini hivyo itaruhusu watu binafsi kugombea, kitu ambacho nchi hairuhusu mgombea binafsi!
......Wewe lofa kwa nini unanakili uzi wote kwa hiyo mistari yako mitatu iliyojaa pumba?? Kwani ukimtaja Pasco kwenye new page na kuweka comments huko Lumumba hawatakuewa?Kipimo kiimoja wapo cha Demokrasia ni Uchaguzi Huru na wa Haki 'Independent and Fair Elections'
...Lazima usome kila uzi? Kama hili kwako ni kelele pita kimya,au nenda MMUMch mtikila alienda mahakamani wewe unashindwa nini kwenda mahakamani kwani kupiga kelele jf haitosaidia kitu.