Kipaji ni uwezo wa kufanya jambo juu ya uwezo wa wengi. Wanafunzi wanaoenda kwenye hizi shule kama MZUMBE, ILBORU , TABORA BOYS, KIBAHA, MSALATO, TABORA GIRLS n.k wengi wao wana uwezo mkubwa (kipaji) ama wa kufikiri au kukariri.
Kuna jamaa yangu alisoma TABORA BOYS alikuwa na uwezo wa kufikiri na ku solve swali la hesabu hata kama hajawahi kujifunza topic husika. Atatumia njia yoyote kulitatua swali.Alikuwa hasomi sana.
Jamaa yangu mwingine alisoma MZUMBE, Alikuwa na uwezo wa kukariri REVIEWS ZOTE maswali na majibu, yakiisha anatafuta mengine kwenye S.CHAND, google na hata shule jirani, yaani ukimletea swali linalofanana na lile alilowahi kuliona hakosi. Ila ukimletea jipya kulipata ni vigumu, hasa kama hana concept yoyote. Mda mwingi alikuwa anasoma na kutafuta maswali mengi na kukariri.
A talented student can either be a GENIUS, INTELLIGENT or BOTH.