"Shule za vipaji maalum" inamanisha nini hasa?

"Shule za vipaji maalum" inamanisha nini hasa?

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,057
Reaction score
10,731
Hii dhana ya shule za vipaji maalum, inanipa shida kidogo kutokana na sababu zifuatazo;

Ndio, wanachaguliwa walio na maksi za juu, lakini:

- Walimu wanaofundisha ni walewale kama wa shule za kawaida,

- Mtihani wanafanya uleule kama wa shule za kawaida na kushindanishwa ni kule kule kwa vigezo vile vile.

Huu ukipaji maalum, unahusu nini haswa?
 
Wale wanafunzi huwa wanaanza kupikwa huko kwa ajili ya matumizi ya Taifa hata waalimu wao huwa ni maalum.

Tufunge huu uzi.
unaposema walimu wao ni maalumu unamaanisha nini?
Alafu ni akina nani wanasimama kama mifano ya wanafunzi wenye vipaji maalum hata kwenye mambo ya teknolojia hapa kwetu, Africa Mashariki au Africa kwa ujumla?
 
Hivi mbali na kuangalia tu ufaulu wa wanafunzi kwenye mtihani wao waliofanya ni vipaji gani vingine vinavyoangaliwa kabla ya kumchagua mwanafunzi na kumpeleka kwenye hiyo shule ya "vipaji" maalumu? Maana bila ufaulu mzuri hata kama mwanafunzi anavyo vipaji vingine mfano kuimba, kupiga chombo/vyombo vya muziki, kukimbia, sarakasi n.k. hawezi kuchaguliwa kujiunga na shule hizo.

Badala ya kuitwa shule ya vipaji maalumu pengine zingeitwa shule kwa wenye ufaulu wa kipekee. Vinginevyo pasipo kuangalia ufaulu pekee yake wachukuliwe na wale wenye vipaji kama nilivyotaja hapo juu na kuwaweka pamoja ili kuleta maana halisi ya vipaji maalumu.
 
unaposema walimu wao ni maalumu unamaanisha nini?
Alafu ni akina nani wanasimama kama mifano ya wanafunzi wenye vipaji maalum hata kwenye mambo ya teknolojia hapa kwetu, Africa Mashariki au Africa kwa ujumla?
Wakati nakua mzee wangu alipenda niende shule moja hivi ya Vipaji maalum ila nilizembea nimekuja kujua alitaka nini tukiwa watu wazima.
 
Hivi mbali na kuangalia tu ufaulu wa wanafunzi kwenye mtihani wao waliofanya ni vipaji gani vingine vinavyoangaliwa kabla ya kumchagua mwanafunzi na kumpeleka kwenye hiyo shule ya "vipaji" maalumu? Maana bila ufaulu mzuri hata kama mwanafunzi anavyo vipaji vingine mfano kuimba, kupiga chombo/vyombo vya muziki, kukimbia, sarakasi n.k. hawezi kuchaguliwa kujiunga na shule hizo.

Badala ya kuitwa shule ya vipaji maalumu pengine zingeitwa shule kwa wenye ufaulu wa kipekee. Vinginevyo pasipo kuangalia ufaulu pekee yake wachukuliwe na wale wenye vipaji kama nilivyotaja hapo juu na kuwaweka pamoja ili kuleta maana halisi ya vipaji maalumu.
Kuna waalimu maalum katika shule hizi za kawaida pia ambao hutafuta wanafunzi maalumu waende huko kwa matumizi maalumu hasa Upigaji kura.
 
Hahahaa Mimi mwenyewe huwa nashangaa kuna shule flani ipo huku nyanda za juu nayo ni vipaji , ila mwanafunzi wakija hapo wanaongezewa na vipaji vya kubet
 
Hahahaa Mimi mwenyewe huwa nashangaa kuna shule flani ipo huku nyanda za juu nayo ni vipaji , ila mwanafunzi wakija hapo wanaongezewa na vipaji vya kubet
Hahahaha hao ni makapi kwenye nafaka. Huwa sio rahisi nafaka zote kuwa sawa.
 
Hii dhana ya shule za vipaji maalum, inanipa shida kidogo kutokana na sababu zifuatazo;

Ndio, wanachaguliwa walio na maksi za juu, lakini:

- Walimu wanaofundisha ni walewale kama wa shule za kawaida,

- Mtihani wanafanya uleule kama wa shule za kawaida na kushindanishwa ni kule kule kwa vigezo vile vile.

Huu ukipaji maalum, unahusu nini haswa?
Ni wale walio na ufaulu wa juu darasa la saba ili kuingia kidato.cha kwanza,na waliofanya vizuri kidato cha nne kuingia kidato cha tano,mf.mm darasa langu f.vpcm kibaha enzi hizo.wote walikuwa na div one from.olevel,na AAA za combination
 
Walimu ni wa kawaida tu na ukizembea unafeli kawaida tu!ndio maana kuna wanaofeli wachache kinachosaidia wengi ni msuli wa kufa mtu na ushirikiano,
 
Maana yake, ni shariti somo la HESABU ulijue kama unavyojua kuongea.[emoji23]
Jamani Member hili ndilo jibu SAHIHI kabisa
kuna kitu kinaitwa Pure Mathematic, Physics, Chemistry, Biology na Math ya kawaida na wanapewa waalimu pia vigongo maana wakizubaa wanaweza kufundishwa na haohao wanafunzi/
Hizi shule za siasa/siasa na kiswahili au Ualimu si za wataalamu (si za vipaji) ni kuwaandaaa wabwabwaji tu mitaani na kwennye vyama vya siasa CHUNGUZA
 
Simple sana
Kujua nini maana ya maalumu
Mwangalie mzee chenge ndio mfano mzuri wa maalum.
Wengi wa alumni wa special school wana uwezo mkubwa wa akili (akili kibongobongi inapimwa na performance in class though kwa wazungu kuna vitu kama SAT
 
Back
Top Bottom