Nadhani shule za Kikatoliki ndivyo zilivyo, jamaa wangu hufundisha pale Kristu Mfalme Tabata, wanapiga balaa. Usiogope, wale ni wataalamu na wanajua wanachofanya.
Usiogope, inawezekana mwanao unamdekeza sana, hajazoea kuchapwa au unaumia sana kuona anachapwa. Hakuna tatizo kwenye viboko vya adhabu, hayo ya saikolojia sijui blah blah ni ya wazungu.
Kumbuka watoto pia wana tabia ya kukuza mambo wanapokuwa wanashitaki, usiwatilie sana maanani, lakini usipuuze concern zao. Mfano kama anasema amepigwa sana muambie akuoneshe mahali alikochapwa, kama hakuna madhara yoyote ya kimwili basi hakuna la kuhofu.
Tatizo langu na shule za Kikatoliki ni ule mchezo ambao huwa wanawafanya watoto wa kiume huku tukiwavumilia kwa kuwa ni wawakilishi wa Mwana wa Mungu.
Karibu!