Shukrani zangu za dhati kwa wana JF

Shukrani zangu za dhati kwa wana JF

Pole sana KOKUTONA tu pamoja nawe katika kushiriki maumivu uliyonayo kwa sasa.Na Mungu azidi kukutia nguvu wakati huu mgumu kama nini.
 
Last edited by a moderator:
MUNGU akuzidishie Uvumilivu! Na hekima! Shukuru kwa kila jambo! We love you too!
 
Pole sana mpendwa wetu. Mungu Ataendelea kukupa faraja hai ambayo sisi kama binadamu hatuwezi. Imani yako ndiyo itakayokuvusha siku hadi siku. Ubarikiwe sana!

Ameen, ahsante. Mungu yu mwema.
 
Hakika Mwenyezi Mungu hampi mja wake mtihani ambao hawezi kuushinda.
Naamini huu ni mtihani tuu na kwa nguvu zake naamini utaushinda.
Tupo pamoja sana.

Ahsante sana. Nami naamini hataniacha.
 
Pole kwa yote mpendwa wetu KOKUTONA ..... Tunazidi kukuombea Mungu azidi kukupa faraja
 
Last edited by a moderator:
Kokutona, hatujawahi mimi na wewe kumuongelea huyu mwanao. Lakini nimeumia sana sana juu ya hili. Pole. Naogopa kusema nisije nikamkufuru Mungu. Ujasiri wako unanitoa machozi.

Pole tena.

Ujasiri huu King'asti ni Mungu mwenyewe. Na ninajitahdi sana kuzuia hali ninayoisikia pindi ninapokuwa idle. Sitaki kuwa idle maana nahisi ninaweza kufanya jambo tofauti nikaliza na wengine. Inauma na bado namlilia mwanangu kila iitwapo leo.
 
Last edited by a moderator:
KOKUTONA, Mungu alikuwa na uwezo wa kutokuliruhusu hili kutokea lakin je kwann ameruhusu hili litokee??

Mungu ni mwema sana na ninaamini furaha yako itazidi zaid siku utakapokuta mwanao kifuani mwa Abraham amelazwa pamoja na malaika, nina amini utafurah sana kwan utasema kwa ujasiri TALANTA NILIYOPEWA NIMEIZALISHA.

Kwasasa mshukuru Mungu, jitie moyo endelea kuomba ujasiri na faraja ya Kimungu huku ukikumbuka kwamba furaha uliyoipata siku ulipomzaa mwanao inatakiwa iwe sawa na shukurani unazotakiwa kumrudishia Mungu siku hii ambayo amemtwaa.

love you too dear.

Amen gfsonwin nimefarijika.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana maana yote tunamuachia mungu! ila nikumuomba mungu akufanye utoke katika mawazo yakuondokewa!
 
Back
Top Bottom