Mpendwa
KOKUTONA, narudia tena kusema sina cha kusema zaidi ya kumwombea mtoto wetu apumzike kwa amani. Bahati moja nzuri ni kuwa mtoto huyu amezikimbia tabu na mateso ya dunia iliyojaa uzandiki, dhuluma,fitina, majungu, ukatili, ubabaishaji, wizi na ufisadi na kuelekea mbinguni kuimba na malaika.
Pamoja na kwamba ametutoka duniani na kueleekea kwenye haki, amani na furaha bado haitoshi, kwa akili zetu binadamu kukubali ukweli huu. Inauma sana kushuhudia mtoto asiye na kosa anatangulia mbele ya haki akiyaacha mafisadi, majambazi, mabakaji, mauaji na majangiri yakijivinjari na kupafanya duniani pasiwe sehemu salama ya kuishi.
Pamoja na yote hayo.... Eee Mungu, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, lakini baba kama imekupendeza, basi mapenzi yako na yatimizwe.
Pole sana
KOKUTONA, mapenzi ya Mungu yametimia.
Bwana Ametoa, Bwana ametwaa, mapenzi yake yametimia.