Shukrani zangu za dhati kwa wana JF

Shukrani zangu za dhati kwa wana JF

KOKUTONA

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2011
Posts
8,651
Reaction score
6,109
Mungu ni mwema sana na ni waajabu pia, matendo yake hayaelezeki,yanatisha na wakati mwingine ukimtafakari sana unaweza usifike mwisho wa tafakari yako. Na mwisho uwaweza sema kweli Mungu ni wa ajabu au mwacheni Mungu aitwe Mungu na mengine meengi

Kipekee namshukuru sana Mungu kwani amenipa ujasiri wa ajabu saana sana. Nipo jamvini leo kutoa shukrani zangu za PEKEE kwa familia hii ya JF kwa upendo mkubwa mliuonyesha kwangu na kwa familia yangu baada ya kuondokewa na mwanangu kipenzi wa pekee.

Ilikuwa siku ya tar 10/03/2012 Jumaosi alasiri ndipo Mungu aliponijaalia mtoto huyu, siyo siri it was the happiest day in my life, nilifurahi na kumshukuru Mungu sana sana. Ndiyo safari ya maisha ya mwanangu ilipoanza. Nilijitahidi kwa kila nilichoweza na kwa kila nilichonacho kuhakikisha mtoto anakuwa na siha njema, Na kweli Mungu alimjalia afya njema sana. Na tar 10/03/2013 mwanangu alitimiza mwaka mmoja, na milimshukuru Mungu kuwa nimekuza kuza sasa.

Kama alivyoeleza babu Dark City kuna mlipuko wa ugonjwa usioleweka chazo uliingia wilayani kwetu, na tetesi zilisema watoto wengi wamekuwa affected but hawajonyesha symptoms. Mwangu alianzwa ghafla siku ya ijumaa, alipata treatment tukaruhusiwa kurudi nyumbani na alikuwa happy and healthy hadi jumamosi km saa moja hvi hali ilibadilika ghafla, tulirudi hospitali tukalazwa na akaanza kupewa matibabu, alionyesha matumaini alfajiri ya Jpili hali yake ilibadilika tena na kuwa mbaya zaidi hadi umauti unamkuta ahsubuhi ile kati ya saa 2-3.

Kipekee niwashukuru sana JF Tanga wing kwa moyo wa upendo waliouongesha kwangu regarless uchache wao. Waliweza kuniunganisha na wana JF wote ambao waliungana nami kuomboleza pamoja nao kipindi chote hadi leo, waliweza kuja kunishika mkono na kuuumia pamoja nami katika msiba huu mkubwa.Pia waliwezesha familia hii ya JF kuuniunga mkono kwa hali na mali na kwa faraja na upendo mkubwa. Nawashukuru sana babu Dark City, Mwanyasi, YNNAH, CHUAKACHARA na Arabela, sina cha kuwalipa. Mungu mwenyewe atanyosha mkono wake wa baraka na upendo.

Kipekee sana pia niwashukuru sana JF members woote kwa upendo mliouonyesha kwangu, mmekuwa faraja kubwa kwangu, familia yenye upendo usioelezeka, souce of my hope.

Nawashukuru sana kwa kujitoa kwenu, shukrani kwa waliopost post za kutia moyo kwenye thread aliyoanzisha babu Dark City, nilifarijika sana, shukrani pia kwa wote walioni PM kunipa pole, nawashukuru sana wote walinipigia simu na kunitext, wote mlinifariji sana sana, wapo pia walioweza kunitumia pesa kupitia kwa katibu wetu Tanga wing, niseme ahsanteni sana sana, Mungu akaongeze pale palipopunguzwa kwa ajili yangu.

Sina maneno ya kutosheleza shukrani zangu kwenu, maana maneno pekee hayatoshelezi na hayawezi kuonyesha faraja kubwa niliyonayo kutokana na upendo wenu mliouonyesha. Nawapenda sana sana. Mungu awabariki sana.
Salamu nyingi toka kwa mama, kaka, dada, wadogo zangu na ndugu zangu. Hawakuamini km watu wanaojuana mtandaoni wanweza kufanya makubwa haya. Wamefarijika sana

Rest In Peace my Son

Babu Dark City naomba unisaidie kuongezea, kwaniba ya kitukuu chako, na Tanga wing na JF kwa ujumla

Nilitamani sana kuwataja majina woote but najua na naaamini mtanielewa why sikuweza, ni wengi mmo. Na ndo maana nasema nashindwa niwashukuruje.

Msiba huu umenifundisha mambo mengi sana, nitakuja kutoa ushuhuda siku za usoni kwanini msiba hu umenifundisha makubwa sana na hasa kuwa na hofu ya Mungu na kumshirikisha kwa kila tufanyalo.

Again, I LOVE YOU ALL.

Tuendelee kupendana.
 
Last edited by a moderator:
Mungu ni mwema sana na ni waajabu pia, matendo yake hayaelezeki,yanatisha na wakati mwingine ukimtafakari sana unaweza usifike mwisho wa tafakari yako. Na mwisho uwaweza sema kweli Mungu ni wa ajabu au mwacheni Mungu aitwe Mungu na mengine meengi

Kipekee namshukuru sana Mungu kwani amenipa ujasiri wa ajabu saana sana. Nipo jamvini leo kutoa shukrani zangu za PEKEE kwa familia hii ya JF kwa upendo mkubwa mliuonyesha kwangu na kwa familia yangu baada ya kuondokewa na mwanangu kipenzi wa pekee.

Ilikuwa siku ya tar 10/03/2012 Jumaosi alasiri ndipo Mungu aliponijaalia mtoto huyu, siyo siri it was the happiest day in my life, nilifurahi na kumshukuru Mungu sana sana. Ndiyo safari ya maisha ya mwanangu ilipoanza. Nilijitahidi kwa kila nilichoweza na kwa kila nilichonacho kuhakikisha mtoto anakuwa na siha njema, Na kweli Mungu alimjalia afya njema sana. Na tar 10/03/2013 mwanangu alitimiza mwaka mmoja, na milimshukuru Mungu kuwa nimekuza kuza sasa.

Kama alivyoeleza babu Dark City kuna mlipuko wa ugonjwa usioleweka chazo uliingia wilayani kwetu, na tetesi zilisema watoto wengi wamekuwa affected but hawajonyesha symptoms. Mwangu alianzwa ghafla siku ya ijumaa, alipata treatment tukaruhusiwa kurudi nyumbani na alikuwa happy and healthy hadi jumamosi km saa moja hvi hali ilibadilika ghafla, tulirudi hospitali tukalazwa na akaanza kupewa matibabu, alionyesha matumaini alfajiri ya Jpili hali yake ilibadilika tena na kuwa mbaya zaidi hadi umauti unamkuta ahsubuhi ile kati ya saa 2-3.

Kipekee niwashukuru sana JF Tanga wing kwa moyo wa upendo waliouongesha kwangu regarless uchache wao. Waliweza kuniunganisha na wana JF wote ambao waliungana nami kuomboleza pamoja nao kipindi chote hadi leo, waliweza kuja kunishika mkono na kuuumia pamoja nami katika msiba huu mkubwa.Pia waliwezesha familia hii ya JF kuuniunga mkono kwa hali na mali na kwa faraja na upendo mkubwa. Nawashukuru sana babu Dark City, Mwanyasi, YNNAH, CHUAKACHARA na Arabela, sina cha kuwalipa. Mungu mwenyewe atanyosha mkono wake wa baraka na upendo.

Kipekee sana pia niwashukuru sana JF members woote kwa upendo mliouonyesha kwangu, mmekuwa faraja kubwa kwangu, familia yenye upendo usioelezeka, souce of my hope.

Nawashukuru sana kwa kujitoa kwenu, shukrani kwa waliopost post za kutia moyo kwenye thread aliyoanzisha babu Dark City, nilifarijika sana, shukrani pia kwa wote walioni PM kunipa pole, nawashukuru sana wote walinipigia simu na kunitext, wote mlinifariji sana sana, wapo pia walioweza kunitumia pesa kupitia kwa katibu wetu Tanga wing, niseme ahsanteni sana sana, Mungu akaongeze pale palipopunguzwa kwa ajili yangu.

Sina maneno ya kutosheleza shukrani zangu kwenu, maana maneno pekee hayatoshelezi na hayawezi kuonyesha faraja kubwa niliyonayo kutokana na upendo wenu mliouonyesha. Nawapenda sana sana. Mungu awabariki sana.
Salamu nyingi toka kwa mama, kaka, dada, wadogo zangu na ndugu zangu. Hawakuamini km watu wanaojuana mtandaoni wanweza kufanya makubwa haya. Wamefarijika sana

Rest In Peace my Son

Babu Dark City naomba unisaidie kuongezea, kwaniba ya kitukuu chako, na Tanga wing na JF kwa ujumla

Nilitamani sana kuwataja majina woote but najua na naaamini mtanielewa why sikuweza, ni wengi mmo. Na ndo maana nasema nashindwa niwashukuruje.

Msiba huu umenifundisha mambo mengi sana, nitakuja kutoa ushuhuda siku za usoni kwanini msiba hu umenifundisha makubwa sana na hasa kuwa na hofu ya Mungu na kumshirikisha kwa kila tufanyalo.

Again, I LOVE YOU ALL.

Tuendelee kupendana.

Pole tena, tuko na wewe kwa kila kitu.
 
Pole sana mpendwa wetu. Mungu Ataendelea kukupa faraja hai ambayo sisi kama binadamu hatuwezi. Imani yako ndiyo itakayokuvusha siku hadi siku. Ubarikiwe sana!
 
Pole sana KOKUTONA,

Tunaendelea kukuombea.... Mungu azidi kukupa nguvu na kukuimarisha...ili hatimaye umpe sifa kwa kila aliloamua kulitenda kwako na kwetu sote...

Bado sijapata maneno mdogo wangu..

Pia kwa niaba ya Tanga Wing, nawashukuru wadau wote ambao walituunga mkono, walioshiriki nasi kuomboleza na pia wale wale ambao wako nasi wakati wote katika safari hii ya kumtukuza Mungu..

Mungu awabariki wote na awaongezee upendo zaidi

Na above all, Mungu aendelee kuitwa Yehova na kupewa utukufu milele!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
KOKUTONA, undugu ni kufaana kama hivi. Kurudi kwako kutushukuru kuna maana kubwa sana kuwa pole tulizokupa hazijapotea bure. Asante sana na wewe na pole sana na msiba, Mungu atakusaidia kukuponya na maumivu unayoyapitia
 
Last edited by a moderator:
Kwa jinsi hiki kifo kilivyoniumiza realy sitaki hata kuiona ID yako KOKUTONA rafiki yangu mungu akupe nguvu mimi nisingeweza vumilia kwakweli.karibu sana
 
Last edited by a moderator:
Mpendwa KOKUTONA, narudia tena kusema sina cha kusema zaidi ya kumwombea mtoto wetu apumzike kwa amani. Bahati moja nzuri ni kuwa mtoto huyu amezikimbia tabu na mateso ya dunia iliyojaa uzandiki, dhuluma,fitina, majungu, ukatili, ubabaishaji, wizi na ufisadi na kuelekea mbinguni kuimba na malaika.

Pamoja na kwamba ametutoka duniani na kueleekea kwenye haki, amani na furaha bado haitoshi, kwa akili zetu binadamu kukubali ukweli huu. Inauma sana kushuhudia mtoto asiye na kosa anatangulia mbele ya haki akiyaacha mafisadi, majambazi, mabakaji, mauaji na majangiri yakijivinjari na kupafanya duniani pasiwe sehemu salama ya kuishi.

Pamoja na yote hayo.... Eee Mungu, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, lakini baba kama imekupendeza, basi mapenzi yako na yatimizwe.

Pole sana KOKUTONA, mapenzi ya Mungu yametimia.
Bwana Ametoa, Bwana ametwaa, mapenzi yake yametimia.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom