Shukrani zangu kwenu

Shukrani zangu kwenu

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,152
Nawashukuru wale woote wanaoniunga mkono katika kusaidia vijana ambao hawana ajira ili waweze kujitambua kwa kutafuta mbinu mbadala mbalimbali ambazo zitawasaidia kujikwamua katika hali ngumu ya maisha achilia mbali degree zao au elimu zao ambazo wanazo. Baada ya kupost ile thread iliyosomeka " ushauri kwa vijana ambao wanatafuta ajira" nimepokea email nying sana kwa vijana ambao walionesha nia ya dhat katika kujikomboa kifikra mpaka sasa nimefanikiwa kuwasaidia vijana wawili 1mdada, na mwingine mkaka. ilikua hivi;baada ya kuchat nao kwa muda sana niliona ni kweli wana maanisha mmoja ametokea mwanga kilimanjaro na mwingine ametokea hapahapa arusha. mdada anafanya kazi katika sheli ya panone hapa arusha shahara 95,800/= anapewa chakula na mkaka anasimamia store yaan storekeeper katika kampuni inayoitwa arusha sundries mshahara ni 150,000/= anapewa nauli chakula ni yeye hapa arusha.mdada nimemdhamini anaishi kwangu kwa miez 3, mkaka yupo kwa uncle wake. wote wana degree, nimewaomba waje huku jf wawashuhudie members wengine ili wayaamini haya. otherwise, natoa shukrani zangu za dhati kwa kuniamini na kuniunga mkono katika harakati za kupigana na maisha hasa hili suala la kuweka degree chini na kufanya kile unachoona ni sahihi kwako bila kuchagua ili mradi kiwe halali..naomba tuendelee kushirikiana kwa hili, nawaombea hawa waliojitoa kwa moyo kufanya kazi hizi, nawaombea kila la kheri Mungu awajaalie uhai na maisha marefu ili waje kuwa ushuhuda kama mimi.kile mnachoona kinawasaidia kichukueni ila kile kisichofaa kinachopotosha achaneni nacho hasa mawazo ya watu wanaokatisha tamaa.Mungu awabariki woote, pamoja sana. amelinechao@gmail.com
 
Heshima kazi na ukiwa mwanaume wa kweri hakikisha nyumbani wanapata ugari tufanye kazi jamani hata zege me mbna nipo kwnye site kwa siku napata 15 elfu
 
Heshima kazi na ukiwa mwanaume wa kweri hakikisha nyumbani wanapata ugari tufanye kazi jamani hata zege me mbna nipo kwnye site kwa siku napata 15 elfu

keep it up brother!
 
... mdada anafanya kazi katika sheli ya panone hapa arusha shahara 95,800/= anapewa chakula na mkaka anasimamia store yaan storekeeper katika kampuni inayoitwa arusha sundries mshahara ni 150,000/=.....

wote wana degree...... amelinechao@gmail.com

mi naomba nisiwe mnafiki katika hili,is this fair? ina maana maisha yamekuwa magumu kiasi hiki? hii inatuambia nini tunaotafuta hivi videgree,kwamba tutaenda kupewa elfu 95? na wa adv diploma,diploma,certificates etc? natofautiana na nyie mnaomuona huyo jamaa ni shujaa.
 
Mmh huyo mdada anayeishi kwako ni kwa terms gani? ndiyo umevuta kumfanya kuwa mkeo au mambo hayo yakoje?
 
hii ni kuidhalilisha elimu ya Tanzania otherwise degree zao cjui wamezipata chuo gani??? hili nalo ni la kujiuliza ,... anyway ya Mungu mengi,.. nawatakia kazi njema ,.. lakini wabadilike sasa,..,
 
@ Pena United umetoa pointi inamaana haina haja ya kusoma basi maaana hata mtu wa x7 he/she can do such a job
 
Nawashukuru wale woote wanaoniunga mkono katika kusaidia vijana ambao hawana ajira ili waweze kujitambua kwa kutafuta mbinu mbadala mbalimbali ambazo zitawasaidia kujikwamua katika hali ngumu ya maisha achilia mbali degree zao au elimu zao ambazo wanazo. Baada ya kupost ile thread iliyosomeka " ushauri kwa vijana ambao wanatafuta ajira" nimepokea email nying sana kwa vijana ambao walionesha nia ya dhat katika kujikomboa kifikra mpaka sasa nimefanikiwa kuwasaidia vijana wawili 1mdada, na mwingine mkaka. ilikua hivi;baada ya kuchat nao kwa muda sana niliona ni kweli wana maanisha mmoja ametokea mwanga kilimanjaro na mwingine ametokea hapahapa arusha. mdada anafanya kazi katika sheli ya panone hapa arusha shahara 95,800/= anapewa chakula na mkaka anasimamia store yaan storekeeper katika kampuni inayoitwa arusha sundries mshahara ni 150,000/= anapewa nauli chakula ni yeye hapa arusha.mdada nimemdhamini anaishi kwangu kwa miez 3, mkaka yupo kwa uncle wake. wote wana degree, nimewaomba waje huku jf wawashuhudie members wengine ili wayaamini haya. otherwise, natoa shukrani zangu za dhati kwa kuniamini na kuniunga mkono katika harakati za kupigana na maisha hasa hili suala la kuweka degree chini na kufanya kile unachoona ni sahihi kwako bila kuchagua ili mradi kiwe halali..naomba tuendelee kushirikiana kwa hili, nawaombea hawa waliojitoa kwa moyo kufanya kazi hizi, nawaombea kila la kheri Mungu awajaalie uhai na maisha marefu ili waje kuwa ushuhuda kama mimi.kile mnachoona kinawasaidia kichukueni ila kile kisichofaa kinachopotosha achaneni nacho hasa mawazo ya watu wanaokatisha tamaa.Mungu awabariki woote, pamoja sana. amelinechao@gmail.com

Nataka nikuthibitishie kuwa hakuna hata mmoja uliyemsaidia kama unavyosema. Nimejaribu kusoma post zako kwa makini, unajaribu kujiridhisha tu, na kupima upepo wa ajira ukoje.
Natambua fika, hapo ulipo hakijaeleweka so una test ili kutambua umati ulioko pamoja nawe ni mkubwa kiasi gani. Pole.
 
Back
Top Bottom