Shukrani za dhati

Shukrani za dhati

Mariangonyani

Member
Joined
Mar 31, 2013
Posts
39
Reaction score
59
Napenda kushukuru jf sanasana Asha D , Fixed point , maxence melo, kaunga , riwa , mwa j ,kipipi , blacki woman , mtambuzi , erickb52 na niliowasahau mmefanya nione kuwa na vvu si mwisho wa maisha kwani ilikuwa ngumu sana kukaa nalo moyoni bila familia yangu kujua kupitia nyinyi nimekuwa wazi kwenu na mmenisaidia sana kimawazo na kifedha pia, nawashukuru sana mmefanya nikubali hali yangu napitia changamoto nyingi ila mnanisaidia kama tujuavo kumsaidia usiyemjua ni kazi ila nyinyi mmeweza . Nawapenda sana na mungu awe nanyi
 
Hongera kwa kuweza kukabiliana nalo kwa kiasi hicho.

Ubarikiwe!
 
Napata faraja kuona shukrani. Kila mara kuna watu lukuki wanaomba ushauri,wadau wanatumia muda wao na gharama zao kuwashauri. Baada ya ushauri, watu hao hawarudi kutoa shukrani au kueleza mafanikio yao. Hii imenifanya kuamini hili ni Jukwaa la kuoma ushauri na Elimu, bila ya kujua hatima ya ushauri na Elimu iliyotolewa. Ilifika nahali nikahisi mikasa inayoletwa huku ni ya kutungwa chini ya miti, jamii ya E. Shigongo.
Wakristo kumbukeni Yesu aliposema, "Je si kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi? (Lk. 17:17).
 
well n good...kwani kuna link ya kuomba mawazo uliwahi kuiweka? Naomba hiyo Link tafadhali
 
Mungu analengo nawewe ndugu yangu hongera kwa ujasiri,ila ukisoma yeremia32:27 hamna lisilo wezekana kwa Mungu,hajasema anaponya magonjwa yote isipokua hiv kama unaamuamin yesu nitafute kuna mtumishi kawaombea watu wakapona kabisa hiv nakua -ve
 
Napenda kushukuru jf sanasana Asha D , Fixed point , maxence melo, kaunga , riwa , mwa j ,kipipi , blacki woman , mtambuzi , erickb52 na niliowasahau mmefanya nione kuwa na vvu si mwisho wa maisha kwani ilikuwa ngumu sana kukaa nalo moyoni bila familia yangu kujua kupitia nyinyi nimekuwa wazi kwenu na mmenisaidia sana kimawazo na kifedha pia, nawashukuru sana mmefanya nikubali hali yangu napitia changamoto nyingi ila mnanisaidia kama tujuavo kumsaidia usiyemjua ni kazi ila nyinyi mmeweza . Nawapenda sana na mungu awe nanyi

Sister hilo ni jina lako la kweli? Kama ndio naomba uni PM nafikiri nakukumbuka.
 
sorry hapo juu ni hakuna linaroshindikana kwa Mungu kama una amin nichek 0686399397
 
well n good...kwani kuna link ya kuomba mawazo uliwahi kuiweka? Naomba hiyo Link tafadhali

Hili jina lake sio geni, kulikuwa na bandiko lake mwaka jana ingawaje sikumbuki ilikuwa ni kutamfuta mchumba au ilikuwa ni habari ya kuomba ushauri...

Hata hivyo Mungu akutie nguvu bi dada, kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa shughuli...
 
Pole mi nikiupata sijui kama ntapona, aisee mawazo yataniua kabla ya siku zangu. Hongera kwa kuwa na ujasiri wa hali ya juu.
 
Back
Top Bottom