kwani siku hizi 'walipiga marufuku' kwenda kutoa miahadhara pale (au vyuo vingine)!Nilipokuwa UN tulikuwa tunahimizwa na Katibu Mkuu wetu Kofi Annan kukutana na vijana MTV. Ni utamaduni ambao nimeona unaweza ukatufaa pia Tanzania. Pia kizazi changu tulimshuhudia Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere akifika mara kwa mara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuongea na wanafunzi na walimu. Chuo kilikuwa kimoja. Sasa ni vingi. Jamvi linatusaidia kuwafikia kwa pamoja. Wanasema "technology shapes institutions". Tunakwenda na wakati.
Nakupongeza sana kujiunga Jamvini ambako najua utaweza pata changamoto zinazo husu wizara yako na Jimbo lako. Swali langu ni je? TOKEA UCHAGULIWE KAMA MBUNGE WA MULEBA KUSINI NI KWA KIWANGO GANI UMETEKELEZA AHADI ZAKO? KAMA WAZIRI WA ARDHI: NINI MSIMAMO WAKO KUHUSU MGOGORO WA MRADI WA UUZWAJI WA VIWANJA KATIKA MANISPAA YA BUKOBA? Katonda akuwe amaani akwongeze Ekisha kyo kwenda abantu bawe.WanaJF
Walionikaribisha Ninawashukuru. Sikutegemea wala kustahili ukarimu huu. Asanteni sana.
Walioona sistahili - Ninawapongeza kusema ya moyoni mwao.. Naomba mnikubali kama siyo kwa nafsi yangu, kwa sababu nyie kama mimi ni waumini wa demokrasia ya kweli. Kila mtu awe na haki ya kushiriki katika Jukwaa hili. Hata wa miaka 47 tunaweza tukaleta ya historia ambayo ndiyo hujenga ya kesho. Wenzetu wanasema A people with no history have no future.
Na mbona nimechelewa wengine wamehoji? Ni kweli. Ila, nadhani ni vyema kutambua kwamba Jukwaa hili, wengi wenu mkiwa vijana, ilibidi lipewe nafasi kukua na kuchanua kabla watu kama mimi hatujaingia na mawazo ambayo labda yangelifanya kusinyaa. Sasa limekomaa, hoja na maswali muhimu yanajitokeza kwa hiyo tunaweza tukajibu inapostahili. Ninawapongeza waanzilishi na Gold Members. Hongereni sana.
Imeulizwa, je nitashiriki mara kwa mara?
Wakati ninaomba moderator anisaidie kukusanya maswali yenu yote yanayohusu kazi yangu, na nitakuwa ninayajibu baada ya kufanya utafiti ili nilete evidence based reporting katika jamvi letu, kwa sasa niseme tu katika dunia ya leo, viongozi hatuna budi kuwa kwenye majukwaa ya wananchi hasa vijana, taifa la leo na kesho.
Nilipokuwa UN tulikuwa tunahimizwa na Katibu Mkuu wetu Kofi Annan kukutana na vijana MTV. Ni utamaduni ambao nimeona unaweza ukatufaa pia Tanzania. Pia kizazi changu tulimshuhudia Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere akifika mara kwa mara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuongea na wanafunzi na walimu. Chuo kilikuwa kimoja. Sasa ni vingi. Jamvi linatusaidia kuwafikia kwa pamoja. Wanasema technology shapes institutions. Tunakwenda na wakati.
Kazi ni nyingi ninaweza kuchelewa kujibu hoja zenu ila kwa msaada wa mode nitajitahidi.
Mbarikiwe. Pamoja tunaijenga Tanzania imara leo na kesho.
Mama Tibaijuka
WanaJF
Walioona sistahili - Ninawapongeza kusema ya moyoni mwao.. Naomba mnikubali kama siyo kwa nafsi yangu, kwa sababu nyie kama mimi ni waumini wa demokrasia ya kweli. Kila mtu awe na haki ya kushiriki katika Jukwaa hili. Hata wa miaka 47 tunaweza tukaleta ya historia ambayo ndiyo hujenga ya kesho. Wenzetu wanasema A people with no history have no future.